Naomba kuuliza kuhusu chimbo zuri la kununua mitumba balo za mitumba

Naomba kuuliza kuhusu chimbo zuri la kununua mitumba balo za mitumba

Mi sio mtaalam lakini nimeona nitue nishee kidogo nnachojua.

Japo mitumba Iko tofauti tofauti.....nguo za watoto,za wakubwa, ...kariakoo mtaa wa narung'ombe...... Na mingine mnazi mmoja. Ila ukiweza kununulia mzigo wako godown usiende kwenye hayo maduka ni nafuu kidogo maana mizigo wanashusha godown na kuanza kusambaza kwenye maduka yao.
 
Somo zuri sana.Nilikuwa nataka kuanza biashara ya mitumba mwaka huu naomba kuuliza n sehemu gan wanapouza nguo za mtumba za kike grade A zinazoendana na fashion?naomba ushauri wako
 
Umeelezea vizuri hii bishara, mimi kuna siku nilipita eneo linauza viatu vya mtumba vimepangwa chini, nikaona raba mbili kali sana ikabidi nisogee, kuuliza bei jamaa akaniambia nimpe 12,000 tukaongea pale nikamuambia nachukua 2 kwa nusu bei ila akakaza sana tukafikia bei 7,500 kwa pea na vipo ktk condition nzuri kabisa.

Raba zilikuwa ni Air Jordan 1 Low na Yeezy Boost 350 V2 kwa ile bei sikutaka kuviacha kabisa.

Sasa ulivyoelezea hao mawinga ndiyo nimeelewa maana kuna jamaa ana frame yake huwa anauza mtumba na raba kama Air Jordan 1 ni kuanzia 40,000.

images.jpeg-8.jpg


images.jpeg-6.jpg
 
Habari za muda huu wanajua ii. Gt na professionals wa mambo mbalimbali. Poleni Kwa kadhia, hasa wale wanaosumbuliwa na mapenzi, ajira na siasa. Niseme tu tuendelee kupambana, hamko peke yenu.

Nimeona Kuna uhitaji mkubwa wa watu kufahamu biashara ya mitumba kwani wengi wetu wamekuwa wanaulizia Mara Kwa mara na wengine kutoa baadhi ya wanachokijua kujibu maswali Kwa wasiojua. Nianze kwa kusema kwamba hili la majibu mafupi na uhitaji wa Kujua limenisukuma niandike haya.

Mitumba si biashara rahisi kama tunavyofikiria. Ina utaalamu mchache ambao ni Basic. Utaalamu huu ndio unanisukuma kuandika machache.

Kwanza kabisa, wauza mitumba wapo wa Aina nyingi. Kuna suppliers, ambao wananunua robota 20,10 au 50 Kwa wahindi na kuweka mzigo stoo na kuuza kwa WAFUNGUAJI. Kwa namna hiyo, mnyororo wa Belo unaweza kupita mikono zaid ya mitatu mpaka Belo kumfikia anaefungua Belo kuuza nguo Kwa wavaaji/wuazaji.

Mfunguaji (mfungua Belo) ni mfanya biashara ambae anaweza kuwa na mtaji Kati ya laki 5 (Belo 1/2 kutegemew na uzito au bei Husika) ambae anamiliki kizimba (sokoni n. K) anetegemea Sana kuuza nguo moja moja Kwa wateja wa Aina 3. Napendekeza ukiwa na mpango wa kufungua Belo wateja hawa uwe nao. Hapa nitazungumzia Mtumba grade 1.

1. Mteja wa JUMLA
Ni lazima ukubali kwamba, nguo za mitumba zinaweza kutoka Belo moja lakini ubora ukatofautiana. Kuna nguo unaweza kuuza Kwa elfu 10 (tisheti hii bei ni kubwa mno), Kwa jinzi (ukauza mpaka elf 30). Lakini Belo hilohilo litakupa nguo ambayo hata elfu 1 Mia tano huuzi. Hivyo kadri unavyouza lazima uwe na utambuzi wa bei halisi ya nguo iliyo mkononi. Usikatae kuuza elfu 10 ukaione nzur Sana ukaja kuiuza elfu 7 upate hela ya kula kwanza.Au kinyume chake, ukauza nguo elf 10 kumbe hata elfu 25 ungeuza.

MTEJA WA JUMLA NI YULE ANAEKUJA KWAKO KUNUNUA NGUO ZOTE ZILIZOBAKI MKONONI/KIZIMBANI MWAKO,ILI AKAZIUZE (HAWA MARA NYINGI WANA MWAGA CHINI AIDHA KANDO YA BARABARA AU MINADANI) . Mara nyingi Kwa tisheti wananunua bei ya jumla Kati ya 700 mpaka 1300 inategemea na mapatano.

2. MAWINGA (MAPOINTA)
Hawa pia ni wateja muhimu Sana unapofungua Belo. Ni viungo muhimu Sana kuchagua NGUO KALI kutoka kwenye Belo lako wakauze. Hawa huwa na tabia ya kuchagua Sana, kwenye nguo 300 katika Belo lako ni kawaida kupata nguo 3, 4 au 10 usiawchoke. Wanakuaga na "strong negotiation skills". Wasumbufu. Ila ni muhimu kwani wanasaidia Sana kukutoa kwenye msongo wa kutokuuza, mzigo mbaya au wanakubusti kurudisha mtaji kwani wanaoweza kusababisha ukarudisha nusu ya hela yako mapema mno. Kwa tisheti wengi wapo Nje ya jengo la CHINA PLAZA. Wanakuaga na MAGOLI yao. Kwa tisheti huwa wananunuaga Kati ya elf 5 mpaka 8.

PIA, MAPOINTA, wengine wanaitwaga MAWINGA hawa ni watu ambao hawanunui nguo kwako. Hawa wanaleta mteja kizimbani kwako na kuuza kama za kwao. Ni wazuri pia kuropoka bei. Tisheti ya elf 5 wanaoweza kumropokea mteja kuwa bei ni 12. Ni moja Kati ya watu wanaoharibu biashara za mitumba sokoni zinaonekana ghali. Karume na ilala wamejaa Sana hawa. Ni wa muhimu ila hutakiw kuwaamin, wanaoweza kukudhulumu au kuiba. Lakini pia, ikitokea unawaamini unaweza kuwapa nguo wakauze wakulete hela. Kuwajua pia kunahitajika apa. Wanakuaga na uwezo wa kuuza idadi nyingi ya nguo kuliko mwenye Mali yako. Very potential.

3. WAVAAJI
Hawa ni watu kam mimi na wewe. Ambao wanapita au wanvutiwa Kuja kununua. Hawa wanaoweza kuuziwa na wewe au mawinga. Mara nyingi huwa hatuwajali Sana sabab WANAPITA TU. tunaweza kubambika nguo zilizotoboka wasipoona. Ni biashara, ni rizki. Lakini pia wakijenga uaminifu na kurudi rudi huwa tunawachagulia saizi nzur/dizaini wanazopenda tunawtunzia au kuwapigia simu waje kuziona/ kununua.

Aina nyingine ya wauza mitumba ni hawa MAWINGA /MTUKATI /MAPOINTA. hawa Mara nyingi huwa wanachagua nguo chache NZURI TU. Wanakuaga na teknik za kuchagua nguo nzur Kwa JICHO LA MTEJA. hawa ndio ambao tunawakuta wamebeba nguo mkononi kando kando ya barabara au kukuleta majumbani wengine wanaposti mitandaoni (what's ap status, insta nk). Tabia yao kubwa ni kununua nguo nzur tu (Kam nlivyoeleza). Hawana mitaji mikubwa hawa hata elf 50 inawatoshaga. Pia muda mwingine wanalindwaga na uaminifu tu, wanapewa wakauze walete hela.

Aina ya mwisho ya wauza mitumba ni WAUZA JUMLA. Hawa jamaa huwa na kelele kweli kweli. Kokte wakikaaga hawa lazima kuwepo na kelele za kutangaza biashara yao. Hawa wanatumia hesabu za paukwa pakawa. Mfn. Wananunua tisheti bei ya jumla (nimewaeleza juu hapo Kam wanunuzi wa jumla) Kwa kiasi cha shilingi 800 au 900 Kwa tishet 1 kwa mana tishet 350 *900 (bei) = na Laki 4 mfano. Wanazobeba kwenda kuzimwaga chini na kunadisha elfu tatu 1 (ndani ya siku 2). Mfano umeuza tisheti 80 *3000= na Laki 3 na 20. Siku ya tatu unaanza kunadisha Kwa elfu mbili mbili na kuuza tisheti (260 zilizobaki). Unauza elf mbili-mbili tishet 100 (ndani ya siku 2) Sawa na laki tatu. Siku inayofata unaanza kuuza bukubuku. Tu nategemea kupata faida nyingi Kwa kadri tunavyoshusha bei kila siku Kwa sabb ya kulindwa na yile bei iliyoanza kutumika Mara ya kwanza kabisa. Ukisharudisha mtaji zinazobaki hata Mia tano-tano unauza tu.

NB: HAKUNA UWEZEKANO WA KUUZA TISHETI ZOTE.

HAWA WOTE WANAWEZA KUWA WAUZAJI WA JUMLA KULINGANA NA MASLAHI YAO. SAMAHININI KWA MUANDIKO MBOVU WENYE UHITAJI KARIBUNI HAPAHAPA JUKWAANI KWA KUTAKA UELEWA ZAIDI
Haya kila kitu hadharani
 
safi sana kaka, mimi nipo karagwe mkoa wa kagera, baada ya kupata changamoto kwenye biashara ya vifaa vya simu na m-pesa Nimefikiria mwaka huu nifanye biashara ya mtumba kwa kuanza na Tshirt kufungua belo grade 1 pamoja na simple jacket , maana kwa huku naona biashara ya mtumba bado iko chini sana wengi wao wanaleta nguo ambazo hazina quality kabisa mf. mm binafsi ni mpenzi wa tshirt za mtumba ila huwa nanunua mwanza mlango mmoja au dar ilala au kama ni kampala huwa nanunua pale stendi ya Gisan maeneo ya Hyper market ila huwa nanunua za kuvaa tu.
1. wapi ntapata bero la Tshirt grade 1 ( korea)??
2. Je nianze kwa kufungua belo au nianze kwa kupoint kutoka mwanza mlango mmoja??
3. Nilikuwa nimepanga nitafute frem ili niwe nauzia hapo na zile za quality ya chini nampa kijana kwaajiri ya kutembeza
ushauri plz
 
safi sana kaka, mimi nipo karagwe mkoa wa kagera, baada ya kupata changamoto kwenye biashara ya vifaa vya simu na m-pesa Nimefikiria mwaka huu nifanye biashara ya mtumba kwa kuanza na Tshirt kufungua belo grade 1 pamoja na simple jacket , maana kwa huku naona biashara ya mtumba bado iko chini sana wengi wao wanaleta nguo ambazo hazina quality kabisa mf. mm binafsi ni mpenzi wa tshirt za mtumba ila huwa nanunua mwanza mlango mmoja au dar ilala au kama ni kampala huwa nanunua pale stendi ya Gisan maeneo ya Hyper market ila huwa nanunua za kuvaa tu.
1. wapi ntapata bero la Tshirt grade 1 ( korea)??
2. Je nianze kwa kufungua belo au nianze kwa kupoint kutoka mwanza mlango mmoja??
3. Nilikuwa nimepanga nitafute frem ili niwe nauzia hapo na zile za quality ya chini nampa kijana kwaajiri ya kutembeza
ushauri plz
Oke, kama una uzoef wa kupoint ni bora ufubgue la kwako mana huwezi point mzigo wa kutosha Kwa siku moja. Pia kama una plan ambayo itakupa muda na uwezo wa kuajiri watu wengine fungua Robota lako. Robota unaweza chukua mnazi mmoja pale Kwa jamaa angu anaitwa amiri. Atakuuzia bei nzur tu. Lakin pia unaweza kwenda bazaar kule Tazara karibu na tbc. Kama unaweza pia kupata hapo mwanza kachukue Robota. Uwe na plan ya zile zinazobakia utazipeleka wapi kama kwenye minada au wapi. Mm naona kuchukua Robota risk ni kubwa ila pia faida huwa nzuri. Lakin pia kama utakuwa na mapointa itapendeza zaidi
 
Mkuu naomba mawasiliano yako maana umelimit view katika profile yako 🙏
 
Wakuu naomba mnisaidie mawasiliano ya simu ya muuzaji wa mitumba ya nguo za kike Dar.
Naomba mnitumie JF inbox au normal sms 0624573133
 
safi sana kaka, mimi nipo karagwe mkoa wa kagera, baada ya kupata changamoto kwenye biashara ya vifaa vya simu na m-pesa Nimefikiria mwaka huu nifanye biashara ya mtumba kwa kuanza na Tshirt kufungua belo grade 1 pamoja na simple jacket , maana kwa huku naona biashara ya mtumba bado iko chini sana wengi wao wanaleta nguo ambazo hazina quality kabisa mf. mm binafsi ni mpenzi wa tshirt za mtumba ila huwa nanunua mwanza mlango mmoja au dar ilala au kama ni kampala huwa nanunua pale stendi ya Gisan maeneo ya Hyper market ila huwa nanunua za kuvaa tu.
1. wapi ntapata bero la Tshirt grade 1 ( korea)??
2. Je nianze kwa kufungua belo au nianze kwa kupoint kutoka mwanza mlango mmoja??
3. Nilikuwa nimepanga nitafute frem ili niwe nauzia hapo na zile za quality ya chini nampa kijana kwaajiri ya kutembeza
ushauri plz
Mm niko kayanga hapa tuchekiane mkuu
 
Nguo kali za mitumba grade A, Cream kabisa, za kike na za kiume.

Wanawake.
1. Mashati ya ofisini.
2. Mashati casual.
3. Form 6.
4. Jeans mkataba.
5. Pensi.
7. Flana.
9. Cardet.
10. Suaruali za vitambaa.

Wanawake.
1. Magauni ya sherehe.
2. Madira.

Nicheki #0623123369 wasap nikuunge group au unaweza ukaingia moja kwa moja.

 
Nguo kali za mitumba grade A, Cream kabisa, za kike na za kiume.

Wanawake.
1. Mashati ya ofisini.
2. Mashati casual.
3. Form 6.
4. Jeans mkataba.
5. Pensi.
7. Flana.
9. Cardet.
10. Suaruali za vitambaa.

Wanawake.
1. Magauni ya sherehe.
2. Madira.

Nicheki #0623123369 wasap nikuunge group au unaweza ukaingia moja kwa moja.

Only admins can send messages. Mnaficha nini huko mpaka mzuie watu wengine wasitume texts na ukizingatia ni kundi la biashara? P
 
Nimesha wahi pigwa ndoige moja zamani kwenye hii bznec sina hamu! Tunaenda nunua watu kama kumi hivi ila mimi nikifungua nakutana na matambara hamna cha maana 2M iliteketea
 
Only admins can send messages. Mnaficha nini huko mpaka mzuie watu wengine wasitume texts na ukizingatia ni kundi la biashara? P
Hamna mkuu, nilifunga kwa sababu kuna watu walikua wanashare mambo ya hovyo so nikalifunga kwa muda tu ila mostly group linakuwa wazi
 
Nimesha wahi pigwa ndoige moja zamani kwenye hii bznec sina hamu! Tunaenda nunua watu kama kumi hivi ila mimi nikifungua nakutana na matambara hamna cha maana 2M iliteketea
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Na unakuwa ulichagua mwenyewe au walikuchagulia
 
Back
Top Bottom