Naomba msaada kuhusu hedhi.

Naomba msaada kuhusu hedhi.

bishankara

Senior Member
Joined
Feb 21, 2012
Posts
140
Reaction score
8
Habr za usiku wapendwa. Naomba kufahamu siku salama kwa msichana ambaye ameingia hedhi tarehe 08.
 
Siku zote ni salama kasoro siku ya 14 toka hedhi inaitwa fertile day or at risk day hata hivyo chukua tahadhari siku tatu nyuma na siku tatu mbele kwa ni sperm zinakaa hadi 72hrs kama pH medium za mwanamke na mwanamme zinalinga.
 
Umemjibu vema ila umewahi kujibu kwa kutumia circle ya siku 28. Ikumbukwe kuwa kuna mizunguko ya aina tatu toofauti, kuna mzunguko wa siku 21,28 na 35 sasa sijui huyo msichana wake ana mzunguko wa siku ngapi. Na pia ikumbukwe kuhesabu tunaanza siku ya kwanza mwanamke alipoona siku zake.
 
Umemjibu vema ila umewahi kujibu kwa kutumia circle ya siku 28. Ikumbukwe kuwa kuna mizunguko ya aina tatu toofauti, kuna mzunguko wa siku 21,28 na 35 sasa sijui huyo msichana wake ana mzunguko wa siku ngapi. Na pia ikumbukwe kuhesabu tunaanza siku ya kwanza mwanamke alipoona siku zake.

Asante kwa majibu mazuri sana, yeye ni siku 28, lakn naomba kujua je kama ameanza tar 08 tunahesabu tarehe 08 kuwa siku ya kwanza au tunachukua mtindo wa masaa 24 kwamba kama ni tar 08 saa 2asb basi siku ya kwanza inahesabika kukamilika ifikapo tar 09 saa 2 asbh au tar 09 ni siku ya pili?
 
Tunachukua tarehe hatuko certain sana na masaa ila siku ina masaa 24.

Note: mwili sio kama mashine kwa hiyo kunaweza kuwapo na mabadiliko ya hapa na pale
 
Tunachukua tarehe hatuko certain sana na masaa ila siku ina masaa 24.

Note: mwili sio kama mashine kwa hiyo kunaweza kuwapo na mabadiliko ya hapa na pale
 
Hii makitu ngum sana...mie na wife leo nusura tuzichape. Mi nilidhani shampa mimba leo kavuja nanihii...yaani kidogo tu tungezichapa. Hii sijui kalenda sijui nini ni ujinga mtupu.
 
Habr za usiku wapendwa. Naomba kufahamu siku salama kwa msichana ambaye ameingia hedhi tarehe 08.

1.Siku salama ni tarehe 13,14,15,16,17 endapo hedhi yako ni siku tatu mpaka tano awamu ya kwanza.
2.Awamu ya pili ni tarehe 27,28,29,30,"31" 1,2,3,4,na tarehe tano. Hapo kati ya tarehe 5 na tarehe 6 ni hedhi ya mwezi unaofuata, kutegemea na idadi ya siku katika mwezi uliotangulia.

Aljebra hii ni kwa binti mwenye mzunguko wa siku 28. By MSAKI.
 
kama ameingia hedhi tarehe 8 na kama mzunguko wake ni wa siku 28 basi siku salama kwake zitakua ni;
-tarehe 08 hadi tarehe 19 kisha tarehe 26 hadi tarehe ya mzunguko ujao
NB;hapo siku anazobleed ni inclusive japo sio vyema kufanya tendo hilo kipindi akiwa katika hedhi
 
Mi sijaelewa kama mimi mpenzi wangu anaanza mzunguko tar 18 na anadumu kwa siku 5 je nisiku gani anaweza kubeba mimba
 
kama ameingia hedhi tarehe 8 na kama mzunguko wake ni wa siku 28 basi siku salama kwake zitakua ni;
-tarehe 08 hadi tarehe 19 kisha tarehe 26 hadi tarehe ya mzunguko ujao
NB;hapo siku anazobleed ni inclusive japo sio vyema kufanya tendo hilo kipindi akiwa katika hedhi

Asante mpendwa, lakn sijaelewa vizuri, mbona umetofautiana sana na jamaa mwingine humu ndani?
 
1.Siku salama ni tarehe 13,14,15,16,17 endapo hedhi yako ni siku tatu mpaka tano awamu ya kwanza.
2.Awamu ya pili ni tarehe 27,28,29,30,"31" 1,2,3,4,na tarehe tano. Hapo kati ya tarehe 5 na tarehe 6 ni hedhi ya mwezi unaofuata, kutegemea na idadi ya siku katika mwezi uliotangulia.

Aljebra hii ni kwa binti mwenye mzunguko wa siku 28. By MSAKI.

Asante sana ndugu kwa shule yako nzuri. Kwa hyo una maana kuwa kwa mwezi unaofuata hataingia tarehe 08 kama mwezi huu bali ataanza kati ya tar 05 na 06?
 
1.Siku salama ni tarehe 13,14,15,16,17 endapo hedhi yako ni siku tatu mpaka tano awamu ya kwanza.
2.Awamu ya pili ni tarehe 27,28,29,30,"31" 1,2,3,4,na tarehe tano. Hapo kati ya tarehe 5 na tarehe 6 ni hedhi ya mwezi unaofuata, kutegemea na idadi ya siku katika mwezi uliotangulia.

Aljebra hii ni kwa binti mwenye mzunguko wa siku 28. By MSAKI.


mkuu samahan naomba urudie kidogo hapo uniacha
unamaana kuwa m/mke ana siku za kupata mimba mara 2??
 
Hizi hesabu zenu msipokuwa makini kuna mtu atapewa mimba soon...kalenda ipo tricky sana.
 
Kama unatumia kalenda unatakiwa uwe makini sana,kwani ikibadilika kidogo tu inaweza kula kwako na ni vizuri mzunguko wako ukiwa ni 28 dys
 
Anyway...
Nisaidieni wangu anaingia bleed kila tar 27,28,29 tar 30 alimalizia kidogo sana
sasa naomba mnisaidie anamzunguko wa siku ngapi na tareh yake ya hatari.
watu8, Chocs na wengine embu weken maneno hapa
 
Last edited by a moderator:
1.Siku salama ni tarehe 13,14,15,16,17 endapo hedhi yako ni siku tatu mpaka tano awamu ya kwanza.
2.Awamu ya pili ni tarehe 27,28,29,30,"31" 1,2,3,4,na tarehe tano. Hapo kati ya tarehe 5 na tarehe 6 ni hedhi ya mwezi unaofuata, kutegemea na idadi ya siku katika mwezi uliotangulia.

Aljebra hii ni kwa binti mwenye mzunguko wa siku 28. By MSAKI.

asante na wengine tumeelewa!!!!
 
Asante mpendwa, lakn sijaelewa vizuri, mbona umetofautiana sana na jamaa mwingine humu ndani?

ok ngoja niiweke hivi..
siku ambayo ina probability kubwa yakupata mimba ni siku 14 kabla ya mzunguko ujao;hivyo kama mkeo ana mzunguko wa siku 28 inakua hivi;
-tufanye 28 toa 14 inakua 14 (28-14=14) hivyo siku ya 14 baada ya hedhi kuanza ndio siku hatari zaidi.
-yai(ovum) huwa lina survive masaa kadhaa (36) ambayo ni kama siku moja na nusu hivyo siku ya 15,siku ya 16 na nusu pia ni hatari,ila to be in a safe side tuaproximate kwamba siku ya 15,16 na 17 pia ni hatari.
-mwili wa binadamu hauna formula hivyo yaweza tokea yai likawahi kidogo au likachelewa kidogo hivyo tufanye kwamba siku ya 11,12 na 13 pia ni hatari.
Conclusion:
-siku hatari ni siku ya 11 hadi siku ya 17
-siku zingine zote zilizobaki ni salama.
NB;siku zinahesabiwa kwaanzia hedhi ilipoanza hivyo tunaposema siku ya 11 tunamaanisha siku ya 11 baada ya hesdhi kuanza,yani siku hedhi ikianza ndio inahesabiwa ni day one.
 
Back
Top Bottom