Naomba msaada, mtoto wangu anajinyea

Naomba msaada, mtoto wangu anajinyea

Mtoto miaka miwil kujinyea ni uzembe wa mzazi...Ipo kwa baadhi ya watoto ila malezi yenu ndo yanachangia...Sasabwenzio mtoto akifikabmiez sita tu wanaanza kufundisha watoto kila kitu mpk akifika umr huo anajitegemea!
Mfano mi mtoto wa dadangu akibanwa haja zote anajua lile poti lake la kiti liko wapi..Qnavua nguo ya chini mwenyewe anajisaidia we utaskia mama tayar ujue ukamnawishe,mwingne miezi nane tu hakojoi kitandani wala hamkojolei mtu..Lakini hujachelewa ndugu jitahid umfundishe kbla ya miaka mitatu kufika..Mfundishe kutumia poti na kuvua nguo ya chini mwenyewe utaona..
Daaa umejibu kwa ukali mpaka nimeumia. Sina uhakika kama una mtoto tayari*. Binafsi nina mtoto wa umri uliozaidi ya huo, na bado naendelea kumfunza mwanangu hizo habari za kupupu. Ninachojua ni kuwa watoto wanatofautiana sana linapokuja suala la kujifunza kitu kipya. Wapo wanajifunza mapema na wanaochelewa. Kikubwa kwa mzazi ni uvumilivu.
 
Pole mkuu...kusema kweli Kuna vitu vigeni vikitokea vinachanganya sana...Kuna mtoto wa Dada yanagu alikuwa anakojoa kitandani hadi umri wa miaka 12...walitumia mbinu nyingi sana lakini wakafikia hatua wakakata tamaa dogo akawa kikojozi sugu
Niliporudi tena chuo kujiendeleza nikaamua kumchukua kukaa nae kwangu...nikiwa macho usiku nasoma namshtua kama mida ya saa tisa usiku kila siku namfungulia mlango anaenda kukojoa...kusema kweli ndani ya wiki mbili tu akaanza kushtuka mwenyewe usingizini anafungua mlango anakojoa anarudi kulala
Nilipompa mama yake (Dada yangu) taarifa za mwanae akanambia "kaa nae tu ndo keshakuwa mtoto wako huyo"...hadi leo naishi nae kwangu hapa
Miaka 12 tu? Heri huyo. Kuna watu mpaka wanahitimu kidato cha sita bado.......
 
Halo wadau, mambo ni aje?? Nina mtoto wa kiume wa umri wa miaka miwili na miez mitatu, ananipa mawazo sana, akisikia haja ndogo utasikia anakwambia nataka jojoa na either aende nje au atakwenda kabisa chooni ila ikija kwenye haja kubwa, yaan tumejitahidi kila njia lakin utamuona anakwenda pembeni anasimama na anajinyea. Sasa jamani nifanyeje?? Au itafika mahal ataacha?? Je kuna chochote naweza kufanya kwa sasa kumsaidia?
Wangu alikuwa hivyo hivyo, nikaanza kumchapa viboko, leo hii akisikia tu haja anakwenda mwenyewe chooni.
 
Mzoeeshe kukaa kwenye poti na kila ukijua ni mida yake ya kujisaidia mmwambie akae kwenye pot atazoea tu,pia mpime minyoo
We ndo umemaliza kila kitu mtoto lazima ajifunzie kwenye pot si unamwelekeza aende chooni mana anapata uoga..miaka ya nyuma kinamama walikua wanainyosha miguu yao na kuitanua kidogo kisha wanamkalisha mtoto anajisaidia na anajenga picha kuwa yupo chooni badae anazoea ila siku hizi utandawazi ndo kuna mambo ya kutumia poti vilevile kama mzazi/mlezi kuna zile lugha kali za kuwambia mtoto pindi akibanwa na haja si nzuri huwa zinawaathiri anaweza jifanya kaghairi kujisaidia kumbe ashaharibu..
 
Mie wangu nikimuweka kwenye poti analia utadhani poti lina mdudu nshachoka, anapupu kasimama utadhani ng'ombe
Yaan wa kwangu ni hvyo hivyo, ikimwambia ukisikia kupupu unatakiwa kwenda wapi? Anakujibu poti, ila kalilete sasa, balaah hataki kabisa kukaa, yaan wa kwako na wa kwangu wanafanana kabisa
 
Yaan wa kwangu ni hvyo hivyo, ikimwambia ukisikia kupupu unatakiwa kwenda wapi? Anakujibu poti, ila kalilete sasa, balaah hataki kabisa kukaa, yaan wa kwako na wa kwangu wanafanana kabisa
Mie nimeamua kumuacha, aendelee hivo hivo kama ng'ombe ha ha ha, anaenda pembeni anashika kitu anapupu akimaliza anarudi poti hataki kabisa
 
Back
Top Bottom