Naomba Msaada. Nifanyeje ili niweze kupona ini?

Naomba Msaada. Nifanyeje ili niweze kupona ini?

Mrejesho. Nilipost humu kuomba ushauri kuhusu hali yangu ya afya baada ya kuambiwa ini langu lina shida. OK ilibidi nirudi Amana na kuomba rufaa ya kwenda Muhimbili kuona na Dr bingwa wa ini. Baada ya kufika Muhimbili nilifanyiwa vipimo vyote muhimu vya awali vya utambuzi wa tatizo kwenye ini, kongosho, nyongo na figo. Pia nilifanya Utrasound ya tumbo na Endoscopy. Vipimo vyote havikuonesha dalili ya uharibifu ktk ini na viungo vingine vya ndani, hivyo Dr akiishia hapo kuwa ini halina shida hivyo hakuna haja ya kuagiza vipimo zaidi. Kuhusu maumivu ya tumbo upande wa juu kulia chini ya mbavu Dr alisema huenda ni sababu ya vidonda vya tumbo ambavyo viligundulika kwenye kipimo cha Endoscopy. Hivyo zoezi la uchunguzi kuhusu ini na viungo vingine vya ndani liliishia hapo na ugonjwa pekee uliotambuliwa ni ulcers ambapo nilipewa dozi ya wiki 6. Ahsanteni kwa ushauri wenu na pole mlizonipa.
Da umefanya siku yangu iishe vizuri sana. Mungu ni mkubwa. Japo sikujui lakini huwa nikisia binadamu mwenzangu anakumbwa na tatizo kama ulilokuwa umeambiwa unalo huwa najisikia vibaya mno. Ila kweli Bongo nyoso. N nini kilikuwa kimetokea mwanzoni? Sitaki kumlaumu sana huyo dr kwani hata vipimo vya maabara Bongo wakati mwingine huwa fyongo.
 
Mrejesho. Nilipost humu kuomba ushauri kuhusu hali yangu ya afya baada ya kuambiwa ini langu lina shida. OK ilibidi nirudi Amana na kuomba rufaa ya kwenda Muhimbili kuona na Dr bingwa wa ini. Baada ya kufika Muhimbili nilifanyiwa vipimo vyote muhimu vya awali vya utambuzi wa tatizo kwenye ini, kongosho, nyongo na figo. Pia nilifanya Utrasound ya tumbo na Endoscopy. Vipimo vyote havikuonesha dalili ya uharibifu ktk ini na viungo vingine vya ndani, hivyo Dr akiishia hapo kuwa ini halina shida hivyo hakuna haja ya kuagiza vipimo zaidi. Kuhusu maumivu ya tumbo upande wa juu kulia chini ya mbavu Dr alisema huenda ni sababu ya vidonda vya tumbo ambavyo viligundulika kwenye kipimo cha Endoscopy. Hivyo zoezi la uchunguzi kuhusu ini na viungo vingine vya ndani liliishia hapo na ugonjwa pekee uliotambuliwa ni ulcers ambapo nilipewa dozi ya wiki 6. Ahsanteni kwa ushauri wenu na pole mlizonipa.
Mungu ni mwema, hospital izi ndogo zinaua watu nimegundua,hayo madawa waliyokupa kumbe hayakuwa na haja kabisa
 
Pole na hongera kwa kupata majibu mjarabu,Hao ndo madaktari wetu,kuna muda wanazingua,nilishawahi kutumia vidoge vya tatizo la moyo kwa mwaka mzima jumlisha na vidonge vya presha,duh kwenda mhimbili naambiwa sina tatizo la moyo na wala sitegemei kuugua moyo kwa wakati huo,nilichoka kabisa
Duuh ni hatari sana
 
Ila unaweza Kuta Dr Hana tatizo Bali tatizo limetengenezwa na watu wa vipimo I e maabara na vipimo vya kumulika kama ultrasound, x ray nk hao ndio nahisi wamemuingiza chaka Daktar kupitia majibu ya hivyo vipimo.
Yes hii inawezekana pia
 
Dawa zipo. Kama na wewe una matatizo ya Ini au mengine ya kiafya, njoo PM nitakuelekeza dawa. Karibu sana.
Wazee wa fursa mshatia timu.. 😅

Weka mambo hadharani kama walivyofanya wadau wengine, wewe huko uchochoroni unataka kumfanya nini mwenzio!?
 
Unaweza ukathibitisha pasipo shaka kuwa mimi ni tapeli? Nimemwita aje PM ili tuwasiliane kwa njia ya simu. Unapoongea na mgonjwa na kumsikiliza ni rahisi kujua tatizo lake kuliko kusoma alichokiandika.

Acha ujinga wa kuwaita watu matapeli wakati huwajui. Nimekutapeli nini Mbweha wewe?

 
Wazee wa fursa mshatia timu.. 😅

Weka mambo hadharani kama walivyofanya wadau wengine, wewe huko uchochoroni unataka kumfanya nini mwenzio!?
Tiba ni biashara. Ukienda hospital yoyote ile utalipa ili utibiwe. Mimi nafanya biashara ya TIBA. Sasa siwezi kuweka matangazo yangu hadharani bila kuyalipia. Ukija PM tunaongea nakusikilza na nakupatia tiba. Yes, upo sahihi. Hii ni fursa kwetu sisi watoa tiba mbadala.😀
 
Hii ina tofauti gani na kupiga ramli..?
Wakati mwingine kutegemea na mazingira, upatikanaji wa vipimo na kiwango cha utaalamu wa mtaalamu. Daktari wa Amana amefanya kutokana na uwezo na mazingira yake ashukuriwe.
 
Wakati mwingine kutegemea na mazingira, upatikanaji wa vipimo na kiwango cha utaalamu wa mtaalamu. Daktari wa Amana amefanya kutokana na uwezo na mazingira yake ashukuriwe.
Sahihi kbs, kwa level yake na hospital anayofanyia kazi hakuwa na cha ziada
 
A
Kuna mama mmoja aliandika symptoms za ugonjwa wa mwanae uliomsumbua kwa muda mrefu sana kwenye AI,AI ikampa majibu, akachukua majibu na kuyapeleka kwa daktari wake, daktari akashangaa na kusema huenda hichi ndo kinachomsumbua mwanao kweli, mtoto akatibiwa akapona. Source: News za redioni.

Sisemi kuwa AI itakupa majibu ila jaribu tu uone itasemaje, ukiona kuna jambo la tofauti na madaktari walichokuwa wanasema, nenda kawaonyeshe.
IA zipi hizo,can you mention few of them.
 
Back
Top Bottom