Naomba Mwenye Picha ya Mbowe na Viongozi wa CHADEMA Wakishiriki Msibani kwa Mama Mzazi wa Halima Mdee

Naomba Mwenye Picha ya Mbowe na Viongozi wa CHADEMA Wakishiriki Msibani kwa Mama Mzazi wa Halima Mdee

Mbowe anahusika vipi hapo kwenye msiba au chadema for that matter?
Kwani Msigwa na Jobo wakienda hawatoshi?
 
Mtoto akikosea huadhibiwa. Kwa huu utoto wa CHADEMA tutawadhibu kwenye sanduku la kura.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Sote tunafahamu kuwa Mbunge wa viti maalum wa CHADEMA Mheshimiwa Halima James Mdee amefiwa na Mama yake Mzazi siku chache zilizopita. ambapo mimi binafsi nampa pole sana Mheshimiwa Mdee kwa msiba huo mzito wa kupoteza Mama yake Mzazi.Namuomba Mwenyezi Mungu amtie nguvu na moyo wa Subira wakati huu wa majonzi na huzuni.

Najuwa ni Msiba mzito sana tena sana kwa Mheshimiwa Dada Yangu Mh Halima Mdee. Ndio Maana tumeshuhudia viongozi wetu mbalimbali wa serikali yetu ya CCM pamoja na chama chetu pendwa cha CCM kwa unyenyekevu na upendo mkubwa wakifika msibani na kutoa pole kwa wafiwa.

Lakini sijabahatika kuona picha wala video za Mheshimiwa Mbowe akiwa msibani pamoja na viongozi wenzake wa CHADEMA .Nilikuwa nauliza hawajaenda msibani au wapo ila mimi ndio nimepitwa na habari hiyo?

Kama hawajaenda Msibani hususani Mheshimiwa Mbowe na viongozi wengine watakuwa wamefanya jambo baya sana tena sana lisilo la kibinadamu wala kiungwana .litakuwa ni jambo la kitoto sana tena sana kutohudhuria.litakuwa ni jambo litakalo onyesha namna wasivyo na utu,upendo,ukomavu wa kiakili pamoja na kujaa utoto.

Ikumbukwe au nawakumbusha ya kuwa alipofariki Mama Mzazi wa Mheshimiwa Zitto Kabwe , viongozi wengi sana wa CHADEMA hawakuhudhuria msiba ule kwa sababu wanazozijua wao wenyewe.

Kuna kauli inasema kama wamefanya hivi kwa Mti Mbichi vipi kwa Mti Mkavu?

Naomba nisiongee mengi. Naomba tu kupatiwa picha au hata video.View attachment 3062148

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Siyo vizuri kutumia msiba wa watu kufanyia siasa ndugu. Huko unapotaka tuelekee sipo .
 
Ila Lucas sijui sometimes akili yako unaiweka wapi sijui.

Sasa unajua kabisa kina Halima na huyo Mbowe hawaelewani tena pakubwa tu unataka waende msibani kufanya nini
 
Ila Lucas sijui sometimes akili yako unaiweka wapi sijui.

Sasa unajua kabisa kina Halima na huyo Mbowe hawaelewani tena pakubwa tu unataka waende msibani kufanya nini
Mbona Mbowe alikuwa na akina Mheshimiwa Mdee kanisani kkkt alipokuwa anataka wamchangie mchango kanisani? Au umeshasahau mara hii?
 
1000011398.jpg
 
HIYO HAPO

Mbowe 2.png
Mbowe1.png

Kutoka Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Mpalizwa wa Mbinguni, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam - Kibangu, lililopo Ubungo Kibangu sehemu ambapo ibada ya kuaga mwili wa Bi Theresia Mdee ambaye ni mama mzazi wa Mbunge wa Viti maalum Halima James Mdee aliyefariki hivi karibuni inaendelea, tunakusogezea habari picha zikimuonesha Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa Freeman Mbowe akiwa Kanisani hapo

Kwenye habari picha hii Mbowe anaonekana akiwa ameketi pamoja na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila, Mkuu wa wilaya ya Ubungo, Hassan Bomboko, aliyekuwa mgombea Ubunge wa CHADEMA jimbo la Ubungo 2020 ambaye pia ni Mstahiki Meya wa zamani wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Boniface Jacob na waombolezaji wengine
 
Back
Top Bottom