Naomba neno moja tu la Kingereza ambalo halina tafsiri rasmi ya Kiswahili

Msaada wa kiswahili cha maneno yafuatayo...πŸ˜‚
Adenocarcinoma
Erythroblastosis fetalis
Gait
Retinoblastoma
Cubital fossa
Popliteal fossa
Dysdiadochokinesia
Ataxia
Oligodendrocytes
Astrocytes
Pericytes
Tuberosity πŸ˜‚
Glossitis
Fontanelle
Mesoderm
Ectoderm
Endoderm
Extraembryonic coelom
Tubercle
Substantia nigra
Substantia feruginosa
Styloglossus
Thyrohyoid
 
Mimi natamani tujadili neno la mjasiriamali ambalo kwakimombo ni an entrepreneur kiuhalisia kunatofauti kati ya entrepreneurship na Entrepreneurs, entrepreneurship ni elimu inayo muwezesha mjasiriamali kubuni jinsi ya kuanzisha na kupanga jinsi atakavyo ifanya hiyo biashara kwa kutengeneza mpango wake wa biashara kwa kujumuisha jedwali la matumizi na mapato kwa muda wa mwaka mmoja ama zaidi wakati huohuo akiwa anajua biashara zina changamoto hivyo inatakiwa pia apange mikakati ya kukabiliana nazo lakini kumbe an entrepreneur ni ni mtu ambaye anazichangamkia fursa na kuzigeuza kuwa biashara kwa kuifanya hiyo biashara huyu eti akili yake imefungwa kwa maana hafikirii jinsi ya kubuni na kupanga atavyokabiliana na changamoto kwakifupi hana elimu ya ujasiriamali baada ya ufafanuzi huu naomba tujadili kwa kiswahili huyu mjasiriamali ambaye haja bahatika kupata elimu ya ujasiriamali anatakiwa aitweje
 
Shida kubwa ni kulazimisha kila kitu kipya kiwe na jina la kiswahili, matokeo yake ni kubuni vitu vya ajabu na vigumu au visivyo halisi. Mengine tuyatamke hivyo hivyo kama tulivyofanya kwenye Redio, baiskeli, tochi,kamisheni, n.k
Mfano kuna haja gani ya kuhangaika kubuni vitu kama
1. Flush disk eti_ disiki mweko
2. Computer.....
3. TV.....Runinga
Manene mengine yaingizwe kama yalivyo
Kuna mbwembe nyingine kama
1. Maji tiririka.. Hapa ni kama unayaamuru maji, kwa nini tusitumie --Maji yanayotiririka
2. Taasisi nunuzi (Procuring Entity) Kwa nini isiitwe Taasisi inayonunua?
 
Kiswahili ni lugha ya kuunga unga sana sijui kwanini tunaikumbatia
Yah! Ukiona neno moja la lugha nyingine linatafsiriwa kwa mtiririko wa maneno ili lieleweke hiyo lugha (inayotafsiri) bado sana.

In short Kiswahili is too verbose; you need a number of words to translate a single word from other languages.
 
Nashukuru kwa mchango wako. Je unaweza kusema "Orodha nyeusi" ndio tafsiri rasmi ya "Blacklist?" katika muktadha wa "Mwenye/wenye sifa mbaya iliyopitiliza?"
Labda kuwekewa vikwazo
 
Tafsiri zipo nyingi tu na hata maneno yaliyotoholewa yametafutiwa tafsiri...

Niliwahi kumsikia jamaa mmoja anaongea baadhi ya maneno.
Bora tuendelee na swanglish
 
Serendipity

Hili ni neno linalomaanisha ugunduzi wa kitu kizuri bila kukitafuta, au bahati nzuri isiyotarajiwa inayokuja kwa namna isiyo ya moja kwa moja.

Kiswahili hakina neno moja linalobeba maana hiyo kwa usahihi, hivyo mara nyingi linabaki kama lilivyo au linafafanuliwa kwa sentensi.

Ova
 
Lugha huzaliwa,hukua ,huishi,Kisha hufa.
Lugha ya Swahili hukua Kwa njia mblmbl 1.maendeleo ya tekinolojia.
2.kutohoa ktk lugha za kigeni ktk nyanja za kisiasa,kiuchumi,kielimu nk.
Hata wazungu nao wameamua kubaki na neno ,"UGALI" PASIPO KULITAFSILI KTK LUGHA YA KIINGEREZA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…