Watu wa hivi walishatamani kitambo kuwa kama wewe ila uwezo hawana, nawe hujui nia yao una waona juu, juu tu! wanashindwa vibaya, so wanaanza kujichukia wao wenyewe kwanza kwa kuwa roho na nafsi zao vimeshindwa kuwafanya wawe km wewe!
Tatizo hawajui kuwa wanavipaji ambavyo wewe huna. kwa sababu ya ukosefu wa maarifa ya kutambua vipaji vyao, wanakuchukia kwa sababu wewe umegundua na kutumia kipaji chako! ndiyo maana tunasisitiza someni sana vitabu, JF,FB,WTS. mpate maarifa mwanadamu anasumbuliwa na kutokujua tu basi!
Kumbuka kila mtu hapa Duniani ana kipaji chake alichopewa na Mungu, kukijua ndo kazi ipo!!! ukikijua unapiga Bingo na mibaraka sana, na ukibarikiwa tu hata uwe wapi wenye chuki watajitokeza wengi. unatakiwa ulinde Mafanikio yako,
Hali inakuwa mbaya zaidi wakikuona unavyofaidi kile ulichopata kwa kufanya kazi walizo shindwa wao! Adrenalin zinapanda mwilini mwao hizi husababishia mtu uoga, na roho kuuma sana, na hasira kila siku. ukiwapima BP hawa watu iko juu ya wastani!!!
Hakuna jinsi, na asili ya watu! hii yote sababu ni mafanikio yako, na jinsi Mungu anavo kubariki ndiyo huleta mambo haya yoote! ukitaka haya yasitokee kwako, na yasikupate kabisa fanya hivi;
Uza kila ulicho nacho, au gawa kila ktu ulicho nacho kwa watu.
Usiseme kitu chochote mahali popote.
Usiwe na Elimu yeyote wewe wala mwanao.
Usijenge nyumba , wala usinunue gari. hata mkokoteni usiendeshe!
Usiwe na familia, mke wala watoto.
Usivae nguo nzuri.
usi miliki kitu
Hakuna ktk hali km hii atakaye kusema wala kukuonea gele mpaka mwisho wa Dunia hii. jaribu.