NAOMBA USHAURI: Hizi mbao zilizoko sokoni hapa Dar ni zipi zafaa kwa kupaulia nyumba ya kuishi? naziona kama nyepesi sana

NAOMBA USHAURI: Hizi mbao zilizoko sokoni hapa Dar ni zipi zafaa kwa kupaulia nyumba ya kuishi? naziona kama nyepesi sana

Wauzaji wa hizo mbao wanakuchania hapo hapo kwa mashine. Bei ya kuchana siyo kubwa. Umwone huyo fundi. Akupeleke hapo zinapouzwa ili uulize gharama hasa baada ya fundi kukukadiria mbao zinazohitajika katika boma lako. Ukishafanya tathmini ufanye maamuzi.
Sawa Mkuu asante sana
 
Ukipata mbao ambazo zimezoeleka kwa jina la mlingoti utakuwa umefanya jambo la maana mno. Zenyewe haziwekwi dawa. Upate zilizokomaa na utazifuta kwa rangi yake kuwa nyekunyekundu hivi.

Hapo hautawahi kulia juu ya wadudu. Bati zitaisha, utaezeka tena bati huku mbao zako zikiwa vilevile. Mafundi wengi hawawezi kukuombea juu ya hilo ingawa wanazijua ubora wake kwani wanataka mbao laini.
Sorry mkuu hapa kwenye milingoti unamaanisha "mirunda"??
 
Back
Top Bottom