Naomba ushauri kuhusu kujifunza Gari ya Manual kwa Msichana

Naomba ushauri kuhusu kujifunza Gari ya Manual kwa Msichana

Gari inazima sababu upo kwenye Gia kubwa.
Unapotaka kusimama unasahau upo Gia namba ngapi.
ukitembelea Gia namba 1gari haiwezi kuzima.
Wewe ni DEREVA SASA.
Kwann 1st gear isizime mkuu kama hajafata masharti? Changamoto kubwa ya first time drivers ni jinsi ya kuondoa gari na jinsi ya kusimama bila gari kuzima pamoja na ku control gari lisizime kwenye foleni ya kilimani.
*Point of correction-1st gear ndiyo gear kubwa na siyo vinginevyo.
 
Gari ya diesel unaweza ukaacha kwenye Gia namba 1 na isizime na ikaendelea kwenda..
Sisi huku kitaa tunaamini Gia namba 1 ndo Gia ndogo.
Kwann 1st gear isizime mkuu kama hajafata masharti? Changamoto kubwa ya first time drivers ni jinsi ya kuondoa gari na jinsi ya kusimama bila gari kuzima pamoja na ku control gari lisizime kwenye foleni ya kilimani.
*Point of correction-1st gear ndiyo gear kubwa na siyo vinginevyo.
 
Gari ya diesel unaweza ukaacha kwenye Gia namba 1 na isizime na ikaendelea kwenda..
Sisi huku kitaa tunaamini Gia namba 1 ndo Gia ndogo.
1st gear haijawah kuwa gear ndogo hata siku moja mkuu labda kwenye huo mtaa wenu 🤣 🤣
 
Kama unazima gari wakati wa kuondoka ukiwa Gia namba moja wewe ni mzembe
Mkuu kwa wanaoendesha gari watakupa experience hapa wakati walipokuwa wanajifunza au changamoto walizoziona wakiwafundisha wenzao.
Gari la Manual ni rahisi sana kuliendesha likiwa kwenye motion.
 
Mimi naona ni clutch na break.
Hata ukiwa Gia kubwa unaweza ukasimama Kwa kukanyaga clutch na break na gari isizime
Ukikanyaga Clutch na break haliwez kuzima kama ulivyosema,lakin kiuhalisia 1st time drivers hukimbilia break na kusahau ku engage clutch na hvyo gari kuzima
 
Ni rahisi sana. Ukishamudu kuinyoosha na kukata kona vizuri basi zingatia namna rahisi za kuwasha na kuzima kama hivi hapa chini:

KUONDOA AU KUENDESHA GARI.
Unapokuwa umekagua gari lako na kulikuta liko katika hali nzuri sasa unataka kuliendesha na kuanza safari na gari lako, unapoingia kwenye gari na kuikuta iko katika gea namba moja basi sasa unapaswa kufanya maswala yafuatayo.
i. Weka switch/ yaani ufunguo wa gari katika sehemu yake
ii. Kanyaga clutch mpaka mwisho
iii. Ondoa gea namba moja na kuliweka gari huru yaani free
iv. Ondoa mguu kwenye clutch
v. Anza kuwasha ufunguo wa gari Satrt/Switch gari
vi. Sikiliza muungurumo kidogo
vii. Kanyaga clutch mpaka mwisho/pamoja na brake kulisaidia gari lisiweze kurudi nyuma
viii. Ondoa gari kutoka kwenye free mpaka kwenye nambari moja gea hii mara nyingi hujulikana kama gea ya kuondokea
ix. Legeza mguu wa kwenye clutch mpaka unasikia gari kama inaondoka hivi mlio unakuwa umebadilika na unakuwa constant
x. Kumbuka kutoa handbrake
xi. Ongeza mafuta kidogo na na kulegeza clutch na gari litaanza kuondoka na linapoondoka achia clutch, lakini usiachie ghafla, taratibu baada ya kuona baada ya kuona gari liko kwenye mwendo wa kawaida
xii. Lipe gari nguvu kwa kuongeza mafuta na badilisha gea nambari moja kwenda nambari mbili, unapobadilisha gea hakikisha kuwa unaachioa accelerator na kukanyaga clutch na baada ya gea kuingia unaachoia clutch na unakanyaga acceleretaor
xiii. Utaendelea na safari kwa kubadilisha gea nambari mbili mpaka tatu na kuendelea
Kumbuka gea nambari moja sio ya kutembelea hivyo usiiache kwa muda mrefu bila ya kuibadilisha
 
Ni rahisi sana. Ukishamudu kuinyoosha na kukata kona vizuri basi zingatia namna rahisi za kuwasha na kuzima kama hivi hapa chini:

KUONDOA AU KUENDESHA GARI.
Unapokuwa umekagua gari lako na kulikuta liko katika hali nzuri sasa unataka kuliendesha na kuanza safari na gari lako, unapoingia kwenye gari na kuikuta iko katika gea namba moja basi sasa unapaswa kufanya maswala yafuatayo...
Hizi taratibu ulizompa akizifanya kama zilivyo ipo siku zitamuua au kuharibu gari Mguu kwenye break ni muhimu sana na siyo hiyo clutch kabla ya kuanza kuwasha gari na kufanya mengineyo
 
Ili usiwe na hofu na ujiamini, tafuta ndugu jamaa au rafiki/jirani mwenye gari ya manual na muombe uwe unafanyia mazoezi ya ziada baada ya kumaliza ya shule. Lisaa limoja tu litakutosha na umpe mwenye gari elf 10 kufidia wese lake, ukifanya hivyo kwa siku 5 tu uoga wote unaisha na kuanza kujiamini.
 
Back
Top Bottom