Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Na watoto wa mke wa tatu wana excuse gani?
 
Ushauri wenu ni muhimu sana.

Umri wangu ni miaka 50, nimeoa mke kanisani huu ni mwaka wa 25 naishi naye na tumejaliwa watoto wanne, wa kwanza na wapili wamemaliza tayari chuo kikuu na wa tatu yupo chuo kikuu mwaka wa pili...
Hii chai ina ulazima wa kuongeza kijiko cha sukari aisee
 
Baada ya kuiuza ile nyumba, na kipindi hicho ujue tayali alishaanza kuwa na kachuki fulani hivi ambako sikukaelewa, ila akili yangu ilinituma labda hakupenda tuuze ila nyumba, mimi sikujali,

Ila aliniomba kitu fulani nikifanye wakati wa kupokea ile pesa, ila wakati ananiambia mimi sikusikia vizuri maana naona hata yeye alikuwa na wasiwasi anachonieleza ndio maana maana Sauti yake haikutoka vizuri, nikamwambia naomba urudie unasemaje,

Akaniambia sasa nikasikia vizuri,

NAOMBA HIYO PESA NIWEKE MIMI,

Nikamuuliza kwa nini,? Kwani huniamini, na kwa nini huniamini wakati unajua kabisa wewe tayari ni wangu na tuna watoto, mimi sio mhuni najua lengo la kuuza nyumba ni kwamba tulikuwa na sehemu fulani na ni lazima pigs ua tuee na nyumba yetu nyingine ambayo imeisha ili tuishi sasa kama akina fulani,

Akanjibu, unajua............

Ndugu zangu naomba mguess alikuwa na maana gani na nimkubalie au nikatae?

Mawazo yenu wakati naendelea
 
Baada ya kuiuza ile nyumba, na kipindi hicho ujue tayali alishaanza kuwa na kachuki fulani hivi ambako sikukaelewa, ila akili yangu ilinituma labda hakupenda tuuze ila nyumba, mimi sikujali..
Dah...unatutesa Kama anavyokutesa bi mdogo, Sasa jamani tutaguess Nini hapo? Unataka tukushauri au unatuhadithia tu ili tuanze ku guess.....malizia bwana wahenga wenzio tunasubiri
 
Asante kwa haya maarifa mkuu
 
Tunazidi kuongez maarifa kidogo kidogo
 
Mzee kwanza shikamooo na pole kwa uliyopitia

Ushauri acha kujibu koment maliza story halafu watu tuje kukushaur naona watu wanatoa ushaur kabla hujamaliza
 
Ni kweli, sisi wanaume ni maguvu, lakini usisahau kwamba tuliambiwa majukumu yote ya kulea familia ni yetu, labda ndio maana kutokana na ugumu wa familia huwa tanajifariji kwa mambo kama haya, mwishowe tunapoteza
anko umetupa ushauri bora sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…