Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Atabaki kuwa mchepuko tu mkuu mpaka utakapo amua kumtambulisha kwa mkeo, ndiyo atatambulika kama mke mdogo, hakuna justification
Lakini haina ya kutoa au kuwapa jina hili,
Sio wote huolewa, lakini kumbuka hata wewe mtoto wako siku moja anaweza kuwa bi mdogo wa mtu, au hata mdogo wako

Kwa hiyo kuwa makini na majina ambayo hawana staha, at the wote ni wanawake tu, unaweza kukuta bi mdogo ana staha zai di kuliko huo unaemwita hivyo,

Lakini kumbuka vile vile wanawake wanatuzidi Sadi vile cile, kwa hiyo lazima tubanane hivyo
 
Mkuu naomba ukumbuke kutuwekea muda wa matukio yanavyotokea. Hapa ilikuwa mwaka Gani?
Mbona nilisema, hiyo ni 2016 sasa, mwishoni,
Na kusema kweli matatizo yameanza kuanzia muda huo
 
Yani huyu mwanamke na tena ni mchepuko anakuambia akushikie pesa na unakosa jibu unawaza ufanyaje mkuu, hebu anza kuamka hizo akili sio zako, usijaribu kumpa mwanamke kitita cha pesa zishike uzipangie matumizi
Sawa ndugu, lakini naomba neno mchepuko usilipende sana kulitumia angalau kwa muda huu,
Ahsante kwa kuelewa
 
Mzee umesema ukistaafu una Kama 250m? Naomba nikufariji pindi utakapostaafu umehangaika Sana na majukum ya hapa na pale unahitaji kutulia Sasa na kula mema ya nchi...mi sihitaji kuzaa ucjal
Da Bola yule wa kuzaa, sasa wewe si ndio utakuja kwa mission moja tu ya kunimalizia mapema ili nisijutilie kiwingu, mimi Bi I mkubwa huyo huyo,
Ije mvua kiwake jua
 
Story nzima ni ya mke mdogo, sitaki kuingiza mambo ya mke mkubwa hapa, sitamtendea haki, jana tatizo na mimi, na binafsi nampenda sana, Muda wa kuwa naye upo na hata our tunatoka,

Na yupo happy sana na mimi, kwa sababu matunzo yake anapata kama malkia, na watoto wake anaona wanapanda madaraja, wa kwanza keshaajilia na anakula 2.5 M, Binti mdogo tu, wapili naye 1,8 m, Ana shida gani na hiyo kazi yote nimefanya mimi, Ila kama nilivyosema hao wote wana miaka miwili na mitatu, lakini nimesharushiwa sh 120000 tu.

Lakini vipi mama yao huko, naona kila siku ni nguo
Mpya kabitini, kwa hiyo keshaanza kula matunda ya watoto wake,
Hiyo karma wala haiwezi kunipata, kwani kakosa nini,

Ndugu yangu hapa duniani tunaishi mala moja,
Fanya kile kitu upendacho lakini kwa kiasi
 
Mpaka hapo kanikomesha nini, ni naona kama kanipa faida na ujinga wake, wewe unasema kanikomessha, anyway story bado, mtatoa majibu tu.
Oooh basi tuendelee inakuwa nusunusu adi mzooka unakosa
 
Mzee wangu kwanza pole kwa matatizo yanayokusibu japokuwa najua wewe mwanaume utaweza kuyamudu.

Kabla hata hujamalizia stori yako nadhani wengi tumeshajua shida iko wapi.

SHIDA NI BI MDOGO a.k.a MCHEPUKO japokuwa umesema apewe heshima zote kama mwenza wako lakini naomba nikuambie tuu hilo halitowezekana na wewe upo kwenye delusion state ndio maana akili yako inakataa kukubaliana na ukweli.

Ashakum si matusi, Kabla ya kukushauri naomba nikupe fact moja ambayo bado hujakubaliana nayo japokuwa ndio ukweli wenyewe. Huyo bi mdogo wako ni MCHEPUKO utake usitake. Huu ni ukweli mchungu ambao inabidi uumeze hivyohivyo ili upone. Japokuwa wewe unasema inabidi aheshimiwe na nini eti kwa sababu mmezaa naye lakini thats not a correct excuse.

Kwa nini nasema ni mchepuko/mwanamke ambaye si halali? Sababu kubwa ni kwamba DINI na MKE WAKO HALALI hajaridhia au hajayabiriki hayo mahusiano yako. Ni kweli hao watoto wenu ni halali na hawana kosa lolote lkn mahusiano yenu wewe na mama yao si halali ama ni haramu(ukweli mchungu na ni lazima uumeze ili kupona).

Naamini wewe una ndoa ya kikristo na ndio maana imekuwa ngumu kwako kumuweka hadharani/kumhalalisha huyo bi mdogo. Ungekuwa muislam basi ingekuwa rahisi sana kumhalalisha huyo bi mdogo na haya yote unayotusimulia yasingetokea.

Hivyo mzee wangu hapa cha kwanza inabidi ukubali moyoni mwako kwamba hapa ulibugi step na ni kitu ambacho ni haramu.The first step towards healing is Acceptance. Lazima akili yako ikubali kwamba this is wrong ndipo utaweza kufanya maamuzi sahihi. Huyo bi mdogo kwa bi mkubwa wako ana hadhi ndogo sana zaidi ya mchepuko, hivi imagine leo bi mkubwa wako akijua utamzuia kumuita mchepuko au majina mengine mabaya zaidi ya hilo kisa tuu umezaa naye? Haiwezekani mzee wangu. Yani bi mkubwa wako hatakuelewa kabisa.

SASA NINI CHA KUFANYA:
Kwanza mzee wangu lazima uweke BOUNDARY/LIMIT. Huyo bi mdogo kashasahau nafasi yake, hivyo ni wajibu wako kumkumbusha vividly bila kumuangalia usoni. Hapa lazima uweke mambo ya upendo pembeni. Achana na habari za sijui tunapendana, sijui enzi za 20th alikuwa ananilalia miguuni huku tunasikiliza RTD. ACHANA NAZO KABISA. Mkalishe chini na umpe black & white na mpe terms & conditions zote, kama hatakubaliana nazo basi umpe na consequences zake. Kumbuka HURUMA ISIZIDI UWEZO, MOYO USIZIDI UBONGO. Atake asitake ni lazima ajue kabisa yeye ni mchepuko na kamwe hawezi kukaa nafasi ya bi mkubwa. Na wewe pia utake usitake ni lazima ukubaliane na ukweli kwamba yule atabaki kuwa mchepuko tuu, kama hutaki basi kamhalalishe kwa bi mkubwa ama kanisani

Kingine mzee wangu, BE REALISTIC. Kama aina fulani ya maisha hauyamudu kwa sasa usifosi. Kwa nini ufosi kuwasomesha watoto english medium za 2M kwa mwaka wakati hata za 1M zipo na ni nzuri tuu?. Ishi maisha yako na familia zako hizo mbili kulingana na kipato chako. Hao watoto wa bi mdogo acha kuwapa favor sana. Kama watoto wa bi mkubwa huwa wanachelewa kurudi shule basi na hawa wa bi mdogo nao wawe wanaipata hiyohiyo joto ya jiwe.

Kingine pia mzee wangu, USIWEKEZE KWA MCHEPUKO KAMWE. Mchepuko muda wowote anakuruka na kukukana, yeye yupo kwenye win-win situation wakati wewe upo kwenye lose-lose situation. Yani ilitosha sana kumjengea nyumba, hukutakiwa tena kuanza kujihusisha naye kimaisha hasa ya uwekezaji. Ulichopaswa kufanya ni kuangalia wanao tuu, huyo mchepuko ulipaswa kumpa mtaji tuu kisha yanayoendelea ajijue mwenyewe. Ni kosa sana kupika na kupakua na mchepuko, ni kosa la pili kufanya uwekezaji na mchepuko.

Mengine tutaendelea kuchangia kadri na wewe unavyoshusha stori.
 
Mshua mpangilio wa stori yako ni mbaya sana, inapoteza ila userious na inapoteza focus, mwisho wa siku inakuwa km hadith tu ya abunuwas wakati wewe unataka ushauri. Kama inawezekana andika stori yote then utupie, andika hata kwa masaa 4 yote then tupia. Alafu acha kujibu comment zitakutoa kwenye reli, mwaga stori yote then unapitia kusoma comment na kupembua Ushauri upi unakufaa.
 
hii story imefanana na baba mmoja namfahamu tofauti tu yeye aliishia kwenye viwanja

hajafanikiwa kujenga na wanawake wore walimove on wana maisha yao Ila yeye kabakia anarandaranda duniani
Tulio single tunajulikana tu, saa nane usiku hii tupo online....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…