Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Binamu nakusalimu katika Jina la BWANA.

Uislam ni mzuri kuhusu issue ya wake wanne; kwa wanaume ambao hawajaamua kuridhika; na kwa wanawake ambao wanaenda kuolewa mke wa 2, 3 au 4. Ila kwa mke wa kwanza, suala la wanawake wanne kwake laweza kuwa shubiri;au kwa mke wa 2 na 3 pale anapoongezewa mke mdogo na yeye ndiyo utajua sasa kama wanafurahia kuongezewa wake wenzao.

The bitter truth; mtu asipoamua kuridhika hakuna idadi ya wanawake itakayomridhisha. Kwa sababu kuoa wake wanne haimaanishi ndiyo kwamba wakifika wanne tu na tamaa ya mwanaume inakufa. Ataendelea kutamani, na since hawezi kuoa mke wa 5,6..... basi atawafanya michepuko.

Na huo uke wenza uliohalalishwa; kwa kweli hekaheka zake tunaziona humu mtaani na duniani(especially insta). Hata wanawake tumeumbwa na ubinafsi, kilicho changu sitopenda kushare na mwingine period. Majority wanaolewa wake wenza kwa sababu tu ndiyo dini inataka hivyo na hawana option; lakini hawapendi. Ila most likely kadri unavyoongeza idadi ya wanawake, ndivyo unavyoongeza stress. Mara nyingi kila mwanamke atavutia upande wake na watoto wake ili wapendelewe zaidi wao. Na unaweza kuwatreat wake wote sawa; ila huwezi kuwapenda the same kuna sehemu tu upendo utazidi. Muda sio muda mabifu yanaanza, mara kukamatana uchawi n.k.. kwa zile hekaheka za wake wa mzee Yusuph au Queen Darleen na Sabra; kwa kweli naushukuru Ukristo. Na wanawake wanapeleka chuki zao hadi kwa watoto wa mke/wake wengine; watoto wengi wa kutoka kwenye familia za mitala hawapendani kwa sababu ya sumu wanazolishwa na mama zao.

Binadamu haturidhiki kwa sababu kiuhalisia kila siku kuna matamanio mapya; ni vile inafika hatua unasema na kuamua ngoja tu niridhike. Ni sawa tu na idadi ya partners; usipoamua kuridhika utaoa na kuacha kila siku. Usipojua/jifunza kuutiisha mwili wako; hakuna idadi ya wanawake itakayokutosheleza. Na kwa familia zetu hizo za uchumi wa kuvumiliana: wanawake wengi=umasikini

Na kwa shuhuda chache tu za watu walizozileta humu kuhusu ndugu zao waliokuwa na wake wengi; unaona kabisa jinsi fainali uzeeni inavyo-apply kwa wanaume. Mpende na kumuheshimu mke wa ujana wako.
 
Hiyo nyumba mwachie yeye na watoto. Mkatie eneo kiasi la kiwanja cha kwenye nyumba, eneo linalobaki weka fensi kisha kaendelee na maisha yako mengine.
 
Wa kiislamu mbona wameruhusiwa lakini nao ndio wale wale tu?[emoji2369][emoji2369][emoji2369][emoji2369][emoji2369]
 
Huyu mwanamke simtaki tena, lakini naona kama anawapambe,

Nipeni ushauri wapendwa,
Maana ninachokiona siku moja huyu mwanamke anaweza rudimentary hapa kwa gia ya watoto
Fukuza pumbavu huyu , wewe ni mwanaume Nasema FUKUZA
 

Siku zote mwanamke mwenye tabia za kishamba anakua hivo akili yake haina maarifa yeyote zaidi ya tamaa za kuishi kifahari bila kuangalia utu
 
Huyu mwanamke simtaki tena, lakini naona kama anawapambe,

Nipeni ushauri wapendwa,
Maana ninachokiona siku moja huyu mwanamke anaweza rudimentary hapa kwa gia ya watoto
Mkuu uza nyumba endelea na mishe zako
watoto wa kike hao wameshapandikizwa sumu na mama yao.
Muhimu wanafahamu mambo mengi kuhusu ugomvi wako na mama yao itoshe tu kuwatambulisha hao wanao kwa ndugu zako watakutafuta wakikuhitaji kwa mambo yakifamilia.
 
Very true. Yaan najua kabisa fulani anaye mtu wake ambaye anajulikana officially halafu eti aseme na yeye ni first priority.
Mdogo wangu tu mwenyewe toka awe na mchumba sina story nae tena sembuse mume wa mtu?

Kila mwanamke anatamani kuwa na mtu ambaye atamuweka yeye kama 1st priority kwake. Nianze tu kumpenda mume wa mtu nijiachie kabisa na kushindana na mke halali. Hakuna mapenzi hapo toka awali. Mzee wetu amekua zima moto
 
Demu wenyewe kimeo huyo umeona eeh!Mme wa MTU anakuheshimisha analeta us....e!!Lofa sana.Nafikiri waganga wake sasa wameisha nguvu ndo maana baba anajitambua Mme wa MTU anakupa hadhi yooote hyooo!mfyuu zake huyo mama N
 

[emoji16][emoji16]
 
Hiyo ni family yako. Huhitaji kumuonea aibu bi mkubwa. Mueleze ukweli.
 
Boss naamini hakuna mtoto mdogo hapo unaelea, hivyo nyumba hiyo hati yake naamini unayo, Tafuta mteja uza timkia mbali ukanunue nyumba nyingine, watoto unaeza wapangishia sehem kwanza wakati unafanya taratibu hizi siri isije mfikia huyo ibilisi.

Kwenye makao mapya asikanyage kabisa wala kutambulika kabisa, watoto wakitaka wataenda kumsalimia mama yao huko alipo.
 
Amen[emoji120][emoji120][emoji120]
 
Ushauri wangu ni huu. Huyo mwanamke mwanzoni nilikuwa nampa heshima ya bi mdogo kama ulovyoomba tumuite (badala ya mchepuko). Ila baada ya kusoma hitimisho lako nimeona jina sahihi la kumpa huyo mwanamke ni Mchepuko.

Toka nimeanza kukusoma sijaona mahali kuwa ulifunga naye ndoa huyo mchepuko. Cha kufanya hiyo nyumba mshirikishe mke wako halali (bi mkubwa). Hiyo kesi muuzie bi mkubwa ataimaliza fresh kabisa. Huyo mchepuko hastahili tena upendo wako.

Hata mwenyezi Mungu hutoa adhabu kwa wanaokosea wewe ni nani usimpe adhabu huyo mwanamke? Najua kisheria kuna kauponyo kidogo anaweza kukupelekesha kwa kuwa umeishi naye kwa muda mrefu lakini nina uhakika ukikomaa anaweza asipate hata cent tano. Hiyo nyumba itakuwa yenu (wewe na mke mkubwa). Watoto wa mchepuko unaweza kuwapa kama urithi kwa baadae.

Mwisho kabisa, najua unampenda sana huyo mchepuko ila kaka mkubwa umeshamla vya kutosha sana. 20 years unamkamua hana jipya tena na huna ulichobakiza kwake. Mfutilie mbali kabisa.
 
Naam, pole kwa yote unayopitia.

Nyumba iache iendelee kuwepo kwa ajili ya watoto

Huyo mwanamke ni vyema mkiachana kwa amani, rudi njia kuu kimya kimya muache awe na maisha yake sasa ndo fungu alilochagua

Hujachelewa kurekebisha penye tatizo, bora lawama kuliko fedhea, Unakoelekea ni kubaya sana, giza tupu ( roho ya usaliti ikishamvaa mtu, utu upotea, lea watoto wako wote.

Kama wewe ni muumini wa dini yoyote ni wakati wako sasa wa kumrudia mungu, piga goti kata vifungo vyote. Bwana awe nawe.
 
We mzee Hyo nyumba weka hzo nyumba za kupanga Kama uwazavyo afu ipige bei upate hzo 300mil ...vile viwanja vyako vitatu kimojawapo Jenga ka nyumba ka kawaida Sana ili huyo mchepuko wako akileta kelele umpe hyo nyumba aponee Apo. Wawekee hela watoto kwenye Account zao.! itakayobaki Anza kula Maisha make inaonekana umeanza kuchoka

Kuhusu bi mkubwa umesema tumuache au nasema uongo mzee wangu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…