Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

NILIVOMPATA!

Alikuja mjini DAR akiwa binti mdogo tu na karembo kweli kweli, nikimkuta kwa shemeji yangu mke wa wa rafiki yangu wa kazini.

Baada ya kutoka kazini huyu rafiki yangu aliniambia nimpitishe kwako kuna kitu anachukua halafu tuendelee na mishe zetu, mimi nilikuwa na kagari kangu yeye hana, na mara nyingi alikuwa anapenda kunitumia mimi, na Vibia nikawa navipata vya bure, sasa baada ya kufika kwake shemeji akawa katoka na funguo, ikabidi tumsubiri kwa muda, alipofika hata plan yetu ya kutoka tena ikawa imeishia hapo.

Lakini alikuja na hako kabinti, sasa kukaa tena nyumbani rafiki yangu akaona hapana, akatukaribisha wote kwenye glocery ya karibu na nyumbani, tukanywa pale binti alikuwa hanywi baadaye naye akaanza kidogo kidogo, muda ukaenda na miadi ikaianzia hapo.

Amesoma kiasi, siku hiyo sikuuliza, kaja Dar kufanya nini, nikapewa jibu.

Basi weekend iliyofuata tukakutana na kuelewana zaidi kwenye bar fulani hivi. Na mahusiano yakaanzia hapo!

Mara nikasikia kakorofishana na yule shemeji yangu, na kaamua kupanga chumba chake maeneo ya huko uswahilini. Akanikaribisha, nikamuuliza utawezaje kuishi mwenyewe binti mdogo hivi? Akasema atajua.

Basi nikaona mara akajiunga na wadada fulani hivi kwenda viwanja kufanya vibarua.

Kipindi ameshajua nafanya kazi wapi, sasa kila baada ya siku mbili au tatu nikawa namtembelea kwake, lakini mazingira ya pale kwake yalikuwa hayanifurahishi, kwa sababu kwanza nilimkuta analala chini kwenye mkeka na kagodoro kikuu kuu hivi na jiko la mchina na madumu dumu ya maji.

Kwa kifupi ni kisera sana, sasa kusema kweli niliingiwa na huruma tu, nikamnunulia baadhi ya fanicha, kwa sababu nilimwona kabisa huyu ndio kaamua kuja Dar.

Nilipojitahidi kujiondoa kwenye huo uhusiano kwa kumweleza nina mke, hakutaka kunielewa, nikizidisha siku bila kwenda kumwona nashtukia kaja ofisini. Nikaendelea kununua vitu vyake vya matumizi mpaka chumba kikajaa. Sasa na mimi mdogo mdogo nikawa najisahau nalala kule, lakini mara ya kwanza kabisa kulala kwake alinichezea mchezo, tulipotoka kupata kinywaji nikapitia kwake kidogo, sasa ule uchovu mara kausingizi kakanipitia, hakuniamsha ng’oo kwamba niende nyumbani, kaja kuniamsha karibia kunakucha niende kazini!

Ndio kwa mara ya kwanza nikawa nimelala nje! Nilimwelezaje mke wangu, hiyo ni story ninyingine tuiache.

Sasa mwaka umepita nimenogewa mtoto wa watu ana ujauzito wangu.

Mungu wangu sasa mimi nifanyeje, mume wa mtu tena wa ndoa. Kusema ukweli nilichanganyikiwa, lakini hata hivyo nilikuwa nategemea nini?

Basi baada ya muda akaenda kwao kujifungua na akajifungua salama, nikaenda kumtembelea na kuona wazee. Na nilienda kwa gari langu na rafiki mwingine. Tukalala pale asubuhi nikaona tunachinjiwa mbuzi. Tukala na majirani na ndugu kama 16 hivi walikuwepo, kusema kweli sasa dalili zote kwamba mimi ni mkwe tena wa heshima niliziona pale, ilipofika jioni tukaondoka kwenda kulala mjini yeye bado tukamwacha pale na mtoto wake
Hapo ulipoenda kwao na kuchinjiwa mbuzi ndio ulitambulishwa rasmi kama Mme. Pole

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaa, ndugu yangu, utaendelea asubuhi, mimi nilivyo sasa najiona kama sio mtu,
Sina usingizi, sili, hata nilvyosema naenda kula wala sikula chakula chenyewe kiliungua,

Hawa wanawake hawa we acha tu, Mungu atawageuzia kibao tu, yaani mimi ni mtu wa kukesha kabisa, hata kula sili, kwa shida gani hasa yarabi,?

Haya ngoja nikaoge nijiandae kwenda kazini, labda nitasinzia huko.
😂😂😂😂 We mzee nimecheka sana
 
Watoto wake sasa ndio wamemaliza la saba, nikawatafutia shule nzuri huko kanda, nauli kwenda tu ukihumuisha vikorokoro vyote tokea hapa mpaka afike shule kwa mmoja sio chini ya 200000, bado ada ambayo kwa mmoja kila baada ya miezi 3 ni sh500000 na mwingine kila baada ya miezi 3 ni 450000, na wakirudi unatuma pesa kama 100000, kwa mmoja....
Simple and plain piga chini huyo mwanamke anaekusumbua, baki na Bi mkubwa anaekuheshimu kusanya watoto wako wote bakinao watambukishe wajulikane na wajuane IMEISHA . Umri ulionao sio wa kuhangaikia mapenzi tena kama watoto unao jali familia yako tu. Achana na washenzi
 
Samahani km ntakwaza watu lakini mi naupenda uislamu wangu uliohalalisha wake wanne. Kwa kweli toka dunia ianze wanaume hawajawahi kutosha huyo Dada Leo miaka 20 na zaidi anaishia kuitwa mchepuko wakati angekua muislam angemuoa.

Kingine mbona wakurya wana mitala nnao huku kanda maalum yaani mitala kama zote .

Huyo demu nae kimeo 20yrs unakubali kufichwa km Arv vile...!!! Au ndo tamaa ya pesa mweee!pole yake aseh

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yes naishi na mwanamke sijamuoa. Nayeishi naye sitaki kumuoa namtaka yule mwingine.
Wote wana watoto wawili
Jumla 4 kids
Pair ya kwanza wamepishana miezi 8 wapo vidudu huko.

Pair ya pili wamepishana mwaka mmoja anasimama dede mwingine ndio kwanzaaaa.....

HAKI UCHAWI UPO DUNIANI[emoji3][emoji3][emoji3]
Wamepishana miezi 8, mmoja alizaliwa kabla ya miezi 9 ya mimba?
 
Mama mjengo umenipotea wewe, ila ukweli mama mjengo katika vitu navichukia ni michepuko, yani michepuko inapoteza sana ramani ya familia, stress, zinaongeza chuki ndani ya familia yako, ugomvi na mpasuko ndani ya familia yako, halafu pia bado nae lazima awe na mtu wake sasa yani ni mkanganyiko
Kweli kabisa Ba mjengo,nami nakupendea hapo tu,ila kuna kuzidiwa nguvu na matamanio ndio kasheshe linaanzaga
 
Baada ya kuiuza ile nyumba, na kipindi hicho ujue tayali alishaanza kuwa na kachuki fulani hivi ambako sikukaelewa, ila akili yangu ilinituma labda hakupenda tuuze ila nyumba, mimi sikujali,

Ila aliniomba kitu fulani nikifanye wakati wa kupokea ile pesa, ila wakati ananiambia mimi sikusikia vizuri maana naona hata yeye alikuwa na wasiwasi anachonieleza ndio maana maana Sauti yake haikutoka vizuri, nikamwambia naomba urudie unasemaje,

Akaniambia sasa nikasikia vizuri,

NAOMBA HIYO PESA NIWEKE MIMI,

Nikamuuliza kwa nini,? Kwani huniamini, na kwa nini huniamini wakati unajua kabisa wewe tayari ni wangu na tuna watoto, mimi sio mhuni najua lengo la kuuza nyumba ni kwamba tulikuwa na sehemu fulani na ni lazima pigs ua tuee na nyumba yetu nyingine ambayo imeisha ili tuishi sasa kama akina fulani,

Akanjibu, unajua............

Ndugu zangu naomba mguess alikuwa na maana gani na nimkubalie au nikatae?

Mawazo yenu wakati naendelea
Tuguess???[emoji15][emoji15][emoji849]

Are u serious we mbaba?

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Wakati bado kijana, nlishawahi ku twist mguu wangu, sasa wakati sina hasira najua namna ya kuutembelea na kukimbia kidzain fulani hivi,

Sasa kumbe wakati ule nakimbia nilijisahau nikautwist na kuangukavibaya, niliendelea kukaa pale chini, kwa muda huku nataka kunyanyuka nashindwa, baadaye nikajivuta na matako mpaka kwenye kiti, kusema kweli hata kwenye kiti sikuweza kukaa,

Nikaaa pale chini baada ya muda, ndio akaja yule mwanamke na watoto wakaninyanyua na kunikalisha kwenye kiti,


Watoto wakachemsha maji na kunikanda kwa chumvi, kusema kweli siku nilikuwa naenda kwa bi mkubwa, lakini sikuweza,

Lakini nilimpa taarifa kuna msiba umetokea ofisini kwetu na huyo ni mtu wangu wa karibu.

Kesho yake maumivu bado yalikuwa makubwa nikajijikokota mpaka CCBRT, picha ikaonyeshwa kitu kinaitwa sijui LIGAMENT, ndio imepata madhara madhara,

Ile pesa kusema kweli yule Mwanamke aliikatalia

NI BUASHARA GANI ANATAKA KUFANYA?

Nitaendelea
Huu ni mwaka gani?

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Mzee umesema ukistaafu una Kama 250m? Naomba nikufariji pindi utakapostaafu umehangaika Sana na majukum ya hapa na pale unahitaji kutulia Sasa na kula mema ya nchi...mi sihitaji kuzaa ucjal
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] inaitwa " changamka kabla hujazubaa"

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Jibu lake lilikuwa ni kwamba unajua wewe una mke mkubwa na una familia kubwa huko unaweza kutumia kwa mambo mengine, baada ya kufikilia sana, nikaona ana hoja. Na kwa kuwa lengo ni kujengea nyumba watoto na watoto ni wake, isitoshe hata hivyosikuwa Na lengo baya, basi nilimkubalia kumpa ile pesa,

Ila baadaye nilikuja kugundua kwa mala ya kwanza kule kuwa na kiburi na kisirani kipindi kile tunasubilia pesa ni usmuzi ambao nilimwambia kuwa, basi katika hiyo pesa naomba nitoe kama 15 m ili nikapunguze madeni yangu mbali mbali angalau na mimi nipumue nijione kama kweli nafanya kazi na mshahara nauona,

Maana zaidi ya miaka mitano kusema kweli nilikuwa nikipata mshahara halafu nalipa madeni na nakopa tena hapo hapo,

Ikitokea nimefanyaovertime au nimepata kasafari kidogo ndio hapo nalipia watoto karo zao na nyingine angalau kutumia wazazi,

Lakini kiujweli hali ilikuwa mbaya sana kipesa kipindi hicho, maana nilikuwa Manila madeni, mpaka kazi yenyewe nikaichukia,ilifikia kipindi nikataka kuacha na kazi yenyewe lakini nashukuru kipindi hicho kilipita,

Sasa baada ya kumwambia nitachukua ile 15 m ili nipunguze madeni yangu ALIGOMA

Na mimi nikamwambia basi angalau 10m vilevile akagoma, basi nikamwambia sasa pesa yote tukilipwa naweka kwenye Acc yangu, hapo ndipo akakubali na nikachukua sasa 15m yote nyingine itayobaki aweke yeye,

Nikamweleza mnunuzi kiasi fulani anipe mimi na kinachobaki aweke Kwenye Acc ya mke wangu,
Kwanza alishtuka lakini baada ya kumweleshaakakubali ila akinaambia niwe makini, na nisije nikampa matatizo,

Basi fungu la kwanza ilikiluwa ni 30 m ,
15 akaniwekea mimi iliyobaki ikawekwa kwa Mama
Tunaendelea


NINI KILITOKEA?
Kwahiyo alitaka hiyo ml15 uitafute kwa kutumia chanzo kingine ilhali anajua fika una madeni yaliyo kukalia shingoni na Mshahara wako wote asilimia kubwa unaishia kwenye Makato ya madeni hayo !?? Mzee Nisamehe lakini naomba niseme kwamba huyo mwanamke uliingia choo Cha kike ana ushetani ndani yake Hana huruma hata kidogo na wewe
 
Wanaume tunateseka kwa starehe ya dakka inakutesa maisha yako yote,kisa mtego wa kum. A

Kwasasa sikamatiki tena,nimefanya kosa Mara moja basi,kwasasa nimeforce kutumia condom mpaka nimezoea,utamu uko pale pale
Eti utamu uko pale pale

Pipi ikiwa ndani ya ganda ukaimung'unya unakutaa na ladha gani?

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Sasa baada ya kupokea lile fungu la kwanza
30m, mimi haraka sana nikaenda kupunguza madeni yangu, hata hivyo Hays kwisha,

Na yeye nikamwita kwamba tukae chini ili ile 15m yake tuipangie matumizi ya kwanza kabisa,

Ushauri wangu ilikuwa tununue kiwanja kwanza,

Sehemu ambayo sio ghari sana, Hapo sasa ndio kimbembe kilipoanza,

Ila kufupisha story nilimwambia basi wewe unataka tuanze na nini? Akanijibu hiyo pesa anataka afanyie biashara wakati ujenzi unaendelea, nikamwambia biashara mbona tumefanya na tunasnguka, hata hivvyo sio mbaya wewe kutaka kufanya biashara lakini ni bora tuwe na kiwanja kwanza.

Kusema kweli zogo lilikuwa kubwa ananipayukia na mimi natumia ubaba wangu sasa kulazimisha, ndio alipoamka kwenye kiti(tulikuwa tumekaa nje na watoto wanacheza hapo nje).

Alichoniambiakwa sauti kuu na kali ni kwamba

TOKA HAPA NA VISENTI VYAKO UNAVYONIPAGA,

Du ! Leo naambiwa visenti, yaani huyu mwanamke nimekopa pesa, nimempeleka ufundi cherehani, nimemfungulia saloon , grocer, mghahawa, dala dala, mtaji wa kuku wa kisasa.

Anaanguka namyanyua, anakopa vicoba anashindwa kumaliza nammalzia,

Nalipa watoto karo kwa mwaka jaribia Mil 6 na bado watoto ndio kwanza wanasafari, kwa nini ananivunjia heshima namna hii?

Kusema kweli sikujua kama niliokota jiwe au mti au ufagio, nimpige nao akawahi kukimbia, na mimi nikaanza kumfukuza, kama sijamrushia kila kitu ambacho mpaka leo sikijui, nikaanguka chini, yeye akaendelea sijui wapi , kusema kweli sikumwona,
Kuangalia nyuma naona watoto, kumbe na wenyewe wakawa wameshika mawe wanataka kunipigia nayo, nikaamka ili niwafukuze nikaenda chini tena , sasa hapo ndio nikaanza kusikia maumivu, na watoto wale kule wamesimama, sasa na wenyewe wanapaza sauti,
KWA NINI UNAMPIGA MAMA YETU SI UENDE KWENU!!!!!

Nitaendelea
Loooohhh masikini kumbe siku zote hizo alikuwa ameshaanza kuwajaza chuki taratibu bila wewe kujua

Duhhhhhhh [emoji26][emoji26][emoji26][emoji26][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119][emoji16]
 
Back
Top Bottom