Naomba ushauri: Niliacha pombe, kwa sasa nimerudi kwa kasi

sasa kataa bombe za stress,toka umeanza kunywa hizo pombe umesolve hizo stress hata moja...
Dah swali gumu hili,
Ila sijasovu kitu zaid ya kuongeza matatizo, kila siku naapa kuacha ila najikuta mulemule, badala ya kunywa ufurahi unajikuta unalia pekee ako
 
Kuna dawa inauzwa inauzwa 250000 na babuyangu

Yafuatayo zingatia
1) anayekuwekea kwenye pombe usimjue na Wala usijue
2) utatapika Sana hatakiwi kuzidisha

angekua ndomdogo wako au mkeo kalalamika wewe hujui ilikuwa tamusana hii ,ukiwekewa hiyo hutakuja gusa pombe maishani(abadani)

NB,haikufanyi uwe bwege
 
Dawa ya uraibu ni kuamua kutoka moyoni kuacha, kama uliweza kuacha miezi kadhaa nyuma utaweza kuacha kabisa though it is a struggle
 
Kuacha ulevi fulani ni tabu, mwaka wa 4 huu nimeacha ulevi wa kubeti...
Ulevi wa kwichi kwichi nikaamua nioe kabisa saa.. atleast siku hizi najitahidi kujizuia nakula kwa macho.

Kwanza jitahidi ujue kinachokufanya uwe mlevi, mfano ni kampani(marafiki), mawazo ama nini..
Kisha tizama kipi kinaweza kukuzuia, mfano mama yako ama kitu gani.. jiweke nacho karibu.

Ila mwanzo wa kujuta na kujilaumu, ndio mwanzo wa kuacha
 
Hutaki nyumba za ibada, basi nenda kwa waganga na wachawi.....jinga kabisa
 
Una kiu ya kutenda dhambi maana umefungwa ikafungika.Chagua maombi.Ukiombewa kiu itakata ya ulevi.
 
Andaa kikao tupige bia za mwisho wakati nakushauri,nipo hapa ROMBO GREEN VIEW HOTEL Shekilango
 
Si rahisi kutibu addiction bila kutafita addiction nyingine yenye unafuu, unaweza uka replace uraibu wa pombe kwa kujitengenezea uraibu mwingine kama vile mazoezi, kusoma vitabu etc
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…