Naomba ushauri nimewakosea sana wanaoenda kuwa wakwe zangu kutokana na mkanganyiko wa familia yangu/Sikutokea siku ya Send off

Kweli. Hafai kabisa kuwa mke.
 
Huyu hafai kabisa kuwa mke, ndo wale wananuna bila sababu ukimuuliza tatizo nini hasemi
 
Nagongea msumari,atulize akili ajue nini anataka

Kingsmann
 
Yaani nisamehe bure nimejikuta nimekuchukia ghafla kwa upumbavu ulioufanya, ulikua huna sababu ya kuzimia wakwe zako sim kwa vitu vya kuambiwa. Ungemweleza mama mkwe wako ukwel hata kama alikua kashafika huko kwenu, umekasirika kwa ujinga af kumbe habar sio za kwel. Muangalie vizur mama ako sijui kama ana mapenzi ya kwel na wewe. Yote kwa yote pole sana mweleze mwenzio huenda akakuelewa, mama mkwe wako muombe samahan hata kwa text hata kama haitatokea ukaolewa na huyo jamaa. Pole sana
 
Mama yako kwani hajui singo maza kuolewa Ni shughuli pevu? Huyo kijana alikufanyia fair Sana maana alijua na alikubali kukuoa, suala la yeye kuwadanganya kwao ungemuachia yeye.
 
Hii ni kwel kabisa
 
Mungu amekuepusha na janga kubwa sana huko mbeleni. Achana na huyo mchumba, ndio nimeandika hivyo wala sijakosea kwamba ACHANA NA HUYO JAMAA.

Kwa nini nasema hivi? Sababu kuu ni hizi hapa:

1. Umekiri mwenyewe kwamba kuna kitu alikuambia ambacho baada ya kumshirikisha mama yako alikugomea kabisa kuolewa na huyo jamaa na hata process za ndoa hajashiriki. That means hio kasoro aliyonayo huyo jamaa ni kubwa sana na haivumiliki sema ww utakuwa desperate na ndoa ndio maana umejitoa akili. Mzazi ni mzazi, amezaliwa kabla yako, kaona mengi na akikataa kitu jua kashajua kabisa hapo hamna mwisho mzuri.

2. Jamaa alishawahi kuchumbia kwingine lkn hakuoa. Sasa jiulize kwa nini hakuoa baada ya kuchumbia! Na kwako amejitahidi lkn mmeishia kwenye kutambulishana tuu, siku ya mahari ndio yametokea hayo. That means huko kwao ndio kuna shida mahali. Kaa naye chini muongee vzr akueleze vzr shida iko wapi.

Kingine ukitaka kupata ushauri mzuri eleza kinagaubaga kila kitu, acha kufichaficha, hata hiko kitu ulichosema huwezi kusema we sema tuu ili upewe ushauri unaoeleweka.

Unforgetable
 
Mama yako kwani hajui singo maza kuolewa Ni shughuli pevu? Huyo kijana alikufanyia fair Sana maana alijua na alikubali kukuoa, suala la yeye kuwadanganya kwao ungemuachia yeye.
Mama ake na hao ndg zake kiujumla wana shida sana, au hawapendi mtoto wao aolewe, hamuwez kuandaa sherehe alaf mkakimbikia bila kusikilizina na upande wa pili. Binti nae anashida angetoa taarifa ndg zake wamekimbia sababu wamesikia kuna tatizo fulani
 
Hicho kitu alishakisema kua ana mtoto na jamaa kakubal atamhudumia kwa kila kitu mtoto ila hataki kwao na jamaa wajue kua binti ni single mother. Mama ake ndo hataki anataka wakwe wajue kua ana mtoto
 
Wewe endelea na maisha yako, nimekuona hufai hata kidogo na huna sifa ya kua mke,kwa nini ulipo sikia jambo la aina hiyo hukuniuliza, unamaansha hata tukianza kuishi watu wakakuletea habari za uongo utaondoka mara moja huna akiri kabisa, halafu unakuja hapa jamvini kuanika upupu wako unazani mm sipo humu jamvini? Umenisababishia hasara kubwa pia umeniaibisha mimi, na familiy yangu mama yangu mpaka amekonda kwa ajili ya ujinga wako, nimeumia sana ila mungu atanipa mke mwema, pia inawezekena mungu kaniepushia jambo hapa,kwenda zako tena sitaki hata kukuona niache niendelee na maisha yangu.
 
Hii stori inamfaa coco wa twitter.
Ngoja nimsongezee
 
Ntachangia kwa namba Kama ulivyoweka hoja zako. Kabla nikiri kuwa umetoa hoja nzuri. Ila kwa uliyemshauri hazimtoshi
1. Alishakiri kuwa Jambo lenyewe ni kuwa jamaa hakutaka kwao wajue kuwa anaemuoa ni single mama. Ugomvi Kati ya binti na mama ake ni binti kuficha Siri ya kuwa na mtoto ukweli. Tena kwa maelekezo ya jamaa mwenyewe.

2. Kuchumbia ni suala moja na kuoa ni la pili. Sababu hatujajua sababu za jamaa kutomuoa wa kwanza. Tuliache kwa mtazamo Kama kwa binti hajatuambia alipo baba wa mtoto wake. Na kwann hakuolewa naye.

 
Hicho kitu ulichosema huwezi kutuambia sisi je ulimwambia askofu?
 
Duh, wazazi wako waharibu shahawa zao kukutengeneza, kwangu mm hili ni kosa ambalo halisameheki. Una uwezo mdogo sana wa kufikiri. Jamaa yako inabidi atoe sadaka ya shukrani ya pekee kutokukuoa.
 
Maneno ya kuambiwa,siku zote usipende kusikiliza maneno toka kwa watu ambayo hayana ukwelindani yake,fuatilia kiundani ujue nini hasa kilichomo

Pole sana, nakushauri waombe radhi wazazi wake waeleze yote yaliyokusibu naamini wataelewa
 
Usiri uliopitiliza huaribu ndoa nyingi sana,
Uoga wa wachumba kuogopa kumkosea mwenzio husababisha mambo kama Haya.

Yaani mtu unayechumbiana naye ni tofauti kabisa na mtu ambaye unaoana naye.

Unakutana na vimambo vya ajabu vya kushitua kisa mliogopa kuelezana ukweli wa mambo.

Yaani, vipi kama jamaa angekuwa muwazi kwa kila kitu kwako? Nadhani huo uvumi wa kwamba ameoa usingekuwa Tatizo.

Yaani, kabla hamjafanya utoto mlio ufanya, kulikuwa na shida gani wewe kumuuliza huyo mchumba wako ili akueleze kinaga ubaga?

Na kama familia mlikosea, maana ulikuwa rahisi ile wanafika na kosta yao mnawaingiza chemba mnayaongea na kuwekana sawa na sio kwa staili mliyoitumia ninyi ndio maana nmeuita ni utoto.

Ukikoroga, unywe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…