Naomba ushauri, nina mtaji wa milion 4 nifanye biashara gani?

Naomba ushauri, nina mtaji wa milion 4 nifanye biashara gani?

More Chances

Senior Member
Joined
Jun 24, 2022
Posts
151
Reaction score
344
Habari wakuu
Mimi ni kijana wa kiume age 29
baada ya michongo kwenda vibaya
nikashauriwa kuvungua duka la mangi kwa mtaji wangu milion 4
nikatafuta frame ya mtaani nikapata
ila issue ni kwamba kila
nikikaa na kuwaza naona kama sina mapenzi kabisa na hii biashara na kodi nshalipa , nishaurini deal za kupiga hata huko masokoni wakuu
 
Kumbe tatizo la vijana wengi sio kukosa mtaji. Tatizo ni ukosefu wa maarifa ya biashara. Hili tatizo linaanzia utotoni kwenye malezi ya wazazi. Mama mkwe wangu maisha yake yote ni biashara. watoto wake akiwemo mke wangu wamekulia sokoni. Wife aliniomba laki mbili afanye biashara. Amestawi Sana kwenye biashara yake. Lakini Mimi nina elimu ya chuo kikuu, nimeajiriwa nakopesheka mtaji ninao lakini chakufanya sikioni.
 
Kumbe tatizo la vijana wengi sio kukosa mtaji. Tatizo ni ukosefu wa maarifa ya biashara. Hili tatizo linaanzia utotoni kwenye malezi ya wazazi. Mama mkwe wangu maisha yake yote ni biashara. watoto wake akiwemo mke wangu wamekulia sokoni. Wife aliniomba laki mbili afanye biashara. Amestawi Sana kwenye biashara yake. Lakini Mimi nina elimu ya chuo kikuu, nimeajiriwa nakopesheka mtaji ninao lakini chakufanya sikioni.
Wewe ushaziweya kutumwaa ndio maana yake na hupendi kujituma hupendi kuwa huru.
 
Habari wakuu
Mimi ni kijana wa kiume age 29
baada ya michongo kwenda vibaya
nikashauriwa kuvungua duka la mangi kwa mtaji wangu milion 4
nikatafuta frame ya mtaani nikapata
ila issue ni kwamba kila
nikikaa na kuwaza naona kama sina mapenzi kabisa na hii biashara na kodi nshalipa , nishaurini deal za kupiga hata huko masokoni wakuu
Kwanza upo mkoa gan ili upewe muongozo nn chakufanya au nn uskufanye kutokana na mazngra uliopo
 
Kwauhitajaji wa odds 1.30 kila siku iendayo kwamungu njoo tukae kiofisi lifanyike hilo.utaweza kuingiza zaidi ya elfu50 kwasiku.
Ila kosa kubwa nikutaka hela nyingi uwe tajiri haraka.bali utalidhika nahiyo hiyo faida tuu kila siku.
Ukiwa tayari chukua namba hapo profile picture.
 
Habari wakuu
Mimi ni kijana wa kiume age 29
baada ya michongo kwenda vibaya
nikashauriwa kuvungua duka la mangi kwa mtaji wangu milion 4
nikatafuta frame ya mtaani nikapata
ila issue ni kwamba kila
nikikaa na kuwaza naona kama sina mapenzi kabisa na hii biashara na kodi nshalipa , nishaurini deal za kupiga hata huko masokoni wakuu
Ukiendekeza hisia kwenye biashara basi ujue bado hujakomaa kibiashara,, mfanya biashara anakuwa makini na mahesabu deal na faida sambamba namuda, mfanya biashara huwa anapenda biashara inatakayo mlipa kwa muda fulani, ukiwa kama mfanya biashara unatakiwa uwe na macho ya kuona mbele, mfanya biashara anaweza kufanya biashara ya kawaida lakini anakuwa ameona mbeleni hiyo biashara haitakuwa ya kawaida, Aliko Dangote ni mfanya biashara mwenye mafanikio makubwa sana lakini mafanikio yake yametokana na uwezo wake mkubwa wa kuona fursa, sio kwa sababu alipenda kitu fulani, mfanya biashara unatakiwa kupenda biashara yenye faida,,
Kama biashara yako ya duka inakulipa unatakiwa ukomae lakini pia uwe una mitazamo ya kukua kibiashara kama huna akili ya biashara wee nenda tu katafute ajira ukilazimisha sana kufanya biasha kwa mihemko utalia sana mkuu,,

Kiwango chako cha kufanya biashara kina pimwa kwenye uwezo wa kuona fursa na bidii na subira, kaa chini fikiria vizuri ni fursa gani unaweza kuwekeza

Kama huoni fursa mimi naweza kukushauri lakini pia naweza kukupa orodha ya fursa zilizopo hapa Tanzania ni nyingi sana sana mkuu huo mtaji wako ni mkubwa sana kiasi kwamba unaweza kuanzisha hata kampuni, mimi naona fursa nyingi sana ingawa kwangu mimi natamani kufanya project kubwa, lakini sina mtaji kwahiyo nimeanza na biashara ndogo ila wewe hiyo 4M naitamani sana mkuu ningekuwa nayo mimi 😂😂
 
Kila biashara inatoa Ila anzia sokoni na utafute MTU aliyetoboa tayari akucholee ramani au awe mentor wako

Ukifatisha maoni ya watu walioshindwa kutoboa utachanganikiwa Sana.

Anzia sokoni , usome mchezo then invest .
Dr Hapo umesema soko lina siri kubwa sana na hata msingi wake sio mkubwa lkn vijana wavivu hawataki kufanya kaziii.
 
Habari wakuu
Mimi ni kijana wa kiume age 29
baada ya michongo kwenda vibaya
nikashauriwa kuvungua duka la mangi kwa mtaji wangu milion 4
nikatafuta frame ya mtaani nikapata
ila issue ni kwamba kila
nikikaa na kuwaza naona kama sina mapenzi kabisa na hii biashara na kodi nshalipa , nishaurini deal za kupiga hata huko masokoni wakuu
Sasa kama ulishauriwa kufungua duka la Mangi, na ukafikia mpaka hatua ya kulipia fremu! Na bado umegundua huna mapenzi na hiyo biashara; huoni ni wakati wako sasa wa kuiamini nafsi yako, na hivyo kufanya ile biashara utakayoipenda!!

Unaweza kushauriwa kufanya biashara ya kuuza samaki! na wakati hapo ulipo hakuna mto, ziwa au bahari!! Fanya biashara yoyote ile inayoendana na mtaji na pia wateja wako.
 
Sasa hizo fursa umeona Tanzania mbona husemi, ama mpaka tukufuate pm?
Ukiendekeza hisia kwenye biashara basi ujue bado hujakomaa kibiashara,, mfanya biashara anakuwa makini na mahesabu deal na faida sambamba namuda, mfanya biashara huwa anapenda biashara inatakayo mlipa kwa muda fulani, ukiwa kama mfanya biashara unatakiwa uwe na macho ya kuona mbele, mfanya biashara anaweza kufanya biashara ya kawaida lakini anakuwa ameona mbeleni hiyo biashara haitakuwa ya kawaida, Aliko Dangote ni mfanya biashara mwenye mafanikio makubwa sana lakini mafanikio yake yametokana na uwezo wake mkubwa wa kuona fursa, sio kwa sababu alipenda kitu fulani, mfanya biashara unatakiwa kupenda biashara yenye faida,,
Kama biashara yako ya duka inakulipa unatakiwa ukomae lakini pia uwe una mitazamo ya kukua kibiashara kama huna akili ya biashara wee nenda tu katafute ajira ukilazimisha sana kufanya biasha kwa mihemko utalia sana mkuu,,

Kiwango chako cha kufanya biashara kina pimwa kwenye uwezo wa kuona fursa na bidii na subira, kaa chini fikiria vizuri ni fursa gani unaweza kuwekeza

Kama huoni fursa mimi naweza kukushauri lakini pia naweza kukupa orodha ya fursa zilizopo hapa Tanzania ni nyingi sana sana mkuu huo mtaji wako ni mkubwa sana kiasi kwamba unaweza kuanzisha hata kampuni, mimi naona fursa nyingi sana ingawa kwangu mimi natamani kufanya project kubwa, lakini sina mtaji kwahiyo nimeanza na biashara ndogo ila wewe hiyo 4M naitamani sana mkuu ningekuwa nayo mimi [emoji23][emoji23]
 
Sasa kama ulishauriwa kufungua duka la Mangi, na ukafikia mpaka hatua ya kulipia fremu! Na bado umegundua huna mapenzi na hiyo biashara; huoni ni wakati wako sasa wa kuiamini nafsi yako, na hivyo kufanya ile biashara utakayoipenda!!

Unaweza kushauriwa kufanya biashara ya kuuza samaki! na wakati hapo ulipo hakuna mto, ziwa au bahari!! Fanya biashara yoyote ile inayoendana na mtaji na pia wateja wako.
Huyo jamaa sidhani kama anayo elimu ya kutosha kwenye biashara, anahitaji mifano mingi sana ili akae sama
Watu wamefanya biashara za aina nyingi lakini si kwamba walizipenda zote, akiwa anataka kufika mahali fulani ni lazima uipende kila hatua unayo ipiga,
Nitoe mfano wa Ally yule mmiliki wa kampuni ya Lake oil grup
Alieza kuwa yeye alivo maliza chuo huko Canada mzee wake alianza kumzingua hela za matumizi, ndipo alipo amua kumuomba mtaji mzee wake alianza buashara ya mitumba aliifanya hiyo kwa bidii kwa muda wa miaka miwili alivo jikusanya vya kutosha aliamua kuhamia kwenye biashara za mafuta alianza kwa mtaji wake ule ule mdogo na alivofanikisha kuanza ndipo aliweza kukopeshwa na mabenki hadi sasa ipo kwenye nchi kadhaa ikiwemo kenya wanategemea sana mafuta toka kwa huyu jamaa,

Ushauri wangu kwa wewe jamaa tafuta kwanza spirit ya biashara ili ukiwasha moto uwake moja moja hadi hadi taifa litambue kuwa kuna kijana amewasha moto,, tafuta elimu zaidi,, jifunze kupitia historia za wafanya biashara mbalimbali hakuna mtu mkubwa asiye kuwa na historia ya msoto,, na maana halisi ya msoto ni kwamba mtu anakuwa kwenye hatua mbaya asiyo ipenda, vitu tunavyo vipenda havipatikani kirahisi mkuu
 
Habari wakuu
Mimi ni kijana wa kiume age 29
baada ya michongo kwenda vibaya
nikashauriwa kuvungua duka la mangi kwa mtaji wangu milion 4
nikatafuta frame ya mtaani nikapata
ila issue ni kwamba kila
nikikaa na kuwaza naona kama sina mapenzi kabisa na hii biashara na kodi nshalipa , nishaurini deal za kupiga hata huko masokoni wakuu
Si bure tiyari ushapigwa kidude(kurogwa).
Waswahili viumbe khatar sana.
 
Kwauhitajaji wa odds 1.30 kila siku iendayo kwamungu njoo tukae kiofisi lifanyike hilo.utaweza kuingiza zaidi ya elfu50 kwasiku.
Ila kosa kubwa nikutaka hela nyingi uwe tajiri haraka.bali utalidhika nahiyo hiyo faida tuu kila siku.
Ukiwa tayari chukua namba hapo profile picture.
Acha utapeli katafute kazi
 
Back
Top Bottom