Naomba ushauri wa Kisheria katika hili, nataka nivunje uchumba na huyu mwanamke

Naomba ushauri wa Kisheria katika hili, nataka nivunje uchumba na huyu mwanamke

Ndama Jeuri

JF-Expert Member
Joined
Jul 9, 2015
Posts
1,520
Reaction score
1,504
Habari za asubuhi wana jukwaa la sheria,

Kama kichwa cha mada kinavyojieleza hapo juu. Nipo kwenye mahusiano na binti mmoja wa miaka 23, nilifanikiwa kwenda kwao kujitambulisha na nikawa kwenye mpango wa kupeleka posa mwezi January mwaka huu, lakini ukatokea mvutano baina ya mama yake binti na mimi kuhusu suala la imani, mama yake binti akitaka nifuate imani ya mwanawe ili nimuoe binti yake, nilimwambia binti tubaki marafiki na uhusiano uvunjike kwa kuwa sitaweza kabadili imani yangu.

Baada ya kumwambia hivyo tulikaa siku kadhaa bila mawasiliano, lakini baadae alinitafuta kwa njia ya simu na kuniambia kuwa mama yake ameridhia yeye kubadili imani kunifuata mimi. Nikamuelewa mapenz yakarudi na ghafla akanasa ujauzito kipindi kile kile kifupi tangu aniambie mama yake hana tatizo Tena kwenye imani.

Nikamueleza kwa kuwa tayari una ujauzito mueleze mama yako unaenda kubadili Imani ili nilete posa tufunge ndoa haraka before huo ujauzito haujafika hata mwezi,binti akaanza kupiga chenga kumueleza mama yake, baada ya kumsumbua sana kwa wiki kadhaa akanipa jibu kuwa nimuoe Kwanza then atabadili dini akiwa kwangu, nadhani hakuna imani yoyote inaruhusu hilo iwe ya kikristo au kiislamu, yafaa umkili kristo ni bwana na muokozi wa maisha yako ndipo uoelewe na mkristo au ukili Mungu ni mmoja (Allah s.w) na Muhammad ni mjumbe wake ndipo uolewe na muislamu.

Hapo nikagundua kuwa binti aliongopa kuwa mama yake ameridhia abadili imani. Ikabidi nimtafute mama yake mdogo ambaye yeye imani yake inaendana na ya kwangu, kwani hata mama yake na huyu binti alibadili imani kumfuata mwanaume aliyemuoa sasa. Nikamueleza hali halisi na yule mama yake mdogo akanambia kuwa atamueleza dada yake ambaye ni mama yake na binti kuwa binti abadili dini ili posa iletwe,japo aliniambia kuwa mama yake hataki mwanawe abadili imani ila atazungumza naye.

Alimpigia simu na kumueleza suala hilo,lakini cha kushangaza usiku wa saa 4 siku hiyo aliyozungumza na mdogo wake, mama wa yule binti alimleta kwangu yule binti, kwa bahati mbaya sikuwepo nyumbani nilikuwa kazini, akamuamsha jirani mmoja na kumkabidhi yule binti, nikirudi kazini nikabidhiwe. Nilipopigiwa simu usiku na yule jirani nikamuambia amfungulie mlango yule binti kwa kuwa alikuwa na ujauzito wangu na sikuwa tayari kumtelekeza,nakumbuka ilikuwa tarehe 02/01/2020.

Niliporudi asubuhi toka kazini sikutaka kwenda kwao binti nikaa kimya tu kwa vile mama yake alikuja kwa uhasama. Mama yake baada ya kuona kimya akamwambia binti yake arudi, Binti akagoma kurudi ikabidi niletewe wito wa kwenda pamoja na mshenga wangu, nikaenda ukweni lakini nilipofika shutuma za kwanza nimemtorosha binti yao, hivyo nipigwe fine ya laki 2 pamoja na posa ya laki 2 na nikaambiwa wao wanahitaji mahali tu.

suala la nani,wapi tutafunga ndoa, tutajua wenyewe, kweli nilikaa siku kadhaa nikawapelekea hiyo laki 4 ,wakatoa majibu ya posa siku hiyo na waliorodhesha vitu vingi kweli kwa ujumla vilifikia 2,174,000. Baada ya siku kadhaa kupita nikapela pesa yote hiyo,walipo fikishiwa hiyo pesa wakasema kuna baadhi ya mambo hayajakamilika hivyo ni vizuri mshenga wangu afanye utaratibu wa kunichukua mimi pamoja na binti tuende kwa wazazi wake, hilo suala nikamgomea mshenga.

From there nikawa sina ushirikiano na familia ya binti na binti amenigeuka ananilazimisha kuwa lazima niwe Na ushirikiano na familia yake na sasa binti amebakisha miezi 2 ajifungue. Nataka kuvunja uchumba,na binti nimemwambia kuwa suala la kumuoa nimeshalifuta.

Amewaeleza kwao,na kwao wamemuambia kuwa aniambie nimtafutie pa kukaa kwavile itakuwa aibu kwake, kukaa kwa mwanaume muda mchache then akaachika. Nilikaa naye na kumvumilia kutokana na hali yake ujauzito lakini nimegundua kuwa hajihurumii.
Nataka nimtoe kinguvu nimpeleke kwao.

Na nikawaeleze wazazi wake kuwa nimevunja uchumba. Naomba msaada wa kisheria kama kutakuwa na sehemu nitakosea juu ya uamuzi wangu?.

Au Kama kutakuwa na utaratibu mzuri wa kisheria wa mimi kuufuata ili wasiweze kuutumia ujauzito na mtoto anayetazamiwa kuzaliwa kama mgodi wa kuchimba hela.
 
Ngoja nisubili manguli wa hizi mambo....pole kwa changamoto...ndio ukubwa.
 
Hiyo mimba inawezekana sio yako.

Kwa namna unavyoeleza, inaonekana alijigundua ana mimba ndio akaja kwako tena, kwa gia kwamba mama yake amekubali!!! Na wala hakuelezwa kitu, sasa mama alipoona ameelezwa na mimba hiyo kaona itakua aibu, akamleta kwako bila kupenda!

Unavyoandika ni kama vile umekuwa mzito kung'amua mambo fulani.

Ntarudi kusoma comments
 
Hiyo mimba inawezekana sio yako.

Kwa namna unavyoeleza, inaonekana alijigundua ana mimba ndio akaja kwako tena, kwa gia kwamba mama yake amekubali!!! Na wala hakuelezwa kitu, sasa mama alipoona ameelezwa na mimba hiyo kaona itakua aibu, akamleta kwako bila kupenda!

Ntarudi kusoma comments
Asante kwa maelezo yako, kwani yamefanya nielewe story nzima.
 
Mkuu wewe naye mbona sikuelewi,umesema umeshatoa mahali kiasi cha 2M+ lakini bado unasema huyu binti ni mchumba,au hujui màana ya neno mchumba? Huyo sio mchumba wako kwa sasa Bali ni mke.

Uchumba ni hali ya mwanamke na mwanamme kuwa marafiki wa karibu kwa lengo la kujuana ili kuwa mke na Mme.

Ndoa ni muunganiko wa hiyari kati ya mwanamke na mwanamme kama mke na Mme

Hivyo wewe tayari umeshaungana na Huyo binti,theni usiseme ni mchumba ila sema mke.

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Mkuu wewe naye mbona sikuelewi,umesema umeshatoa mahali kiasi cha 2M+ lakini bado unasema huyu binti ni mchumba,au hujui màana ya neno mchumba? Huyo sio mchumba wako kwa sasa Bali ni mke.

Uchumba ni hali ya mwanamke na mwanamme kuwa marafiki wa karibu kwa lengo la kujuana ili kuwa mke na Mme..
Upo sahihi kabisa mkuu
 
Aahhh Mzee Baba, Embu Tuliaa, kwan binti mwenyewe anataka kuondoka?.? ?
Habari za asubuhi wana jukwaa la sheria,

Kama kichwa cha mada kinavyojieleza hapo juu. Nipo kwenye mahusiano na binti mmoja wa miaka 23, nilifanikiwa kwenda kwao kujitambulisha na nikawa kwenye mpango wa kupeleka posa mwezi January mwaka huu, lakini ukatokea mvutano baina ya mama yake binti na mimi kuhusu suala la imani, mama yake binti akitaka nifuate imani ya mwanawe ili nimuoe binti yake, nilimwambia binti tubaki marafiki na uhusiano uvunjike kwa kuwa sitaweza kabadili imani yangu....

Alafu huyo umeshamtolea mahali, ni Mkeo huyo semea labda unataka kufunga Ndoa.
 
acha maamuzi ya haraka mkuu, mvumilie binti na familia yake kwa malezi bora ya mwanao ajae
 
- Umeishi na unaishi nae nyumba moja.

- Umemzalisha mtoto.

- Na kikubwa zaidi umemlipia mahali.

Bro huyo ni mke wako, hapo sio kuvunja uchumba ni kuvunja ndoa, unachotakiwa kufuatilia ni sheria za taraka.[emoji1][emoji1]
 
- Umeishi na unaishi nae nyumba moja.

- Umemzalisha mtoto.

- Na kikubwa zaidi umemlipia mahali.

Bro huyo ni mke wako, hapo sio kuvunja uchumba ni kuvunja ndoa, unachotakiwa kufuatilia ni sheria za taraka.[emoji1][emoji1]
kuna ndoa inayotambulika kisheria bila cheti cha ndoa?
 
Mkuu wewe naye mbona sikuelewi,umesema umeshatoa mahali kiasi cha 2M+ lakini bado unasema huyu binti ni mchumba,au hujui màana ya neno mchumba? Huyo sio mchumba wako kwa sasa Bali ni mke...
Je, sheria inatutambua kama wanandoa,ikiwa hatuna cheti cha ndoa,na hatujaishi pamoja zaidi ya miaka miwili?
 
Kisheria bado hajawa mke

Mosi: Kutoa mahari pekee na kutambulika ukweni, hakumfanyi mtu kuwa mke (ndoa haijafungwa Kanisani, Msikitini, wala Bomani)

Pili: Kuna ile sheria inayotambua mtu kuwa mume na mke endapo wameishi miaka 2 na mashajidi wakadhihiriasha hivyo

Haya mambo yote hayajafanyika, huyo binti bado ni mchumba
Mkuu wewe naye mbona sikuelewi,umesema umeshatoa mahali kiasi cha 2M+ lakini bado unasema huyu binti ni mchumba,au hujui màana ya neno mchumba? Huyo sio mchumba wako kwa sasa Bali ni mke.

Uchumba ni hali ya mwanamke na mwanamme kuwa marafiki wa karibu kwa lengo la kujuana ili kuwa mke na Mme...
 
Kisheria bado hajawa mke

Mosi: Kutoa mahari pekee na kutambulika ukweni, hakumfanyi mtu kuwa mke (ndoa haijafungwa Kanisani, Msikitini, wala Bomani)

Pili: Kuna ile sheria inayotambua mtu kuwa mume na mke endapo wameishi miaka 2 na mashajidi wakadhihiriasha hivyo

Haya mambo yote hayajafanyika, huyo binti bado ni mchumba
Ahsante mkuu
 
Kisheria bado hajawa mke

Mosi: Kutoa mahari pekee na kutambulika ukweni, hakumfanyi mtu kuwa mke (ndoa haijafungwa Kanisani, Msikitini, wala Bomani)

Pili: Kuna ile sheria inayotambua mtu kuwa mume na mke endapo wameishi miaka 2 na mashajidi wakadhihiriasha hivyo

Haya mambo yote hayajafanyika, huyo binti bado ni mchumba
Marekebisho hapo kwenye miaka, sheria ilishafanyiwa marekebisho siku hizi ni miezi sita,na hawa tayari washakaa zaidi ya miezi sifa,hivyo hawa ni mke na mume

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Mkuu kama unaweza ku screen shot hicho kipande kinachosema miezi sita, tuma hapa

Vinginevyo ninachojua ndio hicho, na mwaka huu au jana mwishoni katika pita zangu nimekutana na kitu kama hicho (miaka 2)

Miezi 6 huwa ni lugha inayotumika mtaani ambayo ni wrong (mfano niliwahi kuaminishwa miaka ya nyuma kuwa baba anaweza kuchukua mtoto alifikisha tu miaka 4 kumbe sio)
Marekebisho hapo kwenye miaka, sheria ilishafanyiwa marekebisho siku hizi ni miezi sita,na hawa tayari washakaa zaidi ya miezi sifa,hivyo hawa ni mke na mume

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Sijui sheria ila nashauri mtoto akizaliwa tu upime DNA kama wa kwako rasimisha. Kama sio unakua na sababu mahsusi ya kuvunja huo uchumba
 
Sijui sheria ila nashauri mtoto akizaliwa tu upime DNA kama wa kwako rasimisha.,

Kama sio unakua na sababu mahsusi ya kuvunja huo uchumba
suala la kurasimisha ni gumu kidogo,kutokana na kuwepo kwa historia ya uhasama baina yangu na wazazi wake,na pia hata ningemuoa bado nisingekuwa na ushirikiano na familia yake,hivyo solution ni kuvunja uchumba
 
Back
Top Bottom