Naomba ushuhuda kwa watu waliokuza mitaji yao kupitia vikoba

RUSTEM PASHA

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2016
Posts
4,707
Reaction score
11,365
Wakuu salama.
Kuna watu wamekuwa wakinishiwashi niingie kwenye vikoba kuwa ntapata mikopo yakukuzia biashara. Nilikuwa naomba watu waliofanikiwa kukuza mitaji kupitia vikoba wanieleze kwa undani, maana hawa wanaonishauri niingie wananiambia faida za vikoba tu ni kiwauliza hasara zake ni nini hawaniambii.

Mimi binafsi ni mwanafunzi chuo wa mwaka wa mwisho, lakini nimebahatika kuajiri watu wanne, wawili kwenye saluni barbershop, mmoja kwenye banda la mpira na mwingine kwenye mchele lakini nilihitaji nikuze mtaji zaidi. Sasa nashawishika kuingia kwenye vikoba ingawa akili yangu pia inasita.

Naombeni ushuhuda kwa waliofanikiwa.
 
Kwani bado unaendelea na course yako ya uhandisi,? Mchele kuuza uliacha? Daa mkubwa nikikumbuka kipindi kile unatembeza mchele najikuta hata mimi nijiingize kwenye biashara ndogondogo na ukatengeneza banda la mpira sasa sijui iliishia wapi bado unaendelea na kuonyesha mpira au uliacha



Wewe mpambanaji achana na vikoba kwanza ingia cryptocurrency utanikumbuka
 
Vikundi vya VICOBA vipo vuzuri na vipo ambavyo vinawaacha watu kwenye majuto. Watu wengi sana wamenufaika na vikundi vya VICOBA hilo halina upinzani. Unachotakiwa ni kujiunga katika kikundi ambacho kinazingatia kanuni na taratibu hapo utafurahia lkn kama Hautapata Kikundi kizuri Ohhhhh Utaishia kujuta
 
Yaan mm najuta na vikoba.yn hapa natamani nitukane zinga la tusi ,ndio kama nahisi ntafarijika.mkuu kua makini na vikoba.
 
Yea nipo mwaka wa mwisho wa nne,mchele bado nauza nilifungua frem nauzia kwenye frem ingawa pia nasambaza,banda la Mpira bado lipo pia nimefungua kisaluni cha kiume.

Sasa kuna watu wananishauri niingie kwenye vikoba,nilitaka nifahamu na ubaya wake pia.
 
Nimekuelewa mkuu,vipi kikiwa kibovu fedha ulizotoa hazirudishwi?.
 
Yaan mm najuta na vikoba.yn hapa natamani nitukane zinga la tusi ,ndio kama nahisi ntafarijika.mkuu kua makini na vikoba.
Mkuu funguka vikoba vilikufanyaje kiongozi?.Maana watu wanaelezea mazuri tu nilitaka nifahamu naubaya wake kwa mtu aliewahi kushiriki.
 
Kuna vikoba hapa kwanza kila wiki unapiteza 4000, hiyo mnachangia afya, ukiumwa, ukifiwa haiwahusu.


Kukopesheka ni baada ya mwaka km una shida ya haraka ni ngumu kupata...!!!

Utafaidika na vikoba kama unatembeza biashara kule ni kuinuana ukikutana na mwana vikoba mwenzio anakuchangia....!!!
 
Nimekuelewa kiongozi,sio kwamba kila kikoba kinakuwa na kanuni zake na taratibu?.Je wewe binafsi hukufaidika chochote na vikoba?
 
Nimekuelewa kiongozi,sio kwamba kila kikoba kinakuwa na kanuni zake na taratibu?.Je wewe binafsi hukufaidika chochote na vikoba?
Sijajiunga mkuu... Nilielezwa hizo options na mwenyeji wangu anayeshauri nijiunge vikoba.


Ila kwa vile nilitaka hela ya chap isiyo na Riba kubwa naona nakwama... Vikoba vyafaa sama km wewe ni mwenyeji wa sehemu hiyo. Ila kwa sie wapitaji ni shida....!!
 
OK asante kiongozi,nimekuelewa vizuri nilikua nasikia kuwa wanatoa mkopo wa viwanja kwa bei nafuu sasa nami nilitaka niingie.December mwaka huu nami nichukue kakiwanja maana maisha magumu sana napesa yakulipa kwa pamoja nishiida kuipata,pia nikuze namtaji.
 
OK asante kiongozi,nimekuelewa vizuri nilikua nasikia kuwa wanatoa mkopo wa viwanja kwa bei nafuu sasa nami nilitaka niingie.December mwaka huu nami nichukue kakiwanja maana maisha magumu sana napesa yakulipa kwa pamoja nishiida kuipata.
Duu vikoba? Wanatoa viwanja kwa bei nafuu??
 
Duu vikoba? Wanatoa viwanja kwa bei nafuu??
Kuna taasisi zinazokowakopa wanachama wa vikoba viwanja,bodaboda, bajaji kwa riba nafuu kwa namna nilivoambiwa but sina uhakika.Pia niliambiwa kuna vikoba endelevu,na vikoba visivyo endelevu.Vile visivyo endelevu huvunjwa mwisho wa mwaka.
 
Hivi vya mitandaoni siviamini kabisa na sijawahi, navisikiaga tu eti wanafaidika
 
Kila Vicoba ina sheria zake. Kwa mfano sisi chetu unaweza kukopa miezi mitatu baada ya kununua hisa na unapewa mkopo mara tatu ya hela uliyoweka. Hasara ni kwamba ukiingia vicoba ya watu wasiowaaminifu utalizwa. Zaidi ya hapo Vicoba ina faida sana
 
Kila Vicoba ina sheria zake. Kwa mfano sisi chetu unaweza kukopa miezi mitatu baada ya kununua hisa na unapewa mkopo mara tatu ya hela uliyoweka. Hasara ni kwamba ukiingia vicoba ya watu wasiowaaminifu utalizwa. Zaidi ya hapo Vicoba ina faida sana
OK asante Mzigua90 nimekuelewa vizuri.
 
Naona matangazo fb mkuu, wanatoa na pikipiki, bajaji nk, hadi mh 4th prezdaa anahamasisha, ndo maana nimesema siamini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…