Naomba ushuhuda kwa watu waliokuza mitaji yao kupitia vikoba

Naomba ushuhuda kwa watu waliokuza mitaji yao kupitia vikoba

vikoba watu inabidi wapate elimu ya kutosha ili kujiunga;akili za watu wengi wanawaza kujiunga vikoba kwaajili ya kukopa tu hapo ndo shida pia mkopo wa vikoba hauhitaji uchukue kwaajili ya pesa ya matumiz au starehe vikoba ni kwaajili ya kujiinua binafsi siwez kuacha kucheza vikoba kwa sababu zifuatazo nakopa mala3 ya hisa zangu riba ya mkopo ni ndogo na mwisho kuludisha mkopo miez3 Hua Nina tabia ya kuchukua mkopo vikoba kwaajili ya kuboresha biashara zangu yaani nachukua 1 million baada ya miez mi3 naludisha million moja na elfu50 hapo hiyo elf50 ni faida yangu nitaichukua mwisho wa mwaka baada ya kuvunja vikoba hivyo nikichukua hiyo 1 million baada ya miez mi3 inanipa faida zaidi ya laki 5 kwahyo naludisha pesa yao na riba ya mkopo kisha nabaki na faida zangu nafanya hivyo kila mala na hakuna kikomo cha kukopa Hua nalipa deni na kukopa papo hapo ninavyofanya hivi napata faida zaidi ya mala1 faida ya kwanza biashara zangu haziyumbi yaani mtaji unasimama hauyumbi wakati huo nazalisha faida lkn pia napata faida ninavyokopa mala kwa mala faida hiyo napata mwisho wa mwaka pindi twavunja USHAURI WANGU vikoba husaidia wajasiliamali kuboresha vibiasha vyao na sio watu wasiojishughulisha kutegemea pesa ya mkopo wa vikoba kwaajili ya kulipa pango,ada,kuhonga au starehe ndio mana watu huona vikoba havifai
 
Shida Ya Vicoba Ni Marejesho Tena Mkiwa Mnafahamiana Hata Kudaiana Mnashindwa Matokeo Yake Vinakufa
 
Yea nipo mwaka wa mwisho wa nne,mchele bado nauza nilifungua frem nauzia kwenye frem ingawa pia nasambaza,banda la Mpira bado lipo pia nimefungua kisaluni cha kiume.

Sasa kuna watu wananishauri niingie kwenye vikoba,nilitaka nifahamu na ubaya wake pia.
CHASHA FARMING njoo hapa uone biashara za uchuhuzi
 
Hizo biashara za uchuuzi mkuu ndio zinasababisha tuishi vizuri, huku tukielekea kwenye malengo makubwa.
Biashara ya mchele na nafaka zingine mauzo sipungufu ya laki nne kwa siku,banda la Mpira faida kwa mwezi sio pungufu ya 400K , saluni kwa mwezi faida 210K.Na pia kwa sasa nina biashara ya utumbo wa ng'ombe kwa siku mabanda mawili 14K, kwa mwezi 420K.Na hapo utumbo,banda la Mpira,saluni siwafahamu nakuwajua TRA.

Fanya hesabu zako uone napata faida kiasi gani,na nikufahamishe tu mpaka sasa nimenunua shamba hekari 31 Kilosa nahitaji nikalime mpunga,nimechukua hekari 10 Kimange huko. Lengo la uchuuzi nikuelekea lengo kuu .

Cha mwisho nina degree ya Mechanical ngineering na nimekataa kazi ya Kulipwa 720K. Baada ya miaka miwili kutoka sasa tutafutane.
Kweli na hongera kwa juhudi zote bara la Asia ambalo walikuwa wabovu kuliko afrika walijikita na wanajikita na uchuuzi na wapo mbali kwenye biashara kubwa.
 
Mkopo unaurudisha baada ya muda gani?
lengo lao ni kuchukua watu wa hali zote, za juu na za chini,,

kila wiki wanakutana, kima cha chini elf 2,

mwenye kipato kidogo anatoa elf 2, so kwa mwezi atakuwa ametoa elf 8,,

kama uko poa unaruhusiwa kutoa zaidi,

unaruhusiwa kukopa ×3 cha ulichochangia,, kama kwa mwezi ulichangia laki 3, basi unaweza kukopa laki 9.

hichi hakibagui kipato,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
How is this possible? Ili hali akaunti ya kikundi wanaitakiwa kutoa pesa hawatakiwi kua chini ya wawili?
Naona ndo kama mfumo wa vicoba unavyokua. Ila Vicoba watu wakishakua wengi sana ni changamoto. Kuna kikundi kimoja mwenyekiti alikula 50M. Wanakuja kushtuka hamna hela kwenye account.
Vicoba ni nzuri sana. Huwa natamani kila mtu angekua kwenye vicoba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Be blessed uchambuzi murua sana huu!
Habari mkuu. Sinaufahamu sana na vikoba lakini najua lengo la vikoba nikukuza mtaji na kuwezesha kupata mtaji kwa njia ya mkopo kwa watu ambao kwenye mfumo wa kibenki hawakopesheki. Mfano kama ww ni mwanafunzi,hauna nyumba kama dhamana kukopea benki hivyo kimbilio ni huko. Sasa cha msingi ni je wewe unahotaji nn toka huko kikoba? Swala sio kujiunga tu coz kama mtaji wako unajitoshereza kwa sasa hakuna haja ya kufanya hivyo. Pia nafikiri kama hauna iman na kikoba basi unaweza kuopt saccos coz nazo vigezo na mashart vinaendana na vikoba na tofauti n ndogo sana.
Kuhusu risk kila sehemu risk zipo rejea benk zilizofungwa juzi hapo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom