Naomba wasifu wa mtafsiri wa movies na series za abroad anaefahamika kwa jina la OMMY DJ

Lipia tangazo
 
Binafsi muvi ikishatafsiriwa hasa kwa namna hiyo ya hao madj napoteza mzuka hata wa kuicheki, wengi wanadanganya sana.
Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya kuwa na low IQ, kupenda bongo movies na kuangalia movies ZILIZOTAFSILIWA....🚮🚮
 
Noma sana. Watafsiri movie wana kamba sana muda mwingine wanaharibu kabisa story na kueleza vitu tofauti. Movie pekee ninazoweza kutazama ni zile zilizokuwa dubbed kwa lip sync tena professionally.
Otherwise bora nisome subtitles kama lugha haieleweki. Nilikuja kugundua nilikuwa nadanganywa baada ya kurudia kutazama movie za zamani zilizokuwa zinatafsiriwa na Mkandara Rufufu (RIP). Alikuwa anatupiga kamba sana na kubadilisha hata story.
Ukinipatia movie iliyotafsiriwa na hawa maDJ siwezi kuitazama kabisa.
 
Ni Faza mmoja hivi, nakumbuka nikiwa yanki kabisa alikuwa anatangaza picha Arusha na Mererani BCBG.
Karibuni amekuwa aki record na Full Respect Family ya DJ Murphy na Pirates Studios
Miongoni mwa MaDJ wa mwanzo kurecord movie za kutafsiri, kwenye kanda za VHS.
Binafsi naona anajua sana History na geography. Ingawa ni muongo pia kwaajili ya kunogesha.

Kama amefungiwa(au sijaelewa) itakuwa kwasababu ana tukana wakati mwingine, hasa mtu mweusi akinyanyaswa na watu weupe kwenye movie
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…