MAZINGIRA YENYE UTATA KUHUSU MKATABA WA BANDARI
Kuna mazingira yenye utata mkubwa na yanayoibua hisia na maswali mengi kutoka hatua ya MoU, kusainiwa na kuridhiwa kwa mkataba huu wa IGA, nitaongelea vipengele vitano kama ifuatavyo.
(a) Kampeni za wazi, Spika wa Bunge kuandaa ziara mwezi Februari 2023 ya wabunge 60 kutembelea maeneo ambayo DP World amewekeza na maeneo mengine Duniani ili kujifunza uwekezaji wa sekta binafsi katika uendeshaji wa bandari. Zoezi hili lilifanyika wakati mkataba haujatangazwa wala kufahamika kwa wananchi na wabunge wenyewe lakini pia ziara hiyo inatuhumiwa na wananchi kugubikwa na rushwa kubwa ili kulishawishi
Bunge kuipa upendeleo Kampuni ya DP World.
(b)Baadhi ya Viongozi na watendaji wa Nafasi za juu serikalini kuondolewa kwenye Nafasi zao bila Maelezo yoyote akiwemo Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari, Eric Hamis aliondolewa tarehe 4/7/2022, Katibu
Mkuu Kiongozi Balozi Hussein Katanga na Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa, Kamishna Diwani Athumani ambao waliondolewa kwa pamoja tarehe 3/1/2023. Viongozi wote hawa waliondolewa ndani ya kipindi cha
mchakato wa MoU na Kuridhiwa kwa mkataba huu na Bunge.
(c) Kuchukua kipindi kirefu cha miezi 8 kuingia Mkataba tangu kusainiwa MoU na katika kipindi hicho Serikali haikufanya tathmini wala feasibility study kujua mahitaji na manufaa ya mradi.
(d)Kutangaza kufanyia marekebisho ya Sheria ya Manunuzi na Sheria za Ulinzi wa Rasilimali kabla ya kuingia Mikataba ya HGAs baina ya TPA na DP World.
(e) Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Mbarawa na timu ya Serikali ya majadiliano kuendelea kutoa Ufafanuzi wa Mkataba wa IGA badala ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Jaji Dk. Eliezer Mbuki Feleshi na Baba wa Mikataba na Baba Negotiation, Mhe. Profesa Palamagamba Aidan Mwaluko Kabudi. Viongozi hawa wamekaa kimya badala ya kujitokeza hadharani wawaeleze watanzania ukimya wao unasukumwa na nini?
Kuna mazingira yenye utata mkubwa na yanayoibua hisia na maswali mengi kutoka hatua ya MoU, kusainiwa na kuridhiwa kwa mkataba huu wa IGA, nitaongelea vipengele vitano kama ifuatavyo.
(a) Kampeni za wazi, Spika wa Bunge kuandaa ziara mwezi Februari 2023 ya wabunge 60 kutembelea maeneo ambayo DP World amewekeza na maeneo mengine Duniani ili kujifunza uwekezaji wa sekta binafsi katika uendeshaji wa bandari. Zoezi hili lilifanyika wakati mkataba haujatangazwa wala kufahamika kwa wananchi na wabunge wenyewe lakini pia ziara hiyo inatuhumiwa na wananchi kugubikwa na rushwa kubwa ili kulishawishi
Bunge kuipa upendeleo Kampuni ya DP World.
(b)Baadhi ya Viongozi na watendaji wa Nafasi za juu serikalini kuondolewa kwenye Nafasi zao bila Maelezo yoyote akiwemo Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari, Eric Hamis aliondolewa tarehe 4/7/2022, Katibu
Mkuu Kiongozi Balozi Hussein Katanga na Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa, Kamishna Diwani Athumani ambao waliondolewa kwa pamoja tarehe 3/1/2023. Viongozi wote hawa waliondolewa ndani ya kipindi cha
mchakato wa MoU na Kuridhiwa kwa mkataba huu na Bunge.
(c) Kuchukua kipindi kirefu cha miezi 8 kuingia Mkataba tangu kusainiwa MoU na katika kipindi hicho Serikali haikufanya tathmini wala feasibility study kujua mahitaji na manufaa ya mradi.
(d)Kutangaza kufanyia marekebisho ya Sheria ya Manunuzi na Sheria za Ulinzi wa Rasilimali kabla ya kuingia Mikataba ya HGAs baina ya TPA na DP World.
(e) Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Mbarawa na timu ya Serikali ya majadiliano kuendelea kutoa Ufafanuzi wa Mkataba wa IGA badala ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Jaji Dk. Eliezer Mbuki Feleshi na Baba wa Mikataba na Baba Negotiation, Mhe. Profesa Palamagamba Aidan Mwaluko Kabudi. Viongozi hawa wamekaa kimya badala ya kujitokeza hadharani wawaeleze watanzania ukimya wao unasukumwa na nini?