Naombeni kufahamishwa namna tofauti za upishi wa dagaa

Swahili_Patriot

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2018
Posts
358
Reaction score
831
Nipo chuo na ninaishi na mshkaji wangu. Huyu jamaa ninayeishi nae, ni mpenzi mkubwa sana wa dagaa. Ila, jamaa hawezi kuzipika.

Kwa wiki ni LAZIMA tuzile angalau mara 1 ila ladha ndio mtihani.

Nilikuwa ninapenda sana kula dagaa ila huyu jamaa ameniharibia kabisa taste yangu.

Kwa wenye ujuzi wa upishi wa dagaa, naomba mnisaidie recipes tofauti tofauti.

Kuhusu viungo sio shida, nitanunua tu.

Asanteni
 
Napenda dagaa wa Mwanza ila wale wasio na michanga wanakua na vimajani kidogo

1. Pasha maji yawe ya vuguvugu kwa ajili ya kuoshea dagaa, osha mpk wawe wasafi

2. Km mpenzi wa tangawizi na limao, kwangua tangawizi changanya na dagaa kamulia na kimao

3. Andaa carrot, nyanya za kutosha, kitunguu na hoho

4. Weka mafuta jikoni yapate moto, weka kitunguu kikikaribia kuiva weka dagaa wakaaange vizuri wawe wanaelekea kukauka halafu weka nyanya na carrot

5. Zikikaribia kuiva weka hoho, acha zichemke mpk nyanya ziive (ile shombo ya nyanya mbichi iishe kabisa)

NB. Dagaa inataka nyanya na mafuta ya kutosha ya kukaangia

Sent from my CPH2015 using JamiiForums mobile app
 
Safi sana mkuu.
 
Dagaa wa aina gani kwanza!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…