Alichosema ni kwamba, kabla hajawauzia mkopo kutoka Loan Board, alikuwa na mkopo wa NMB! Baada ya kuwauzia mkopo, aka-top up, na kiwango alichopata kutokana na ku-top up, akabakiwa na TOTAL LOAN X (NMB + Board Loan) na mwenyewe alitarajia angebakiwa na Sh. 5,660,000/=
Lakini kwavile ali-overdrawal, akajikuta ana DENI la Sh. 4,234,000... huu sio mkopo bali deni!
Ndo maana nikasema jumla ya pesa anayodaiwa ni ule mkopo uliotokana na kuwauzia deni la Loan Board ambao ulichanganywa na mkopo wa NMB + TZS 4,234,000 .
Hii 4,234,000 haiwezi kutokea kwenye salary sleep, na ndio maana akaunti yako ina negative balance ili mshahara ukiingia according to salary sleep, automatically utakatwa na system... I bet system itakuwa set kwamba kila ikifika tarehe fulani, itungue utakaoingia kwenye akaunti! Kwahiyo hapo uingie mshahara au pesa kutoka chanzo chochote kile, itatunguliwa juu kwa juu unless hiyo pesa/mshahara iwe imeingia b4 a set date!
Kuhusu hiyo miezi 8, naona hajaweka bayana, manake amesema tu kwamba "... na sasa wanashikilia mshahara wote mpaka deni liishe ni zaidi ya miezi 8 na wote tunajua maisha ya mfanyakazi bila salary. " Sasa kama anachomaanisha imebaki zaidi ya miezi 8 deni kwisha, ina maana hadi mwezi huu atakuwa tayari ameshalipa miezi 6 kwa sababu alichukua loan mwezi wa 2.
Hapo pia, ktk mazingira ya kawaida anaweza kufanya top up kama ameshalipa 6 installments. Top up atakayofanya sio ya hiyo TZS 4,234,000 bali ya ule mkopo wake! Sasa akifanyashafanya top up, ile surplus ndiyo ataitumia ku-clear deni la TZS 4,234,000.
Kutegemea na mshahara wake, hiyo surplus baada ya top up inaweza kufuta deni lote la 4,234,000 au sehemu yake! Na kama atabaniwa kufanya top up kwa kuona ule mkopo wake rasmi hajalipa kwa kiasi kinachompa sifa ya ku-top up basi anaweza kwenda benki nyingine kwa sababu salary slip yake haitaonesha deni la 4,232,000.