NAOMBENI MSAADA WA KISHERIA KUHUSU JAMBO HILI LA URITHI

NAOMBENI MSAADA WA KISHERIA KUHUSU JAMBO HILI LA URITHI

UMUNYU

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2017
Posts
726
Reaction score
564
Hapa nilipo baba yangu mkubwa alifariki miaka zaidi ya ishirini iliyopita akamuacha mama mkubwa na watoto wake saba.Pia katika kipindi hicho baba mkubwa alizaa watoto wawili kwa mama tofauti,akawachukua na kuwaleta kwa mama mkubwa ndiye aliyewalea wote!Hivi sasa watoto hao ni mama wazima na wana familia zao.Sasa kilichotokea wamekuja wanataka urithi wao.Wanadai nyumba iuzwe ili wapate haki yao!Ila huyo mama mkubwa ambaye aliwalea bado yuko hai na anaishi hapo!Naombeni ushauri nini kifanyike kwa mujibu wa sheria?Pia,pamoja na mume wake kufa,inamaana huyo mama hana haki yoyote kwenye hizo Mali hasa ikichukuliwa kuwa aliishi na mumewe toka 1970 hadi umauti unamkuta 1993?.Naombeni ushauri wadau maana mama mkubwa ana mawazo sana hasa ikichukuliwa kuwa hata umri wake umesonga.
 
Hakuna watakacho kipata hapo, labda kwanza mke wa marehemu afariki.
Waambie waende mahakamani, na wapigeni marufuku kukanyaga hapo na mkawafungulie kesi kama wanakuja kufanya fujo. Kama undugu unakufa pia ni sawa, maana tayari hao nduguzenu wamesha ingiwa na tamaa ama wameshauriwa vibaya.
 
Ni kweli baba yao alishafariki na Wana haki ya kurithi.Siyo lazima nyumba iuzwe ndo wapate urithi,itafutwe stahiki yao katika mgao wa baba yao familia ijichange wapewe haki yao.Ni vizuri hili jambo likapita mahakamani ili haki itendeke.Wanachofanya ni haki yao isipokuwa haitakiwi kulazimisha nyumba kuuzwa.
 
Hakuna watakacho kipata hapo, labda kwanza mke wa marehemu afariki.
Waambie waende mahakamani, na wapigeni marufuku kukanyaga hapo na mkawafungulie kesi kama wanakuja kufanya fujo. Kama undugu unakufa pia ni sawa, maana tayari hao nduguzenu wamesha ingiwa na tamaa ama wameshauriwa vibaya.
Nashukuru kwa ushauri!Tatizo wamekuwa kero kwa mama mkubwa!Wanamdai hadi vyumba walivyokuwa wanalala enzi hizo kabla hawajaolewa!Eti wamuuzie yeye!
 
Urithi ni mali ya mke halali wa marehemu na sio mwingine. Wakumbushe tu watunze ndoa zao sababu pia wao sio watoto halali isipokuwa marehemu Ali acha wosia wa kuwatambua. Otherwise wao ni walelewa tuu
 
Nashukuru kwa ushauri!Tatizo wamekuwa kero kwa mama mkubwa!Wanamdai hadi vyumba walivyokuwa wanalala enzi hizo kabla hawajaolewa!Eti wamuuzie yeye!
Mnawachekea tu hao....
Hakuna mtoto anaeweza kuchukua urithi wa marehemu babayake ikiwa mke wa marehemu akingali hai na hizo mali alizichuma na mumewake.
Hao kawafungulieni kesi polisi kwa kosa la kufanya fujo hapo nyumbani kwa mama mkubwa.
Kama wao wanalao jambo, basi waende wakafungue shauri mahakamani ili wadai urithi.
 
Mnawachekea tu hao....
Hakuna mtoto anaeweza kuchukua urithi wa marehemu babayake ikiwa mke wa marehemu akingali hai na hizo mali alizichuma na mumewake.
Hao kawafungulieni kesi polisi kwa kosa la kufanya fujo hapo nyumbani kwa mama mkubwa.
Kama wao wanalao jambo, basi waende wakafungue shauri mahakamani ili wadai urithi.
Nashukuru kwa ushauri
 
Back
Top Bottom