Naombeni ushauri kuhusu huyu mwizi aliyepigwa Mtaani kwetu

Naombeni ushauri kuhusu huyu mwizi aliyepigwa Mtaani kwetu

Unaonekana ulishiriki kumpiga mshukiwa wa wizi tegemea kushitakiwa kwa makosa yafuatayo:-

1. Kupiga na kudhuru
2. Kujichukulia Sheria mkononi

Halafu mliyempiga atakudai fidia😬
 
Huku mtaani kuna mwizi alichezea kichapo usiku baada ya kutuhumiwa ni mwizi na kama mnavyojua hili neno ukiitiwa usiku wa saa 7 hata kama sio mwizi raia wanapiga.

Sasa inasemekana kapona hajafa na polisi wanataka kumpitisha awatambue waliompiga na Mimi nilikua nimeenda kumshuhudia akichezea kipondo nawaza asijepata wenge akanijumuisha na Mimi kwamba nilimtembezea mkong'oto.

Nauliza hapa kama nikakamatwa na mimi natokaje kwenye huu msala wakuu sababu hapa JF ni kisima cha maarifa.
Kwa wewe wakufunge tu,maana unajaza Server za Jf kwa upuuzi wa kila muda.
 
Haya masuala ya kusikia mwizi unajitokeza na kuanza kupiga pasipo kujua chanzo ni aina nyingine ya ukichaa, ilishatokea jamaa na mpenzi wake walipigombana yule jamaa akataka kuchukua vyake ikiwemo simu aliyomnunulia, yule mwanamke akaanza kuita mwizi, jamaa aliuawa kimasikhara....

Hata unapoona ajali imetokea kama unajua ukifika eneo la tukio hakuna msaada utatoa basi ni bora usifike kushangaa....
 
Haya masuala ya kusikia mwizi unajitokeza na kuanza kupiga pasipo kujua chanzo ni aina nyingine ya ukichaa, ilishatokea jamaa na mpenzi wake walipigombana yule jamaa akataka kuchukua vyake ikiwemo simu aliyomnunulia, yule mwanamke akaanza kuita mwizi, jamaa aliuawa kimasikhara....

Hata unapoona ajali imetokea kama unajua ukifika eneo la tukio hakuna msaada utatoa basi ni bora usifike kushangaa....
Sawa mkuu
 
Atakaa wiki
kesi nyepesi hio unashinda hata kama ulimtembezea kipigo
.
hapo hakuna ushahidi hata wakikamata we kataa katu katu utakaa/ kulala sero asubuh wanakuachia
Sijashiriki mkuu
Nikutonye tu, kesi zinazoonekana nyepesi Kuna muda hugeuka kuwa ngumu na ukaishia kusota jela.

We endelea kuchati jamiiforums ubebwe halafu ukijifanya jeuri PP atakupeleka mahakamani.

Huko ukienda kukiri tu Eti ulikuwepo wakati raia wakimpiga ila wewe hukumpiga unakula mvua kwa makosa Yale Yale ya waliompiga.

Jiongeze fallah wewe 😬😬😬
 
Back
Top Bottom