Naombeni ushauri nataka kuuza mali zangu polepole nifurahie maisha urithi kwa watoto ni elimu niliyowasomesha mnasemaje?

Sir John Roberts

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2017
Posts
12,835
Reaction score
23,584
Sina mali nyingi ila nashukuru Nina nyumba kadha wa kadha, viwanja , mashamba na mifugo kijijini kwetu.
Watoto wangu wanasoma na watamaliza bila shaka. Nimetafakari haya maisha hayana garantii naweza kufa saa yeyote je kwanini nisianze kula mali zangu taratibu kabla sijafa? Naombeni ushauri.
 
Wewe uza mali zako zote kabisa ili ufurahie maisha. Kimfaacho mtu chake!
 
weka bei na ni mkoa gani tununue, maisha ni haya haya
 
Na hii ndio sababu kubwa kwanini ngozi nyeupe inatuzidi mbali, sisi ni wabinafsi sana tunataka tunapopotea kwenye uso wa dunia basi tupotee na kila kitu chetu tulichofanikiwa kuwa nacho.

Hii ni roho ya kuendeleza umasikini kizazi hadi kizazi, kuna hasara gani wanao, wajukuu, wakinufaika na matunda aliyopanda baba/babu yao?
 
Viwanja vipo wapi mkuu tununue?
 
UZA TU KWANI SISI INATUHUSU MKUU
 
Hata ukiviacha wanatoana roho kwa kuvigombania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…