Naombeni ushauri wa busara, amemfukuza mke wake kwa sababu yangu

Naombeni ushauri wa busara, amemfukuza mke wake kwa sababu yangu

Recycle bin imekutendea mbaya mkuu, pole sana kwa mkasa huo.
 
aliambiwa kaua na hajaua akafungwa alivotoka akamuona yule jamaa alofungwa kwajil yake,,akamuua kwel mbele ya watu wazito😆😆kama sijakosea
Kweli kabisa..yaani alitumikia adhabu kabla ya kosa..alivyotoka akatenda lile kosa alilofungwa nalo kesi ikaisha.
 
Kweli kabisa..yaani alitumikia adhabu kabla ya kosa..alivyotoka akatenda lile kosa alilofungwa nalo kesi ikaisha.
aloooh umemshauri kitaalamu sana,,asipoelewa basi tena
 
  • Thanks
Reactions: BRN
Nyie kama sio walimu basi mnisamehe..maana walimu ndio wana mambo ya kijingajinga hivi..
Anyway we mchape mashine tu huyo mke wa jamaa ili kuhalalisha hizo tuhuma zake.
 
Sio wote walioko magerezani wana makosa.
Nakushauri uingie ndani kwako uombe serious kabisa kwa Imani yako mwisho hili jaribu litapita kushoto lenyewe.... Kumbuka shetani sio mpaka umuone sura
 
Kuna kitu unaficha kwenye hiyo convo, weka wazi haiwezekani kwa hizo sms 4 tu iwe hivyo mkuu na kama ni hivyo basi huyo jamaa yako ni kisusio, anajua kususa sana.

Katika kitu huwa sitaki ni mazoea na mashemeji zangu, huwa siruhusu ukaribu wa aina yeyote ule. Na huwa nawaambia kabisa jamaa zangu tusitiane majaribuni.
Za asubuhi shemeji
 
Sasa hv tumelewa.. huo ushauri wa busara hadi kesho baada ya supu.
But on a serious note, lazma uliendelea kum entertain huyo shemeji yako maana ungeweka mipaka tangu mwanzo yasingetokea haya
Ni kawaida ya waomba ushauri wengi huwa hawaongelei upande wao mbaya, mabaya yote huyasukumiza kwa wengine
Si ajabu hata hizo sms kaziedit .
 
Ni kawaida ya waomba ushauri wengi huwa hawaongelei upande wao mbaya, mabaya yote huyasukumiza kwa wengine
Si ajabu hata hizo sms kaziedit .
MKUU hii ni kweli kabisa hawa watoa ushauri, hata ukikuta kwenye ndoa mume kamtendea vibaya mke wake hasa maswala ya kucheat au kuzaa nje ,
Mke akilalamika utakuta wanamtupia lawama mke wake.

Wengi wao wanasema mume kakuoa kwa sababu wewe ndo mke na wengine sio, ila wanasahau kuwa mume ni malaya, hasa wenye huu ushauri ni watoa ushauri wa kiume.
 
Utakuwa umemla tu, haiwezekani mwanaume akurupuke hivyo.

Kama unajiamini hujamla issue iende kwenye uongozi hapo job kwenu.

Kufanya kazi ofisi moja wana ndoa matokeo ndo hayo.
 
Muachage mazoea na ndoa za watu. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wakuu kwema,

kama mada inavyojieleza, hapa nipo njia panda nakosa la kufanya,naamin ntapata maoni kupitia nyinyi.

Labda niwaeleze kisa na mkasa mpaka kufikia hatua ya kupandisha uzi usiku huu.

Nina rafiki ambaye tulitokea kuwa marafiki na kilichotukutanisha ni kazi tuliyokuwa tukifanya sehemu moja (kampuni moja), nadhan ni moja ya marafiki ambao tuliaminiana kwa mengi sana na tumekuwa tukishirikiana katika mambo kadha wa kadha (nampa big up sana hana roho mbaya) kiumri ananizidi mbali,yeye ana mke na mtoto.

Kadiri siku zilivyozidi kwenda alinitambulisha kwa mkewake so tukawa kama ndugu sasa huku mm nikimwita mkewake shemeji.

Wakati tukiendelea na kazi jamaa ilibidi amfanyie mchongo mkewake naye akapata kazi hapo hapo tukaendelea kusukuma gurudumu. tatzo lilianza mkewake alitengeneza mazoea ya ghafla na mm ,ule u-shem shem na kumisiwa kukawa kwingi, japokuw nilijitahid kumkwepa lkn alikaza mwishowe jamaa nafikir aliusoma mchezo mzima

Upesi upesi jamaa kapunguza ule ukaribu yaan yale mazoea hataki tena, sikutaka hata kuuliza mimi pia nikala kmya, sasa kwa upande wake akahisi ni kweli namchapia mkewe.

Sasa juzi mwamba hakufika kazini wala kakutoa taarifa yoyote, alikuja mkewake tu na wafanya kaz wengne kwa mbali nikawasikia waliokuw pembeni wakidai jamaa anaumwa,

Kumbuka wakati huo mi sina mazoea na shemej zaidi ya yeye kunichangamkia tu.

Muda wa kurudi home naona text

No ngeni "mamb"
Mimi safi habari
No ngen. nzur 2

Nikaipotezea, dakika chache simu inaita namba ileile akajitambulisha na akanipa habari za mumewe kuugua bas nikawapa pole yao na maongezi yakaishia hapo

Nafika nyumbani text tena inaingia

No ngeni (ile ile)
"ila shem huwa nakumic sana ni bas tu usinifikirie vibaya jamani"
Mimi."shem tulia na mme wako" yeye."hata kama ila mi nakupenda tambua hilo'

Sikujibu tena kwanza nilihisi wapo wote wananiigizia kwanza namba kaipata wap.

Ndugu zangu ile meseji kwanza ilitisha nikahisi ni mtego so nikaichunia nikaendelea na masuala mengne hata yy kakunichek tena

Sasa jana nimekaa zangu home naona mwamba huyu hapa na mkewake,aisee hata kabla sijawakaribisha mwamba kaniporomoshea matusi ya nguoni huku mwanamke analia.

Cha kushangaza zaidi akanambia "kwa kuwa mnapendana nimeamua kukuletea kabsa furahini sasa" kisha jamaa huyo akaondoka speed kwa mbaaali namsikia akimshukuru kwa kumzalia tu mtoto.

Huyu shemej akanipa mkasa sasa aisee kwanza nilihuzunika kumbe zile sms alifuta zikabak kwenye recycle bin (wazee wa Samsung) alijisahau na mme wake akazifuma kule kule

Sasa wazee nipo njia panda mwanamke kakimbilia kwa rafik yake ,kule jamaa nae sijui ananifikiria nn na mm natafuta njia ya kumuaminisha kuwa sikuwa wala sina mahusiano na mkewake,

Naombeni ushauri juu ya hili
Pumbavu
 
Utakuwa umemla tu, haiwezekani mwanaume akurupuke hivyo.

Kama unajiamini hujamla issue iende kwenye uongozi hapo job kwenu.

Kufanya kazi ofisi moja wana ndoa matokeo ndo hayo.
 
Back
Top Bottom