Naombeni ushauri wenu nifanyeje niweze kurudisha umbo langu la zamani

Naombeni ushauri wenu nifanyeje niweze kurudisha umbo langu la zamani

thelostnuts

Member
Joined
Jan 16, 2015
Posts
67
Reaction score
19
Wanajukwaa kama mada inavyojieleza hapo juu mimi ni mama wa makamo( miaka 35) nimejishangaa ghafla nimebadilika umbo langu bila kutegemea nilikuwa na umbo zuri kwa kweli sikuwa na tumbo kabisa pamoja na kwamba Nina Watoto wawili, mikono yangu ilikuwa midogo kuendana na mwili wangu huku ikiwa nyama zimekaza sasa tumbo limekuja na mikono imejaa,mbaya zaidi nyama za mikono na tumbo zimelegea.!

Siwafichi kwa hili linanikosesha confidence mbele ya watu, mume wangu naye amekuwa akiniambia kuwa siku hizi sipendezi kama ilivyokuwa zamani Kwa kweli inaniumiza.

Sijabadilisha mfumo wa maisha yangu ni ule ule wa siku zote, sijawahi kufanya mazoezi wala kufanya diet, sasa ninajiuliza ni kitu gani kimenibadilisha ghafla hivi.

Naombeni ushauri wenu ni nini nifanye niweze kurudisha umbo langu,na pia niweze kuwa na confidence kama zamani maana hata nguo naona hazinipendezi tena na pia nahisi nitakimbiwa na mume maana hana amani na hili liumbo utafikiri kalibeba yeye.
 
Mara nyingi hutokea kwa wazazi kwa hiyo si hali ya ajabu au mpya kwa kuwa mfumo wako wa maisha ni ule ule jaribu kubadili mfumo wa kula fanya diet kidogo na mazoezi kidogo kupunguza unene huo.
1. Je umeongezeka na kilo?
2. Vipi kuhusu sehemu nyingine za mwili?
3. Uzazi wa pili una muda gani baada ya kujifungua?
4. Unafanya shughuli zinazoshughulisha mwili wako?
5. Nini upendelea kula?

Nakushauri jitahidi kucontrol hiyo hali usije kukaribishiwa vimodo
 
Mara nyingi hutokea kwa wazazi kwa hiyo si hali ya ajabu au mpya...
Kwa kuwa mfumo wako wa maisha ni ule ule jaribu kubadili mfumo wa kula... Fanya diet kidogo na mazoezi kidogo kupunguza unene huo...
1. Je umeongezeka na kilo?
2. Vipi kuhusu sehemu nyingine za mwili?
3. Uzazi wa pili una muda gani baada ya kujifungua?
4. Unafanya shughuli zinazoshughulisha mwili wako?
5. Nini upendelea kula?

Nakushauri jitahidi kucontrol hiyo hali usije kukaribishiwa vimodo
Nashukuru kwa ushauri nitajaribu nione kama utanisaidia,
Uzito nimeongezeka kama kilo NNE HV,
Uzazi wa mtoto wa pili ni miaka kumi sasa, na kazi zangu ni za ofisini tu, kwa chakula kwa kweli niwe mkweli huwa nakula chochote kinachopatikana kwa muda huo
 
Nashukuru kwa ushauri nitajaribu nione kama utanisaidia,
Uzito nimeongezeka kama kilo NNE HV uzazi wa mtoto wa pili ni miaka kumi sasa, na kazi zangu ni za ofisini tu, kwa chakula kwa kweli niwe mkweli huwa nakula chochote kinachopatikana kwa muda huo
Uzazi wa mwisho miaka 10 ina maana unaelekea miaka 40 au karibia na hapo kwa umri huo mwili unakaribia menopause ndio kawaida lazima unenepeane kama hau control style ya maisha yako yani ni sawa na ng'ombe aliyehasiwa lazima anenepe tu.
 
Uzazi wa mwisho miaka 10 ina maana unaelekea miaka 40 au karibia na hapo... Kwa umri huo mwili unakaribia menopause ndio kawaida lazima unenepeane kama hau control style ya maisha yako...
Yani ni sawa na ng'ombe aliyehasiwa lazima anenepe tu.
Kwa sasa nina miaka 35 kwan mtoto wa pili nilimpata nikiwa na miaka 25,hata hivyo hili la kukaribia menopause inawezakuwa ndo jibu na hivi sikuwa najicontrol kwenye kula ndo inawezekana imesababisha yote haya nizidi kukushukuru ndg
 
Nitaanza sasa kufanya mazoezi, ni yapi yanayofaa zaidi
Kupunguza mwili kwa kufanya mazoezi inahitaji commitment ya hali ya juu na displine (sikukatishi tamaa ila ndio ukweli). Kama ni mfanyakazi nakushauri fanya diet nyepesi hizi sio za kujiumiza ma pia upate dakika 30-60 za kutembea na kufanya mazoezi ya mwili walau mara 4 kwa week.

Hebu pitia huu uzi hapa unaweza kukusaidia kupata vyakula vya kupunguza mafuta tumboni...
Pia nakushauri usifanye diet kali au kuwa na haraka sana ili mwili uzoee, kuepuka kupata vidonda vya tumbo na pressure mbalimbali pia udhaifu wa mwili...

1. Jinsi ya kuondoa au kupunguza mafuta tumboni kwa wanawake (Vitambi vya kike)

2. Njia 12 za mazoezi ya kupunguza tumbo kwa wanawake

ASANTE NA KARIBU...
 
Umri umeenda tuliza boli life span 50 una 35 unataka nini tena...
 
Back
Top Bottom