Naombeni ushauri wenu nifanyeje niweze kurudisha umbo langu la zamani

Naombeni ushauri wenu nifanyeje niweze kurudisha umbo langu la zamani

Kupunguza mwili kwa kufanya mazoezi inahitaji commitment ya hali ya juu na displine (sikukatishi tamaa ila ndio ukweli). Kama ni mfanyakazi nakushauri fanya diet nyepesi hizi sio za kujiumiza ma pia upate dakika 30-60 za kutembea na kufanya mazoezi ya mwili walau mara 4 kwa week.

Hebu pitia huu uzi hapa unaweza kukusaidia kupata vyakula vya kupunguza mafuta tumboni...
Pia nakushauri usifanye diet kali au kuwa na haraka sana ili mwili uzoee, kuepuka kupata vidonda vya tumbo na pressure mbalimbali pia udhaifu wa mwili...

1. Jinsi ya kuondoa au kupunguza mafuta tumboni kwa wanawake (Vitambi vya kike)

2. Njia 12 za mazoezi ya kupunguza tumbo kwa wanawake

ASANTE NA KARIBU...
Nashukuru kwa Uzi huu Nina imani utanisaidia sana
 
Au fanya hivi nunua extravirgin olive oil+coconutoil+mustardoil+lemon essential oil changanya kwa pamoja uwe na tabia ya kujikanda na hayo mafuta eneo husika
 
Best kama mimi
Yaani nimeshangaa nimefumuka ghafla
Mwili umekuja bila sababu ya msingi.

Mie nimeanza mazoezi na diet kwa mbaaali
Nimeshapunguza kg 3
Bado nakazana
Umenipa moyo kumbe inawezekana kabisa, nitaanza diet, mazoezi, na kula vyakula pendekezwa nadhan nami nitafanikiwa, shukrani
 
Umenipa moyo kumbe inawezekana kabisa, nitaanza diet, mazoezi, na kula vyakula pendekezwa nadhan nami nitafanikiwa, shukrani
Kila la kheri
Pia inaweza kuwa ndani ya akili zaidi
Amini utapungua
Ijenge picha ya unavyohitaji kuwa
Usikatishwe tamaa na neno la mtu.
 
Sidhani Kama ulifunga tumbo ulipojifungua, maana usipofunga mara nyingi madhara yake ni hayo,
 
Pakua hii App "30days workout "....itakusaidia
Panama option ya mazoez ya tumbo name mikono... Although zipo name nyingine ila chagua unayotaka kufanyia kaz
 
Si jambo la ajabu, ni dalili kuwa umri umeanza kukutupa mkono, lazima uyakubali mabadiliko, nadhani unayakumbuka matiti yako wakati unavovunja ungo jinsi yalivyokuwa yamesimama vyema na imara kama kifuu cha nazi, bila ya shaka hali hiyo haipo tena. Kwa ufupi hayo Ndio mabadiliko yanyoendana na umri, muda si mrefu utaona mabadiliko ktk maeneo yanayozunguka macho yako, usishangae bali yapokee tu.

Pendelea kula vyakula vinavyojenga mwili mara kwa mara ( matunda na mboga mboga) vitakusaidia kuimarisha ngozi yako isilegee sana. Pia fanya mazoezi ya kutembea kwa miguu angalau nusu saa kwa siku. Ukitembea 1hr itapendeza. Pia posheni yako ya chakula kila unapokula hakikisha inakuacha ukiwa bado unatamani kula ( iache tumbo wazi japo kidogo).

Jioni unapolala usile hadi kushiba. Unaweza kunywa maji na sambusa moja au mbili.
 
Back
Top Bottom