Naombeni ushauri

Naombeni ushauri

F
Mimi niliolewa mwaka 2017,nilikaa na mume wangu kwa upendo na amani, ila mimi nilimtangulia mwanaume nilikuwa na mtoto mmoja ambae nilizaa na mwanaume mwingine kabla ya kuolewa na mume wangu yeye alikuwa hajawahi kuoa wala kuzaa, kwahiyo katika muda wote huo wakati nipo kwenye ndoa nilikuwa natafuta mtoto,nilikunywa dawa za hospital na mitishamba bila kuchoka ila mume wangu yeye hakuwahi kusema kwamba twende wote tukapime hata siku moja ikiwa hata hospital nilipokuwa naenda nilikuwa naambiwa natakiwa kwenda na mwenza wangu

Lakini hata nilipokuwa namwambia hakuwahi kujali kuhusu swala la kwenda wote kupima ila alikuwa ananipa pesa yoyote inayoitajika hospital nauli na hata ya kula nikiwa huko,ilipofika 2020 siku moja usiku nikakuta meseji ya namba ambayo haijaseviwa kwamba anaambiwa atume pesa mtoto anaumwa,ule usiku niligombana nae sana hadi akaamua kusema huyo mtu anamuomba hela tu amsaidie ila sio mtoto wake

Basi mimi nilichukua namba kimyakimya na kumtafuta huyo mtu nikamuuliza kwanini anamwambia mume wangu ampe msaada juu ya mtoto wake huyo dada alicheka kwanza halafu akaniambia nakusikitia sana muulize vizuri mwanaume wako basi mimi nilianza kutafuta baadhi ya watu ninaowajua sababu ya kuwatafuta hao watu ni kwa sababu alipokuwa anaishi mwanaume nilishawahi kukaa zamani wakati nasoma kwahiyo kuna watu baadhi nilisoma nao na wengine ni marafiki ambao niliwapata tu na hata huyo mwanamke alikuwa anaishi maeneo hayo lakini nilipowapigia watu hakuna aliyeniambia chochote kwamba labda huyo binti mtoto ni wa mume wangu au vipi

Basi lakini huyo msichana alishaolewaga kabla mimi kufunga ndoa na huyu mume wangu huko alizaa mtoto mmoja wa kiume, baada ya kuona kwa mwanaume sipati majibu yoyote niliamua kumshirikisha dada yake mkubwa ambae alikuwa ni mtu wangu wa karibu sana na lakini dada yake alisema hajui chochote ila nikamuomba kumuuliza kaka yake kama huyo mtoto ni wake akasema sawa nitaongea nae kaka mimi mume wangu ni wale wanaume wapole sana na hawatumii kilevi chochote sio sigara wala pombe ila huwa anapenda sana mpira

Kwahiyo sikupata majibu kokote kwa dada yake wala kwake kuhusu huyo mtoto mimi nikasema leo nitamtisha nikamwambia nataka niende kwa mjomba wako nikamwambie kuhusu hili na utakuja kumjibu yeye kama mtoto wako au sio wako akasema usiende nisubiri nikirudi tutakuja kuongea kuhusu swala la mtoto mimi na wewe usiku aliporudi alisema anataka ale kwanza ndo azungumze haya nilimwekea chakula baada ya pale tulizungumza na akakubali kwamba mtoto ni wake ila anaomba nimsamehe

Aiseeee usku huo sitakuja kuusahau kwenye maisha yangu 😭😭😭😭nililia usiku kucha na nilifikiria vingi kumbe mimi nakunywa dawa mwenzangu alikuwa ana mtoto huko ndo maana halikuwa ajali swala la kwenda hospital sasa hapo mimi ndoa 2017 mwanamke wa nje ana mimba 2018 nimekuja kujua 2020 nimezungukwa muda wote huu na familia nzima🙌🏻🙌🏻baada ya pale asubuhi nilimchek wifi yangu kumwambia kaka yake amesema mtoto wake nikijua wifi yangu nae hajui jaman inauma sana akaniambia kakubali nikamjibu ndio ila mume wangu alionyesha kukiri kama amekosea baadhi ya wakubwa walinipa ushauri wakasema pambana hivi vitu vipo kila sehemu sio wewe wa kwanza

Basi kaka nilikuwa ni mtu wa kulia ndan ila siwaonyeshi watu huu mwaka mimi baada ya kujua na ndo birthday ya huyo mtoto ilikuwa karibu ilipofika siku ya birthday huyo dada alipost picha ya mtoto na ujumbe wa vijembe sana kukaa kidogo wifi yangu nae akamuweka yule mtoto status tena kwa maneno makali aiseee sikuelewa ilikuwa kitu gani nikamchek wifi yangu nikamwambia kumbe ulikuwa unajua kila kitu ulikuwa unanizunguka jaman jaman

Hapo ndo alitoa la moyoni siku hiyo akasema ulitaka kaka yangu afe ugumba hiyo siku alitema sumu nyingi wifi yangu nadhani mnaoishi na familia ukiwa na changamoto hiyo mnaelewa hiyo siku niligombana sana na mwanaume na kumlalamikia kwamba kwanini dada zake wananifanyia vile basi kesho yake nilianza upelelezi wangu binafsi kutaka kujua kwanini mwanamke alitoka kwenye ndoa yake nikaja kujua yule mwanamke aliomba talaka kwa mwanaume yeye mwenyewe akimwambia mume wake mimba sio yake lakini hapo alidai talaka mimba ikiwa na miezi minne ikiwa miezi mitatu ya mimba aliishi na huyo mwanaume

Kwahiyo mumewe alikataa kumpa talaka kwa sababu ni mjamzito lakini yeye alienda hadi serikali za mtaa ili apewe talaka kwahiyo watu wazima waliamua apewe talaka hata kama ana mimba maana anaonekana mtu amedhamiria kutaka talaka kwahiyo alipewa talaka akarudi kwao wakati huo alikuwa ana mtoto wake wa kwanza na mimba ya miezi minne kwahiyo mume wake alikuwa anaenda nyumbani kwao kumuona na kupeleka matumizi ya mimba na ya mtoto na huku mume wangu nae alikuwa anaenda kupeleka matumizi ya mimba baada ya kujifungua ndo alimwambia mume wake mtoto sio wake ila siku ya 40 ya mtoto wifi zake upande wa mume wake walienda na zawadi wakapeleka baada ya kujua hayo nikaona au mume wangu amebambikiwa na yeye mwenyewe hajui?

Hebu niwe namuuliza baadhi ya vitu lakini alikuwa hanijibu kuna siku nikamuona mume wa yule dada kapost picha ya mtoto ambae mume wangu anamhudumia nikamuonyesha mume wangu nikamwambia usimtafute hebu tuone mwisho wa hili lakini mwenzangu kumbe hakuweza kuvumilia akamtafuta huyo mwanamke na kumwambia mwanamke muda huo huo akamtafuta huyo mume wake wa zamani na kumwambia afute hiyo picha ya mtoto aliyoiweka mtandaon aiseeee!!!!

Basi mimi kuna siku nikamtafuta huyo mwanamke kwa simu nikawa namwambia usije ukawa unatupa mtoto ambae sio wa mume wangu yule dada alinitukana na kusema mimi sitokuja kuzaa kwa huyu mwanaume kwa sababu nina laana ya mama mkwe kwamba mama yake mwanaume wakati anakufa alimwambia mwanae asinioe basi ikawa mimi kujua kwangu kama nimewapa uhuru wifi zangu pia kutoa sumu wakawa wanapostiana fb kwa mahaba sana hadi mimi baadhi ya rafiki zangu ambao sikai nao karibu walijua changamoto ya ndoa yangu kupitia fb sababu wana urafiki na wifi zangu tangu hapo nikawa siongei na wifi zangu tena

Kuna siku shangazi wa mwanaume akaniita ni mke wa mjomba wake yaani kaka yake mama yao mkewe akaniambia nisikate tamaa maana nilishaacha kuywa na dawa kuanzia hapo akasema tujaribu mara ya mwisho akaniambia mimi nitakusaidia hata hela basi kuna siku nikapita sehem nikaona duka la madawa nikaingia nikamuelezea huyo muuzaji changamoto zangu akanipa ushauri huyo mwenye duka la dawa ni nurse kwenye hospital ya AMANA nikamtafuta shangazi kumwambia gharama nilizoambiwa ilikuwa ni elfu stini(60) dose yote basi akanitumia elfu 25 nikanunua dawa nikaanza kutumia

Baada ya pale nikamshirikisha na mwanaume hela iliyobaki akawa ananipa kidogo kidogo ila pia wakati ule nilikuwa namshirikisha Mungu sana matatizo yangu changamoto yangu kubwa ilikuwa sipati period lakini zile dawa zilikuwa za siku(30) nilipofika siku ya (27) nikaanza kuingia period na nilipomaliza dose huku nikiwa kwenye perido nikarudi kwa yule Dokta akaniambia hapo nisitumie dawa yoyote nirelax na mume atoe ushirikiano

Basi mimi kufika mwezi wa tisa(9) 2022 nikawa ni mjamzito wa mwezi mmoja kwa kweli nilishukuru ila hata kipindi nina mimba mwanamke alikuwa ananitukana ananitumia picha akiwa ametoka na mume wangu kwakweli mambo yalikuwa magumu sana hadi nikajifungua mwaka jana mwezi wa nne(4) tena nilipata operation

Yule mwanamke alipata taarifa akaanza kunitafuta na kunikashifu kwa kupata kisu na kuniambia ninywe urojo basi kuna siku akapost picha yake na kusema mwakani zamu yangu 🫄muda huo mimi mwanangu mdogo aiseee mwaka Huu mwezi wa pili Yule mwanamke nikasikia ni mjamzito na hivi anakaribia kujifugua jamani mwanaume ameshindwa kuachana nae mambo hayo wapo tangu 2017 mimi naolewa hadi Leo na sio mwanamke mstaarabu huwa ananitukana sana Kama anataka mimi niondoke yeye abaki na mwanaume

Hebu nisaidieni kiushauri nimwachie tu mwanaume mimi nikaanze upya maisha yangu au nifanyeje maana ndoa imekuwa doa mawifi zangu hawana mapenzi na mtoto wangu wao wapo na huyo mwanamke wa kaka Yao na huyu mwanaume ndo mnafki nifanyeje Mimi?
Futa namba za huyo mwanamke, usimuambie chochote mme wako kuhus huyo.mwanamke wake, akikupigia uyo mwanamk usimpokeelee wala usimjib msg, wewe fanya majukum yako kwa mme wako, mpend muonesh upendo, fanya kama hujui kitu japokua unajua na wala usiyafatilie tena, kuhus mawif zako achana nao, wakikusalimia waitikie vzr t ila hayo mamb yao hata ukiona status zao ww kaa kimya usiseme kitu, muache Mungu aamue.
 
Mimi niliolewa mwaka 2017,nilikaa na mume wangu kwa upendo na amani, ila mimi nilimtangulia mwanaume nilikuwa na mtoto mmoja ambae nilizaa na mwanaume mwingine kabla ya kuolewa na mume wangu yeye alikuwa hajawahi kuoa wala kuzaa, kwahiyo katika muda wote huo wakati nipo kwenye ndoa nilikuwa natafuta mtoto,nilikunywa dawa za hospital na mitishamba bila kuchoka ila mume wangu yeye hakuwahi kusema kwamba twende wote tukapime hata siku moja ikiwa hata hospital nilipokuwa naenda nilikuwa naambiwa natakiwa kwenda na mwenza wangu

Lakini hata nilipokuwa namwambia hakuwahi kujali kuhusu swala la kwenda wote kupima ila alikuwa ananipa pesa yoyote inayoitajika hospital nauli na hata ya kula nikiwa huko,ilipofika 2020 siku moja usiku nikakuta meseji ya namba ambayo haijaseviwa kwamba anaambiwa atume pesa mtoto anaumwa,ule usiku niligombana nae sana hadi akaamua kusema huyo mtu anamuomba hela tu amsaidie ila sio mtoto wake

Basi mimi nilichukua namba kimyakimya na kumtafuta huyo mtu nikamuuliza kwanini anamwambia mume wangu ampe msaada juu ya mtoto wake huyo dada alicheka kwanza halafu akaniambia nakusikitia sana muulize vizuri mwanaume wako basi mimi nilianza kutafuta baadhi ya watu ninaowajua sababu ya kuwatafuta hao watu ni kwa sababu alipokuwa anaishi mwanaume nilishawahi kukaa zamani wakati nasoma kwahiyo kuna watu baadhi nilisoma nao na wengine ni marafiki ambao niliwapata tu na hata huyo mwanamke alikuwa anaishi maeneo hayo lakini nilipowapigia watu hakuna aliyeniambia chochote kwamba labda huyo binti mtoto ni wa mume wangu au vipi

Basi lakini huyo msichana alishaolewaga kabla mimi kufunga ndoa na huyu mume wangu huko alizaa mtoto mmoja wa kiume, baada ya kuona kwa mwanaume sipati majibu yoyote niliamua kumshirikisha dada yake mkubwa ambae alikuwa ni mtu wangu wa karibu sana na lakini dada yake alisema hajui chochote ila nikamuomba kumuuliza kaka yake kama huyo mtoto ni wake akasema sawa nitaongea nae kaka mimi mume wangu ni wale wanaume wapole sana na hawatumii kilevi chochote sio sigara wala pombe ila huwa anapenda sana mpira

Kwahiyo sikupata majibu kokote kwa dada yake wala kwake kuhusu huyo mtoto mimi nikasema leo nitamtisha nikamwambia nataka niende kwa mjomba wako nikamwambie kuhusu hili na utakuja kumjibu yeye kama mtoto wako au sio wako akasema usiende nisubiri nikirudi tutakuja kuongea kuhusu swala la mtoto mimi na wewe usiku aliporudi alisema anataka ale kwanza ndo azungumze haya nilimwekea chakula baada ya pale tulizungumza na akakubali kwamba mtoto ni wake ila anaomba nimsamehe

Aiseeee usku huo sitakuja kuusahau kwenye maisha yangu 😭😭😭😭nililia usiku kucha na nilifikiria vingi kumbe mimi nakunywa dawa mwenzangu alikuwa ana mtoto huko ndo maana halikuwa ajali swala la kwenda hospital sasa hapo mimi ndoa 2017 mwanamke wa nje ana mimba 2018 nimekuja kujua 2020 nimezungukwa muda wote huu na familia nzima🙌🏻🙌🏻baada ya pale asubuhi nilimchek wifi yangu kumwambia kaka yake amesema mtoto wake nikijua wifi yangu nae hajui jaman inauma sana akaniambia kakubali nikamjibu ndio ila mume wangu alionyesha kukiri kama amekosea baadhi ya wakubwa walinipa ushauri wakasema pambana hivi vitu vipo kila sehemu sio wewe wa kwanza

Basi kaka nilikuwa ni mtu wa kulia ndan ila siwaonyeshi watu huu mwaka mimi baada ya kujua na ndo birthday ya huyo mtoto ilikuwa karibu ilipofika siku ya birthday huyo dada alipost picha ya mtoto na ujumbe wa vijembe sana kukaa kidogo wifi yangu nae akamuweka yule mtoto status tena kwa maneno makali aiseee sikuelewa ilikuwa kitu gani nikamchek wifi yangu nikamwambia kumbe ulikuwa unajua kila kitu ulikuwa unanizunguka jaman jaman

Hapo ndo alitoa la moyoni siku hiyo akasema ulitaka kaka yangu afe ugumba hiyo siku alitema sumu nyingi wifi yangu nadhani mnaoishi na familia ukiwa na changamoto hiyo mnaelewa hiyo siku niligombana sana na mwanaume na kumlalamikia kwamba kwanini dada zake wananifanyia vile basi kesho yake nilianza upelelezi wangu binafsi kutaka kujua kwanini mwanamke alitoka kwenye ndoa yake nikaja kujua yule mwanamke aliomba talaka kwa mwanaume yeye mwenyewe akimwambia mume wake mimba sio yake lakini hapo alidai talaka mimba ikiwa na miezi minne ikiwa miezi mitatu ya mimba aliishi na huyo mwanaume

Kwahiyo mumewe alikataa kumpa talaka kwa sababu ni mjamzito lakini yeye alienda hadi serikali za mtaa ili apewe talaka kwahiyo watu wazima waliamua apewe talaka hata kama ana mimba maana anaonekana mtu amedhamiria kutaka talaka kwahiyo alipewa talaka akarudi kwao wakati huo alikuwa ana mtoto wake wa kwanza na mimba ya miezi minne kwahiyo mume wake alikuwa anaenda nyumbani kwao kumuona na kupeleka matumizi ya mimba na ya mtoto na huku mume wangu nae alikuwa anaenda kupeleka matumizi ya mimba baada ya kujifungua ndo alimwambia mume wake mtoto sio wake ila siku ya 40 ya mtoto wifi zake upande wa mume wake walienda na zawadi wakapeleka baada ya kujua hayo nikaona au mume wangu amebambikiwa na yeye mwenyewe hajui?

Hebu niwe namuuliza baadhi ya vitu lakini alikuwa hanijibu kuna siku nikamuona mume wa yule dada kapost picha ya mtoto ambae mume wangu anamhudumia nikamuonyesha mume wangu nikamwambia usimtafute hebu tuone mwisho wa hili lakini mwenzangu kumbe hakuweza kuvumilia akamtafuta huyo mwanamke na kumwambia mwanamke muda huo huo akamtafuta huyo mume wake wa zamani na kumwambia afute hiyo picha ya mtoto aliyoiweka mtandaon aiseeee!!!!

Basi mimi kuna siku nikamtafuta huyo mwanamke kwa simu nikawa namwambia usije ukawa unatupa mtoto ambae sio wa mume wangu yule dada alinitukana na kusema mimi sitokuja kuzaa kwa huyu mwanaume kwa sababu nina laana ya mama mkwe kwamba mama yake mwanaume wakati anakufa alimwambia mwanae asinioe basi ikawa mimi kujua kwangu kama nimewapa uhuru wifi zangu pia kutoa sumu wakawa wanapostiana fb kwa mahaba sana hadi mimi baadhi ya rafiki zangu ambao sikai nao karibu walijua changamoto ya ndoa yangu kupitia fb sababu wana urafiki na wifi zangu tangu hapo nikawa siongei na wifi zangu tena

Kuna siku shangazi wa mwanaume akaniita ni mke wa mjomba wake yaani kaka yake mama yao mkewe akaniambia nisikate tamaa maana nilishaacha kuywa na dawa kuanzia hapo akasema tujaribu mara ya mwisho akaniambia mimi nitakusaidia hata hela basi kuna siku nikapita sehem nikaona duka la madawa nikaingia nikamuelezea huyo muuzaji changamoto zangu akanipa ushauri huyo mwenye duka la dawa ni nurse kwenye hospital ya AMANA nikamtafuta shangazi kumwambia gharama nilizoambiwa ilikuwa ni elfu stini(60) dose yote basi akanitumia elfu 25 nikanunua dawa nikaanza kutumia

Baada ya pale nikamshirikisha na mwanaume hela iliyobaki akawa ananipa kidogo kidogo ila pia wakati ule nilikuwa namshirikisha Mungu sana matatizo yangu changamoto yangu kubwa ilikuwa sipati period lakini zile dawa zilikuwa za siku(30) nilipofika siku ya (27) nikaanza kuingia period na nilipomaliza dose huku nikiwa kwenye perido nikarudi kwa yule Dokta akaniambia hapo nisitumie dawa yoyote nirelax na mume atoe ushirikiano

Basi mimi kufika mwezi wa tisa(9) 2022 nikawa ni mjamzito wa mwezi mmoja kwa kweli nilishukuru ila hata kipindi nina mimba mwanamke alikuwa ananitukana ananitumia picha akiwa ametoka na mume wangu kwakweli mambo yalikuwa magumu sana hadi nikajifungua mwaka jana mwezi wa nne(4) tena nilipata operation

Yule mwanamke alipata taarifa akaanza kunitafuta na kunikashifu kwa kupata kisu na kuniambia ninywe urojo basi kuna siku akapost picha yake na kusema mwakani zamu yangu 🫄muda huo mimi mwanangu mdogo aiseee mwaka Huu mwezi wa pili Yule mwanamke nikasikia ni mjamzito na hivi anakaribia kujifugua jamani mwanaume ameshindwa kuachana nae mambo hayo wapo tangu 2017 mimi naolewa hadi Leo na sio mwanamke mstaarabu huwa ananitukana sana Kama anataka mimi niondoke yeye abaki na mwanaume

Hebu nisaidieni kiushauri nimwachie tu mwanaume mimi nikaanze upya maisha yangu au nifanyeje maana ndoa imekuwa doa mawifi zangu hawana mapenzi na mtoto wangu wao wapo na huyo mwanamke wa kaka Yao na huyu mwanaume ndo mnafki nifanyeje Mimi?
Pole sana mkuu
 
Suratul mujadilah.... Kama n muislam soma hiyo kila siku usiku mara moja na asubuh mara moja!!!

Quran n muujiza ..... Ni mazingatio, tiba, ponyo la hapohapo, pia n uchawii
(Ni daraj la kwenda pepon ikitumika vizuri pia n njia ya moton kwa wenye elim kubwa za kiroho kwan wanaweza itumia vby kuleta maangamizi n.k)

Inategemea unaitumiaje.
(Ni vile kukosa elim za kiroho tu,
Ila hyo n inshu ndogo sana)

kama n mkristo nenda kamtafte padri huwa pia waaelim za kiroho wale nenda kweny parokia kubwa (nikisema elim ya kiroho simaanishi uchawi..... Yan namaanisha anaweza kuitumia Bible na aya zake kufanya muujiza
acha hawa wanaopiga kelele kwa kubahatisha,.
mfano ile sala ya BABA YETU ULIYEMBINGUNI,,,, ukimpata mtu anayejua kuitumia Bible haswaaa inaweza kukufanyia maajabu mpk ukashangaa

🚶🚶
 
Back
Top Bottom