Naona Kula Mgahawani ni nafuu kuliko kupika kwa mtu mmoja

Hio ndio biashara ambayo inanifanya nishindwe kupika yani. Kupika ni raha sana ila ingekuwa kuna namna ukishashiba vyombo vinajiosha ingekuwa raha sana. Mchina atufyatulie mashine hio tafadhali. Kupika sio kazi, ishu kuosha vyombo yani ndio balaa!!!
Unaweza mwaga maji chumba kizima, mara kudeki, yani full karahaa
 
Mkuu upo vizur kama mm tunafanana
 
Hahaha
Changamoto nayopata ni kuosha vyombo...inafika mahali natamani vuta jiko. Pia naeza enda gengeni 3 times...kwan naeza fika gheto..mara nimesahau...karoti...sijui hoho...tangawizi...daah kazi kweli..
sasa mkuu we hujui unaenda pika nini kwani? Huwezi kuwa serious, unataka uunge mboga kisha ufikegeto umesahau kitunguu na nyanya
 
Kusema ukweli kwa mtu mmoja kupika mwenyewe ni usumbufu zaidi bora tu ule mgahawani.

Faida unazozikosa ni ubora wa chakula kwa kuwa hauna maamuzi au mamlaka juu ya kiasi na aina ya mafuta wanayotumia, ubora wa nafaka na vitu vingine.

Hii ni tofauti na ukiandaa mwenyewe, tatizo ni ile usumbufu na kupoteza muda.
 
Hakika mkuu!!
 
Hahaha

sasa mkuu we hujui unaenda pika nini kwani? Huwezi kuwa serious, unataka uunge mboga kisha ufikegeto umesahau kitunguu na nyanya
Najua mkuu...unajua wanaume ni tofauti na wanawake. Mwanamke anaelewa labda ndani..vitu hivi vinakaribia kuisha....nini kinahitajika hasa kwenye maswala ya maakuli...lakini kwa mimi sometime na gues viungo vingine vitakua ndani...ko sinunui..kumbe vishaisha..ndo balaa linaanzia hapo
 
Wanapendwa kuanzwa hao. Ebu tia gia kwanza halafu uone kama yajayo hayafurahishi
Hahhahahah
Mkuu ngoja nimpe mtongozo wa hapahapa na wanajukwaa waone, akinikataa mshuhudiee, akikubali mshuhudiee...

culture gal wadau wanapenda mimi na wewe tudumu na hata milele,

Sijui ww unaonaje??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…