Naona wazazi wangu wamenichoka, ni muda sasa nami nianze kujitegemea

Amri ya tano, Waheshimu baba na mama upate miaka mingi na heri duniani.
Mbona me nawaheshimu sana tena sana kama kazi walizoniambia nifanye nafanya tena kwa moyo mmoja ila lipokuja suala la kufokewa na maza tena kwa sauti kubwa kwenye mambo madogo madogo kwangu mimi hili apana kwakweli nimevulimia sana ila naona imefika mwisho nahitaji kupata utulivu wa nafsi ndio maana nimeamua kuanza harakati za kutafuta chumba na niwaage kwa amani. Sasa hapo mkuu mimi kosa liko wapi au kuna sehemu gani mimi nimeonyesha zarau kwa wazazi
 
kwa umri huo bado unastahili kufanya kazi za nyumbani japo sio kuosha vyombo,kufagia ndani au kudeki choo,labda kama unaishi wewe na wazazi tu nyumbani lkn km kuna watu wengine hapo nyumbani fagia uwanja,fyeka majani,punguza matawi ya miti km ipo ila kama hata hayo huwezi sawa hama lkn sio kuwakasirikia wazazi iyo ni mbaya sana...
 
Huu uzi japo ww mtoa mada unaumia mm huku nakufa mbavu..
Any way pole sana hata mimi nahisi nitakua mzazi mwenye ngenga(maneno maneno)
 
Sasa mkuu kama kula home nakula usiku tu nikirudi na kama kuwategemea wazazi basi ni sehemu ya kulala tu ila mengi najitahidi kujihudumia mwenyewe ila manyanyaso bado hayaishi.
Ni manyanyaso au kuhimizwa kuwajibika kama kijana uliyepo hapo nyumbani?
 
Malezi mazuri toka utotoni yanasaidia sana kupambana na changamoto ukubwani.
Nakumbuka Mother kipindi nasoma secondary school nilikuwa TV room naangalia lBonge la movie, mama aliponikuta naangalia TV mpaka usiku alizima na kuambiwa niende chumbani kulala, nilimind lakini hamna namna, sasa hawa vijana wetu wa sasa ukiwafanyia hivyo lazima aje kukuanzisha thread JF.
 
Hamna bana kuna wazazi wengine wanyanyasaji kweli...bullying their own children etc...
 
Sijui ni utandawazi au malezi,,Mimi nimeshindwa kabisa kumuelewa kijana eti hataki kugombezwa....Binafsi nimeshuhudia Wazazi wangu baba ,baba wadogo,na mashangazi zangu wakienda ndivyo sivyo Bibi yangu alikuwa anawakalisha chini na anampa mtu risala,,,,na wazee wanakuwa humble wanaenda kulalamika pembeni .Hiyo tumerithi hadi watoto pamoja na ukubwa wetu mzazi akikoroma unakuwa mtiifu.Ngoja kwanza akafundishwe na ulimwengu
 
Waefeso 6:1-3
Waefeso 6:1-3

Watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, kwa maana kufanya hivyo ni vizuri. 2 “Waheshimu baba yako na mama yako,” hii ndio amri ya kwanza yenye ahadi, 3 “upate baraka na uishi siku nyingi duniani.”
 
Tukiwambia watu Kuna wazazi wanateza watoto wao Wana kataha


Mm mwenyewe nilioyapitia kwa kaka angu siwezi sahaugi nakikumbuka nalia kbsa

Ila SAS nimetuliaa nimekuwa kma adui SAS Sina hamu nae
 
Tukiwambia watu Kuna wazazi wanateza watoto wao Wana kataha


Mm mwenyewe nilioyapitia kwa kaka angu siwezi sahaugi nakikumbuka nalia kbsa

Ila SAS nimetuliaa nimekuwa kma adui SAS Sina hamu nae
Umeandika kwa hasira mpk mwandiko umechanganywa
 
Waefeso 6:1-3

Watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, kwa maana kufanya hivyo ni vizuri. 2 “Waheshimu baba yako na mama yako,” hii ndio amri ya kwanza yenye ahadi, 3 “upate baraka na uishi siku nyingi duniani.”
Kwani amesema awaheshimu ?au wao ndio Wana msakama kila siku na kumfanya ashundwe kujiamini Hadi anambiwa kak mudi kaoshe vyombeee na nk .....
Dr vip ....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…