Naona wazazi wangu wamenichoka, ni muda sasa nami nianze kujitegemea

Naona wazazi wangu wamenichoka, ni muda sasa nami nianze kujitegemea

Vyombo sio kwamba sioshi mkuu!! Vyombo naosha sema maza bado atakufokea mara huoshi vyombo vizuri mara vyombo utavivunja unavibamiza kwa nguvu yaani maneno ni mengi
Mmh huyu sasa kazidi[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] Una uhakika ni mama mzazi kweli???
 
tabia yako au tabia zenu watoto mliozaliwa kuanzia 1995 ni ovyoo sana wazazi wameisha kata tamaa na tabia zenu mnakaa kuiga wasanii mnaona ndio njia bora ya kuishi kumbe mzazi hapendezewi na tabia zenu mimi kama mzazi natamani muondoke mkaishi huko mnapojua nyinyi
 
Habarini wakuu! Ni mimi kijana wenu humu jamiiforums nina miaka 21, kama mnavyojuwa umri huu bado nipo masomoni chuo flani hivi apa dar na bado nipo home.

Sasa tuludi kwenye mada, unajua nini hapa home sipaelewi sikuhizi nimekuwa nikichukiwa pasipo na sababu za msingi, hasa bi mkubwa amekuwa mtu wakunifokea fokea hadi majirani huwa wanasikia jinsi ninavyofokewa. Majuzi kati hapa niliambiwa sikuhizi hapo home sifanyi kazi na ninachelewa kurudi nyumbani, nikiwauliza wazazi wangu ni kazi gani wanataka mimi nizifanye hapa nyumbani naambiwa nioshe vyombo, mara nifyeke majani na mikazi mengine kibao.

Okay siku na kipingamizi kwasababu hawa ni wazazi wangu hivo ni wajibu kuwasikiliza na sio kwamba siku za nyuma nilikuwa sifanyikazi? Hapana ni kutokana na majukumu ya masomo huku chuoni yananibana sana hivo nakuwa mtu sio wakushinda nyumbani maana mda wote na huku chuoni huwa na baki mpaka saa 3 au nne usiku ndio narudi home. Nafanya hivi ili nikimbie majukumu ya nyumbani ila baadae nahisi wazazi wangu walinishukizia.

Anyway sasa kila nikifanya kazi za hapa nyumba bado maneno yanakuwa mengi mara uwambie urudie kuosha vyombo mara mbili wakati apo vyombo ushaosha na vinan'gaa bila shida , ukitoka hapo mara uwambiwe chooni unaachafua mara hausafishi mara unaingiza mchanga mara uwambiwe uliacha mavi leo asubuhi yaani maneno yanakuwa mengi halafu bimkubwa anaongea kwasauti kubwa hadi majirani wanasikia

Mimi hali hii sipendezwi nayo, naona wazazi wangu kama wameanza kunichoka, hapa nafanya mpango mwisho wa mwezi huu nichomoke hapa home najua mwanzo wa kujitegemea huwa mgumu ila potelea mbali siwezi kuendelea kukaa home huku nikidharirishwa na maneno ya bimkubwa.

Anyway natafuta chumba bei iwe 50k maeneo kuanzia ubungo kibo, kona mpaka kimara korogwe. Kama unaona au unasikia kuna chumba kinapangishwa maeneo hayo anipange sasa. Wakuu #natanguliza shukuran
Sasa pokea ushauri huu,sema na wazazi wako uwape ukweli wako wote,pia timiza wajibu wako vizuri tu na wazazi wako watakuheshimu tu
 
Wewe barehe inakusumbua na inaonekana una kiujinga Fulani hivi(sorry). wasikilize wazazi wako dogo utakuja kujuta, wewe unadhani kusoma ndo iwe sababu ya wewe kushindwa kusaidia kazi za nyumbani mpaka ulazimishwe?

Kwanza hapo kwenu hakuna kazi, yaani kuosha vyombo na kufyeka majani nayo kazi? Sisi wenzako tulikua tukitoka shule jioni tunapitiliza shambani kwenda kulima, na usijifanye eti Leo nimechelewa kutoka shule, utaikuta nafasi Yako ya kulima umeachiwa ipo inakusubili!!

Kwanza kazi nyingine sio mpaka uambiwe, kwa hiyo wewe unataka ukute chakula mezani tu unakula na kwenda kulala? Kazi hutaki? Njoo uishi kwangu uone kama hujatimka ndani ya siku mbili tu dadeq
 
Pole sana kuna wazazi na walezi wengine huchangia kuharibu watoto manyanyaso yanakuwa mengi mm nishawahi ishi maisha kama hayo nilivumilia mpaka muda ulipofika nikaondoka.
Mkuu usimjaze ujinga huyo dogo hataki kazi! Awe makini tu asije akawa choko. Mimi siku zote ninaamini mzazi hawezi kumnyanyasa wanae labda kama huyo mzazi ana matatizo ya akili.

Waswahili walishasema usie funzwa na ***** Dunia itamfunza.
 
Yani umeona swala lako wewe na familia yako tena WAZAZI wako ndio litapatiwa suluhisho humu,acha akili za kijinga kijana huo ujana usikupeleke pupa hivyo,Mzazi ana wajibu wa kukuambia chochote ikiwa hakileti madhara kwako na sijaona sababu ya wewe kulalama humu kisa tu kuambiwa ufanye MAJUKUMU ya HAPO NYUMBANI,kabla haujawa na miaka mpaka leo wamepambana,wamekupigania vya kutosha mpaka sasa hapo ulipo,huna haja ya kulalama mtandaoni humu hakuna msaada mkuu.

Rudi tena kwa Mama kapige magoti kamuombe msamaha huwezi jua kuna kitu ulifanya ama yeye anahisi kuna kitu mbele huko utafanya ambacho si kizuri.Kama waliweza kugundua wakati wewe bado ni mtoto mdogo hujui kuongea,wewe ni KUCHEKA na KULIA pindi ukipata maradhi hata ya tumbo basi Mzazi anajua hata kama huja muambia.

Heshima iwafikie WAZAZI WETU WOTE haijalishi wametulea katika mazingira Gani.

Tatizo la vijana wa sasa tunapenda sana USASA maisha ya TV na MTANDAONI {GLOBALIZATION} angalia WAZAZI WETU pindi walivyokuwa na umri kama wako walikuwa wanapewa majukumu gani kwao kwa WAZAZI WAO.

AHSANTE.

Sent from my V2204 using JamiiForums mobile app
Matoto ya siku hizi ndio maana mengi yanakua machoko, Mzazi ukiingia tu kwenye mtego wa kumlea mtoto anavyotaka basi ujue umesha mharibu mtoto. Yaani dogo analalamika eti kuosha vyombo? Kufyeka majani ya uwani? Kusafisha vyoo? Kusafisha uwanja?

Una miaka 20 alafu kazi kama hizo unataka mpaka mama akufokee ndo ukazifanye tena kishingo upande? Kweli? Wadau nao mna muunga mkono??
 
Mkuu nakushauri usitoke hapo home. Ni heri ukavumilia hayo unayoita manyanyaso, kuliko kukutana na mateso ya kuingia kitaa kurupu kurupu bila mipango.

Bado uko chuo, matumizi na mahitaji yako ni mengi sana. Nakushauri endelea kujipanga mdogo mdogo, make sure siku unayo graduate chuoni, tayari uwe na ramani kamili ya kuingia mtaani.

Yani kwa ufupi, uwe na double graduations. Yani unagraduate chuo, at the same time una graduate nyumbani.

Ila ukisema utumie hasira na kuondoka home sasa hivi bila plan, trust me, chance ya kupoteana ni kubwa mno, na hivi double kick na smart gin ni 2000? Si
 
Mkuu, kwanza nisamehe kama tafsiri iliyokuja kwako ni kuwa nakutishia maisha.

Pili, naomba nikutakie heri katika huo uhamuzi wako.
Mpaka hapo sie tushajua kwa Nini mama yake anamfokea! Kiufupi dogo pasua kichwa, na siku akiondoka hapo home bibi mkubwa wake atachinja kuku na kujipongeza.
 
Back
Top Bottom