Naondoka na Slaa kampeni ya CHADEMA Asilia!

Naondoka na Slaa kampeni ya CHADEMA Asilia!

jingalao

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2011
Posts
36,197
Reaction score
29,717
Nimepita maeneo ya mianzini jijini Arusha kuna kampeni ya chini kwa chini yenye kupeana hamasa kuwa wanachadema asilia waliojitolea kupigwa risasi na mabomu pale Soweto kwa ushawishi wa Ufuasi wa Slaa.

Sasa wameweka nadhiri kuwa watahama na kumfuata kokote mpendwa wao Dr Willy Slaa ambaye ni baba wa vita dhidi ya ufisadi Tanzania.

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA.


Sababu kuu ni hii, Slaa amejitahidi sana kukijenga CHADEMA, na sio siri CHADEMA imekuwa na nguvu sana baada ya ujio wa Slaa, kama lilivyo jina CHADEMA ni chama cha demokrasia, lakini demokrasi inaanza kutoka na ubabe unaingia.

Kulikuwa na wagombea walitakiwa kuchukua fomu za urais kisha kura za maoni zipigwe hilo limekufa, Lowassa kaja kabaka demokrasia kwa kusema anataka yeye tu apitishwe bila kupingwa, swali langu ni hili kama yeye Lowassa ana mvuto na wafuasi wengi anaogopa nini kupambana na wengine kwenye kura za maoni?

Kwa mtu mwenye uchungu wa nchi huwezi kuanza kumsafisha mtu ambaye hajajisafisha bado, kuna watu wanasema Lowassa katubu, kutubu nijuavyo mimi unakubali kosa kwamba ndio ulifanya kisha unaomba msamaha, lakini Lowassa hajafanya hilo ila amekana hahusiki na lolote analoulizwa, ikiwa hali ya kukana jambo ni kutubu mafisadi wote watakuwa wametubu maana wote wana tabia ya kukana,

Wabunge wengi wa
CHADEMA wamekuwa wakijitahidi kujenga hoja na kuongea na waandishi wa habari kwa lugha nzuri, misingi iliyowekwa na watu kama kina dr. Slaa, lakini leo anakuja Lowassa anaulizwa swali anasema "shut up", "keep quite" haya ni majibu ya hasira na kutisha watu ambayo hayakuwepo CHADEMA, lugha hii anaitumia kwa sababu yuko CHADEMA na watu wanashangili ila angesema maneno haya akiwa CCM angetamani ardhi ipasuke.

Hii inanikumbusha mchezo wa redio wa mzee Jangala na mwanae Mshamu, Mshamu anasema "dingi noma hivyo" kwa sababu Jangala hajui maneno ya kihuni anamsifia mtoto wake kwamba anaongea kiingereza kigumu.

CHADEMA wanasema system ya CCM ndio inawafanya watu wawe mafisadi na Lowassa katoka hiyo system na sasa atafuata system ya CHADEMA na UKAWA, lakini kabla hata ya wiki CHADEMA na UKAWA wanafuata system ya Lowassa kwa kuondoa wagombea wengine ili Lowassa apite bila kupingwa na hili ni sharti alilototoa Lowassa, system ikapindwa.
Dr. Slaa, tunakuomba uwatendee haki wananchi kwa kuanzisha chama kipya cha siasa. Sioni chama chochote cha siasa ambacho Dr. Slaa anaweza kujiunga nacho. Siyo CHADEMA ambao wameamua kumsaliti Dr. Slaa ambaye alihatarisha maisha yake na familia yake na wengine kukipa CHADEMA heshima iliyopata kabla ya ujio wa Lowassa. Dr. Slaa pia hatakiwi kujiunga na CCM, wala ACT, wala CUF, wala NCCR mageuzi wala chama chochote cha siasa.

Kitu pekee anachoweza kufanya Dr. Slaa ili kuwatendea haki wananchi watanzania ambao wanadhamira ya kweli ya kupigana na ufisadi kwa dhati kabisa ni kuanzisha chama kipya cha siasa. Hata kama Dr. Slaa ataanzisha chama chake baada ya uchaguzi mkuu itakuwa ni vizuri mno. Ukweli ni kuwa uongozi wa Dr. Slaa akiwa na chama chake cha siasa unahitajika sana ili wananchi waliopondeka moyo kwa unafiki wa CHDEMA na UKAWA wapate pa kujisitili.

Madonda na makovu ambayo CHADEMA kwa kughilibiwa na UKAWA wameyacha kwa wananchi wapenda haki ni makubwa mno. Njia ya pekee ni kwa Slaa kuanzia chama kipya cha siasa. Kiukweli CHADEMA wamemfanyia Dr. Slaa na wapenda haki wote kitu kibaya mno. Binafsi nimesononeshwa sana.

 
Wakifanya Hivyo Watakuwa Lossers....Ni Neema Kupokea toka CCM Na Ni Kipindi Cha Kutulia na Kuanza Kula Matunda ya Mabomu ya Arusha.

Ni Mjinga tu atakayechua Maamuzi ya Kuiama CHADEMA Kwende Upande wapinzani Watarajiwa. Kama CUF,NCCR na NLD Wamekubali

Kuwa Lowassa Asimame Eti Kuna Mtu wa CHADEMA ambapo Ndio Mgombea wa Umoja Anatoka Atajichanganya na Kutoka, Hii Itakuwa

Sawa Sawa na Kupishana na Gari Linalokuja na ATM Card.
 
Dr Slaa akiondoka maana yake hesabu hazikuzingatiwa kabla ya kumkaribisha Lowasa..... tumesisitiza kumuunga mkono Lowasa kama viongozi wetu wakuu wote wamekubali kwa dhati hesabu zimezingatiwa....kinyume na hapo sitounga mkono maamuzi haya.....
 
Wachochezi tu nyie, hamna lolote, kama viongozi wa CHADEMA akiwemo Slaa wamekubaliana kumpokea LOWASSA nyie mna nini cha kuwaambia wananchi?
CHADEMA wamefanya kitendo cha ki - UNGU kumpokea LOWASSA aliyenyanyaswa vya kutosha na mfumo kandamizi, pia akapokwa haki yake na KITENGO ambacho hakiko kisheria! Sasa ukisema mambo ya kuondoka CHADEMA wakati huu ambapo neema imewazukia kila mtu anakuona wa ajabu! Tulieni LOWASSA achukue Nchi Kwanza!!!
 
Mussa umenena sahihi kabisa....huu ndo muda wakupanga na c kubomoa
 
Lawezaje neno jema kiutoka nazareti?
wachochezi tu nyie, hamna lolote, kama viongozi wa chadema akiwemo slaa wamekubaliana kumpokea lowassa nyie mna nini cha kuwaambia wananchi?
Chadema wamefanya kitendo cha ki - ungu kumpokea lowassa aliyenyanyaswa vya kutosha na mfumo kandamizi, pia akapokwa haki yake na kitengo ambacho hakiko kisheria! Sasa ukisema mambo ya kuondoka chadema wakati huu ambapo neema imewazukia kila mtu anakuona wa ajabu! Tulieni lowassa achukue nchi kwanza!!!
 
Slaa amesalitiwa zaidi ya lowasa kwa nn aonekane lowasa ameua zinguliwa ila slaa hapana
 
Wachochezi tu nyie, hamna lolote, kama viongozi wa CHADEMA akiwemo Slaa wamekubaliana kumpokea LOWASSA nyie mna nini cha kuwaambia wananchi?
CHADEMA wamefanya kitendo cha ki - UNGU kumpokea LOWASSA aliyenyanyaswa vya kutosha na mfumo kandamizi, pia akapokwa haki yake na KITENGO ambacho hakiko kisheria! Sasa ukisema mambo ya kuondoka CHADEMA wakati huu ambapo neema imewazukia kila mtu anakuona wa ajabu! Tulieni LOWASSA achukue Nchi Kwanza!!!

Mkuu.... Ilikuaje Mwenyekiti akasahau kwamba yeye ni mwenyekiti??
Hahahaha.... Alivurugwa na nini?!?
 
Nimepita maeneo ya mianzini jijini Arusha kuna kampeni ya chini kwa chini yenye kupeana hamasa kuwa wanachadema asilia waliojitolea kupigwa risasi na mabomu pale soweto kwa ushawishi wa Ufuasi wa Slaa.

sasa wameweka nadhiri kuwa watahama na kumfuata kokote mpendwa wao Dr Willy Slaa ambaye ni baba wa vita dhidi ya ufisadi Tanzania.


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA

Username can speak it all like that one of lazy bone aka Lizaboni
 
Last edited by a moderator:
Mkuu.... Ilikuaje Mwenyekiti akasahau kwamba yeye ni mwenyekiti??
Hahahaha.... Alivurugwa na nini?!?

Hujasikia Mwandosya anakwambia kuwa JAKAYA alikuja na majina yake kwenye wallet? Sasa amefanya manuva mpaka akasahau kuwa yeye ndiye mwenyekiti wa mkutano ule! MWISHO WA UBAYA NI AIBU TUPU!!!
 
Binadamu sio wakwasikiliza sana siku zote kabla lowassa hajahamia chadema walisema slaa sii chochote wala lolote kwanza hana mvuto

Leo lowassa yupo chadema wanasema lowassa mwizi
Hii dunia ya ajabu sana mtu unavyo ingia kwenye siasa jaribuni kuwa wavumilivu je mtahama vyama mpaka lini? Na Kwenye maisha hamna kitu duniani kilicho kamilika 100% so kama tunaemdelea kuwa wazima na
Lowassa kwa bahati yake kapitishwa na ukawa sio mbaya tutampigia kura na maisha yataendelea kama kawaida hamna kitu kitaalibika.
 
Wachochezi tu nyie, hamna lolote, kama viongozi wa CHADEMA akiwemo Slaa wamekubaliana kumpokea LOWASSA nyie mna nini cha kuwaambia wananchi?
CHADEMA wamefanya kitendo cha ki - UNGU kumpokea LOWASSA aliyenyanyaswa vya kutosha na mfumo kandamizi, pia akapokwa haki yake na KITENGO ambacho hakiko kisheria! Sasa ukisema mambo ya kuondoka CHADEMA wakati huu ambapo neema imewazukia kila mtu anakuona wa ajabu! Tulieni LOWASSA achukue Nchi Kwanza!!!

cc: Lizaboni
 
Last edited by a moderator:
Jaman niulize kiswali kwan chadema ni chama cha wachaga au maana wengi ninaowaona ni wachaga tukiwapa wachaga c ndo kila seckita ngazi za juu watakuwa wachaga tuuuu
 
Jamani [MENTION]MUSA ALAN[/MENTION], ID yake imekuwa hacked? Au naota vile.
Otherwise nakubaliana na Mbowe, kuwa politics is the game of dynamics na unaweza kubadili gia ukiwa angani. Hongera MUSA ALAN kwa kubadili gia angani
 
Wachochezi tu nyie, hamna lolote, kama viongozi wa CHADEMA akiwemo Slaa wamekubaliana kumpokea LOWASSA nyie mna nini cha kuwaambia wananchi?
CHADEMA wamefanya kitendo cha ki - UNGU kumpokea LOWASSA aliyenyanyaswa vya kutosha na mfumo kandamizi, pia akapokwa haki yake na KITENGO ambacho hakiko kisheria! Sasa ukisema mambo ya kuondoka CHADEMA wakati huu ambapo neema imewazukia kila mtu anakuona wa ajabu! Tulieni LOWASSA achukue Nchi Kwanza!!!
Tukikuuliza sababu ya msingi ya malalamiko yako yanayosisitiza Lowassa kuwa bora kwako na watanzania kama rais huwezi kusema!
 
Back
Top Bottom