Nape Nnauye: Nilikatazwa Kwenda kuchunguza Uvamizi Clouds, niliambiwa nitafukuzwa kazi

Nape Nnauye: Nilikatazwa Kwenda kuchunguza Uvamizi Clouds, niliambiwa nitafukuzwa kazi

Nape mbona unataka ushujaa usio na msingi. Ulienda kuomba msamaha wa nini ikulu? Kama ulikuwa na misimamo si ungekaa zako Lindi ulime kama Ally Hapi then ndio uje utusimulie?

Nape fanya kazi uliyotumwa, hizo hadithi zako hazibadili chochote. Tasnia unayosimamia ina matatizo mengi na mengine ulishiriki kutengeneza ikiwemo sheria ya kukataza bunge live.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
Alienda kuomba msamaha ili kumzuga mchungi wa ng'ombe
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye amesema wakati anaenda kufanya uchunguzi wa uvamizi uliofanywa Clouds na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda alizuiwa kwa kuambiwa kuwa atafukuzwa kazi kama ataenda kuchunguza tukio hilo.

“Asubuhi yake nilizuiwa kwenda kuchunguza, nikaambiwa ukienda utakuwa hauna kazi. Nikasema ni bora nisiwe na kazi lakini nilinde heshima.”

Ameongeza, “Kwa sababu katika mazingira wewe ndiyo waziri, watu wanavamia kituo, halafu wewe unatakiwa usiende. Unachagua kati ya heshima na kazi. Heshima utaenda nayo, kazi ipo siku itaondoka tu, kwa hiyo nikachagua heshima ambayo nadhani naendelea nayo leo”.

"Kwamba mwajiri anasema ukienda kazi huna, nikasema sawa, halafu mimi naendelea kusema tunachunguza, mwajiri anasema bhana wewe uliyevamia endelea na kazi vizuri hakuna shida"

Baada ya tukio hilo, Waziri Nape amebainisha kuwa waliunda Tume ambayo siku ya kusoma ripoti walianza kushauriana wasome au wasisome, ambapo aliwaaambia wajumbe wa tume kuwa kama wataisoma yeye hatakuwa tena na hiyo kazi.

"Wakasema Mhe. Waziri tukisoma utafukuzwa kazi, nikasema ndiyo na nimetoka kuthibitishiwa pia sasa hivi maana kabla ya pale nilipitia mahali, nikasema jamani ile taarifa ipo tayari na wananisubiria tufanyeje? Wakasema sasa uamue, uisome afu uondoke au uinyamazie uendelee na kazi. Nikatafakari, nikachagua heshima maana haviwezi kukaa pamoja"

Amekiri kuwa hata kitendo cha yeye kuondolewa wizarani hakikumshangaza kwa kuwa alijua litatokea, wakati anapokea taarifa aliwaambia wajumbe wa tume kuwa kuna gharama za kulipa baadae na yeye yupo tayari.
Nyau huyu kwani hakufukuzwa? Ajabu anafikiri yuko sawa kwa hizo falsafa zake za uhuru hadi nchi imeingiliwa na ushoga na usagaji.
 
Mchungi na udikteta wake wote mbona hakuufuta ushoga? Au Mfufueni aje aufute
Nyau huyu kwani hakufukuzwa? Ajabu anafikiri yuko sawa kwa hizo falsafa zake za uhuru hadi nchi imeingiliwa na ushoga na usagaji.
 
Na Mungu huyo huyo ndio aliyeacha Lissu apigwe risasi kama asingetaka isingekuwa.
Lissu anaishi na ni mwenye furaha na matumaini makuu ya Tanzania mpya ijayo, mchungi funza walishajifaidia siku nyingi.
 
Hapana. Ule ulikua sio uvamizi. Makonda na Clouds walikua washkaji sana.Uhusiano wao ulivuka mipaka ukiangalia before hawajagombana. Hakuna kiongoz alikua anaingia chumba cha utayarishaji lkn makonda alikua anaingia. Kugombana kwao, Nape akataka kutake advantage. Ukifuatilia utaona Makonda na Nape walianza kuvutana kwenye ishu za madawa ya kulevya. Nape alitaka ugomvi wa Clouds na makonda umnufaishe yeye.
Nape alitaka aenda kuchunguza kwani yeye ni jeshi la polisi, sasa atakama angechunguza angempeleka Makonda Mahakamani.
 
Mungu huyo huyo ndie aliyemuokoa Nape asiuwawe.
Hakukuwa na shambulizi lililopangwa kwa ajiri ya kumuuwa Nape hadi useme kaokolewa na kifo, katishiwa bastola akaogopa basi.
 
Huyu nadhani ndiye waziri hopeless zaidi ambaye Tanzania tumewahi kuwa naye. Yani ukimfuatilia mpaka u ajiuliza hivi huo uwaziri watu huwa wanaupataje?
Maskini Tanzania yangu 😢😢
 
Back
Top Bottom