Nape Nnauye: Takribani miti milioni 3.5 ilikatwa kupisha ujenzi wa Umeme JNHP (Stieglers)

Koryo2

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
2,056
Reaction score
2,519
Your browser is not able to display this video.


Your browser is not able to display this video.


Nimemuona Mhe. Nape akichangia hoja yake kwenye Bunge letu la Jamhuri ya Tanzania kuwa kupisha ujenzi wa mradi wa umeme wa Mwalimu Nyerere kunahitajika kukatwa miti takriban 4.3.

Akazidi kuelezea kuwa eneo linalotakiwa kukatwa miti hiyo ni sawa na eneo lote la Dar es Salaam au eneo lote la Unguja. Akaendelea kueleza athari itakayotokana na ukataji wa miti hiyo ni upungufu mkubwa mvua katika Mikoa ya Mtwara, Lindi, Iringa n.k. na hivyo athari hii itawafanya wananchi wakose mvua kwa ajili ya shughuli zao za kilimo.

Mimi binafsi sijaamini maneno yake kama ni ya kweli LAKINI kama ni ya kweli lazima tuwalaumu sana Wabunge wetu tunaowapeleka Bungeni kwa kutosimamia yale tuliowatuma.

Kwanini awamu ya tano kila kitu kilikuwa ndiyoooo bila kutafakari hoja zinazoletwa mbele yao. Miti 4.3m inakatwa?. Wabunge mnashangilia?. Wananchi tuje tukose mvua ikichukuliwa kuwa mvua ndiyo maisha yetu? Hapana hapana.

Tunawaomba tunapowatuma Bungeni simamieni hoja za kuwasaidia wananchi na siyo kumridhisha mtu mmoja. Kwa usemi wa Mhe. Nape kuna shida kubwa sana huko mbele.

======
UPDATE:

 
Mh Nape hapo alikuwa akichangia hoja na akishauri serikali kabla hapa mradi haijaanza. Kuwa waangalie athari za mazingira kwa ukataji huu mkubwa wa miti,ila serikali ya 5 ilikataa huu ushauri na Hayati Magu akatoka adharani akasema kuna wanasiasa na wataalam wameongwa ili mradi usifanyika ila sisi tunakwenda kujenga
 
Wewe na Nape wako wote ni wa kupuuzwa tu.
Nchi hii haihitaji wachumia tumbo kama nyinyi?
 
wakate tu, CCM si ndiyo inaamua wanachokitaka, sheria ndiyo nini ndugu Nape katika nchi hii - sheria za uchaguzi zinavunjwa waziwazi mbona ulikuwa kimya unakunywa kahawa na jamaa zako mkifurahia kupita bila kupingwa.
 
Wewe pia nakulaumu kwa kukosa akili ya kuelewa vitu vidogo sana.Wewe unaweza kupingana au kumhoji mtu ambae amekupa ubunge bure?Unahitaji PhD kujua kuwa enzi za Magufuli wabunge hawakutokana na wananchi bali walitokana na mkono wa serikali kupitia uporaji wa chaguzi?

Unayoyaona ni matokeo ya uporaji wa demokrasia na athari za wananchi kukaa kimya pale demokrasia inapoporwa.Wanaopaswa kulaumiwa hapa ni wewe,mimi na yule kwa kukaa kimya pindi demokrasia inapoporwa.Hujapata taarifa hapa kuwa sasa hivi Ndugai ndiye kambi rasmi ya upinzani bungeni?Unategemea ndugai atetee wananchi au amtetee yule aliempa ubunge(serikali)?
 
Tangu Jiwe aondoke Nape anakuja na Nondo za Kutosha.

-Legasi haitetewi bali inajitetea nyenyewe.
-Iundwe tume ya kuchunguza mikopo iliyokopa awamu ya 5.
Hii ni ya zamani. Kabla hata mradi haujaanza. Ila thread za kupinga huu mradi zinaanzishwa sana siku hizi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…