BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia amethibitisha kuwa Serikali inakamilisha mchakato wa utungwaji wa Sheria hiyo itakayolinda taarifa binafsi za watu.
Kauli ya Nape inakuja wakati kukiwa na madai mengi ya sheria hiyo kutoka kwa watu binafsi na taasisi ikiwemo JamiiForums ambayo imekuwa ikisisitiza umuhimu wa Sheria hiyo kutokana na ukusanyaji, uchakataji na utumiaji holela wa taarifa binafsi bila kuwa na ulinzi.
Amesema "Tumeshuhudia hapa nchini mtu anaingilia privacy ya mtu anachukua taarifa anaziweka hadharani, ndani ya miezi michache tutatunga sheria ambayo itaeleza nani anakusanya taarifa gani, anaziweka wapi, anazichakata vipi anazitumiaje na nani anawajibika".
Mkurugenzi wa JamiiForums akiongea na East Africa Radio alithibitisha kuwa wamepeleka pendekezo la Muswada ambao unaishauri Serikali juu ya umuhimu wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi.
Kauli ya Nape inakuja wakati kukiwa na madai mengi ya sheria hiyo kutoka kwa watu binafsi na taasisi ikiwemo JamiiForums ambayo imekuwa ikisisitiza umuhimu wa Sheria hiyo kutokana na ukusanyaji, uchakataji na utumiaji holela wa taarifa binafsi bila kuwa na ulinzi.
Amesema "Tumeshuhudia hapa nchini mtu anaingilia privacy ya mtu anachukua taarifa anaziweka hadharani, ndani ya miezi michache tutatunga sheria ambayo itaeleza nani anakusanya taarifa gani, anaziweka wapi, anazichakata vipi anazitumiaje na nani anawajibika".
Mkurugenzi wa JamiiForums akiongea na East Africa Radio alithibitisha kuwa wamepeleka pendekezo la Muswada ambao unaishauri Serikali juu ya umuhimu wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi.