Wazo lako ni zuri lakini kiuhalisia utapata hasara!...kwa mtaji wa laki5 huwezi kufanya biashara ya vitenge kutoka kigoma kwa kumtuma mtu asiyekuwa na uzoefu,tena umgharamie chakula na malazi aende kufuata pea 10 za vitenge then ukopeshe uanze kudai!!!!...utaishia kujuta kumbe tatizo ni mipango!
Kwa bei ulizozitaja unaoneka hujafanya utafiti wowote kuhusu biashara ya vitenge kwenye mikoa ya karibu...mfano Dar...Dom..vitenge vya wax pc3 bei za jumla ni 20000-22000,sasa kwann uende kigoma kwa mtaji wa laki5!?tena unatuma mtu badae ukopeshe!
Hujasema unafanya kazi gani lakini
Ushauri wangu:
Kwa mtaji ulionao unafaa ufanye biashara ya nafaka:uza mchele bei za jumla maeneo ya uswahilini,tafuta watu wawili committed wenye maduka au vibanda vya mtaani msaini mkataba uwe supplier wao, laki5 unaeza kuanza na gunia 2(kg200)ukipata Faida ya 150-200 kwenye kg1 si chini ya 30000kwa wiki×4=120,000.
Ukitoa gharama za bodaboda wa kupeleka mzigo madukani na dharura hata ukipata elfu80 kwa mwezi, hii ni sawa na mifuko mitano ya cement!!
Au vinginevyo tafta eneo dogo la wazi isiwe mbali sana na makazi yako..(unaeza ukakodi) lima mbogamboga za fasta (mchicha,chinese,pilipili)anzisha kilimo cha umwagiliaji then mweke kijana (cheap labor)asimamie uzalishaji alafu mwingine asimamie mauzo nyakati za asubuhi na jion(hakikisha ni mtu wa karibu na mwaminifu)usipotoka Nenda katubu!