Napenda kuvaa

Napenda kuvaa

Mimi ni ke mwenye umri wa miaka 25 ,ni mrefu wastani,maji ya kunde/chocolate colour mwembamba wastani ,napenda kuvaa jamani,lakini nikinunua nguo nikianza tu kuivaa sikawii kuichoka,nguo zangu ni za mtumba najua nikienda mtumbani na elfu 50 narudi na nguo nyingi kwa sh 4000_6000 lakini dukani narudi na magauni mawili tu ya sh 25000,je wewe mwanamke mwenzangu au ata mwanaume maana kuna wanaume wako vizuri kwenye fashion wanaweza nishauri pia, je unapenda kununua nguo dukani/mtumbani na vipi utaratibu wako wa kununua nguo upoje? Nguo gani unapenda ziwe nyingi zaidi kati ya skirt,t shirt,na suruali? Wewe unapendelea kuvaa rangi gani zaidi kwaajili ya kupendeza na kuwavutia wengine,na unanunua nguo baada ya mda gani? Karibuni kucomment nipo kusoma comment zenu wapendwa wa jf......
Dizaining inakufelisha. Japo ni kawaida kuichoka nguo uliyoivaa mda mrefu.

Narudia tena "kwenye swala la kudizain mavazi unafeli na ndyo maana unazichoka haraka" lakin pia nguo za mtumba hasa hzi za bei ya barafu huwa zinawahi sana kuchakaa. Jimeki hata ifike 300k ununue kitu cha kueleweka hata kama ni kidogo.
 
Ila binafsi mi Bora nivae special coz siku kadhaa zishafubaa natupa...kiuhalisia unatakiwa ujipende bhana sio kuvaa manguo mpaka watu wanakuzoea wanajua mtu fulani anavaa nguo fulani..

Sioni kama Kuna maana ya kuwa na manguo kibao eti kisa og ambayo huwezi kuvaa mda mrefu umerundika tu ...mi viatu ndo siwezi kuvaa midosho lazima kiwe og mashati makali ule mtumba ulio classic ila fulana ya mtumba siwezi kabisa unakuta limkono lishatanuka haya swagga yaani kola ishakuwa kubwa ...better ninunue fulani 15k nikivaa miezi miwili sina time nayo sio kesi hela si napata bhana kwa nn nivae mamitumba.

Better kuwa stylist kwa wewe mwanamke nguo za mitumba za kike ni fire maana zipo model kibao nzuri tofauti na sisi...kingine binafsi naona magauni fulani marefu a typical baibui yako poa unakuta Bei ni 45k mazuri sana natumai mnayapenda coz yanapendza hata kiofsi vipo visuti vya kike hata 50k vya kishua ivi vya special naona ni vizuri kwenu kuliko majeans yakuchanika hayanaga mzuka kwanza Bei chee.
 
Utakuja tu kuacha

Nguo nyingi Za chini Za Mtumba ukishafika nyumbani inapoteza thamani

Unajikuta unajaza matakataka kabatini

Tenga bajeti Nenda Karume Jumanne/Ijumaa asubuhi wanafungua nguo nzuri

Unapoint , Kama Gauni ni kuanzia 10,000-25,000 inategemea na Quality

Za Dukani nanunua wale wanaleta Chamboo,
Pia naagiza SA Gauni zangu Za kupendezea

Nguo chache unazoweza kuvaa, siyo unatoka unashusha kabati zima huoni cha kuvaa
 
Utakuja tu kuacha

Nguo nyingi Za chini Za Mtumba ukishafika nyumbani inapoteza thamani

Unajikuta unajaza matakataka kabatini

Tenga bajeti Nenda Karume Jumanne/Ijumaa asubuhi wanafungua nguo nzuri

Unapoint , Kama Gauni ni kuanzia 10,000-25,000 inategemea na Quality

Za Dukani nanunua wale wanaleta Chamboo,
Pia naagiza SA Gauni zangu Za kupendezea

Nguo chache unazoweza kuvaa, siyo unatoka unashusha kabati zima huoni cha kuvaa
Izo za karume ni mtumba au
 
Back
Top Bottom