Napendekeza kituo kikuu cha Treni Mwanza kiitwe UMUGHAKA MWANZA STATION

Napendekeza kituo kikuu cha Treni Mwanza kiitwe UMUGHAKA MWANZA STATION

Nsikuchoshe na Usinchoshe, Tusichoshane!


Hili ni pendekezo Kwa viongozi wa Serikali,najua wengi wenu mko humu na mtapitia huu Uzi.


Sababu za Kituo hicho Kipya kitakachokuwa kizuri kupita maelezo kupewa jina la UMUGHAKA ni zifuatazo:-

1. UMUGHAKA ni Jasiri,hivyo kituo hicho kitakachojengwa Mwanza,kitakuwa ni Ishara ya Ujasiri ya watu kutoka Kanda ya Ziwa.

2. UMUGHAKA ni muelewa wa mambo,kituo hicho kitakuwa ni Ishara ya uelewa wa mambo mengi ya watu kutoka Kanda ya ziwa.

3. UMUGHAKA ni Jeuri,Kituo hicho kitakuwa Ishara ya ujeuri ya watu kutoka Kanda ya ziwa

4. UMUGHAKA ni shababi na rijali,Kituo hicho kitakuwa nembo ya wanaume mashababi na marijali kutoka Kanda ya ziwa

5. UMUGHAKA ni Msomi,Kituo hicho kitakuwa ni nembo ya wasomi wote kutoka Kanda ya ziwa

6. UMUGHAKA amejengeka kimisuli,Kituo hicho kitakuwa nembo ya wanaume wote kutoka Kanda ya ziwa waliojengeka kimisuli

7. UMUGHAKA hachagui kazi na ni mpambanaji,Kituo hicho kitakuwa nembo ya watu wote walio wapambanaji na wasiochagua kazi

8. UMUGHAKA ni mtembeza mianzi mzuri mno,Kituo hicho kitakuwa nembo ya wanaume wote wanatembeza mianzi ya kufa mtu Kwa wenzi wao

9. UMUGHAKA ni dereva bodaboda (Afisa ushafirishaji),Kituo hicho kitakuwa nembo ya madereva bodaboda (Afisa Ushafirishaji) nchi nzima

10. UMUGHAKA anampenda na kumuabudu Mungu aliyeziumba mbingu na nchi,Kituo hicho kitakuwa nembo ya watu wote wanaomuabudu Mungu (Allah),mtu kama Kiranga na ndugu zake tutawakaribisha Kwa mikono yote miwili kwasababu hatuta bagua mtu!


Mheshimiwa Dkt. Gwajima D nipigie chapuo huko kwenye baraza la mawaziri mama!

God bless y'all
Ni kama mimi ninavyotaka mji wa kiserikali Mtumba uache kuitwa Magufuli! Sababu zangu ni kama hizi! Na pale Dar pia stendi za Mabasi na Treni ziitwe jina la Kizaramo!
 
Back
Top Bottom