Napendekeza kufutwa kwa somo la ‘Slavery’ kwenye mitaala ya ufundishaji historia nchini

Napendekeza kufutwa kwa somo la ‘Slavery’ kwenye mitaala ya ufundishaji historia nchini

mzungu aliweza kuwakamata mababu zangu na kuwauza kama mbuzi kilinifanya nijione binadamu wa daraja la pili hapa duniani, inauma sana ila ukweli ndio huo
Hivi ni mzungu tu?

Mbona sivyo kwa Tanganyika?

Kwani Tiptip alikuwa mzungu au mwarabu?

Maana inajulikana, Tiptip na Waarabu wenzake wakiwa na magobole, walikuwa wanawinda na kukamata wenyeji kama digidigi kule Kigoma, Tabora, Dodoma, nk na kuwafunga minyororo, kuwapeleka hadi Bagamoyo, na kuwavusha hadi Zanzibar kwenye mnada wa watumwa.

Huko mnadani, walikuwa wakiuzia waarabu wenzao kwa ajili ya kusafirisha kwenda kuuza Uarabuni na Ulaya!

Yawezekana kwingineko Afrika mchakato ulikuwa tofauti
 
Hakuna SoMo la slavery mdau, badala yake Kuna mada tu inayohusu slavery. Somo ni historia!
 
Eti topic kiswahili chake Ni SoMo? Hivi vijana wa siku hizi vipi? Topic kiswahili chake Ni mada , jamani? Rudieni mitihani.
 
Duh, wewe Ni kilaza kabisa. Somo litabakia kuww historia, mada slavery.
 
Acha wafundishwe kwasababu slavery was a choice kwa WAAFRIKA na ndyo maana walichukuliwa na kuuzwa kama mbuzi.

Lazima watoto wafundishwe ili wajue mzungu na mwarabu ni watu wa aina gani.

Lazima wafundishwe ili wajue kuwa katika maisha inatakiwa kusimama imara katika umoja ili kuweza kumshinda adui.

Lazima wafundishwe ili wajue akili za hawa baadhi ya WAAFRIKA ambao walishiriki kuuza na kuwasaliti wenzao kuwa wapo hadi leo.

Watu wanatumikiswa Dubai na Saudi Arabia kama watumwa in the name of housemaid.

NASEMA ACHA WAFUNDISHWE
 
Pendekezo hilo nalitoa kwa sababu kuu tatu.

1.) Kitendo tu cha mimi kujua kwamba mzungu aliweza kuwakamata mababu zangu na kuwauza kama mbuzi kilinifanya nijione binadamu wa daraja la pili hapa duniani, inauma sana ila ukweli ndio huo; kwamba mzungu ni daraja la kwanza, ila sisi daraja la pili kama si la mwisho, naapa, kama nisingefundishwa haya, nisingeweza kupata mawazo hayo kamwe! Japo sasa nimekua na sina hata mawazo hayo, ila chini kwa chini kuna kitu nimeshaharibiwa na somo hilo.

2.) Si kila ukweli katika historia wenzetu huwafundisha watoto wao, huwa wanachagua, ikiwezekana hata kuedit historia ili kuwalinda kisaikolojia. Mfano wale Archeologists wa Kizungu walipogundua kwamba Mapharaoh wa Misri walikuwa ni watu weusi, na waliweza kuwafanya watumwa watu weupe (wayahudi) , walibadilisha na kupindisha ukweli, hata movie zao, mapharaoh wote wanaonyeshwa kwamba ni weupe, wakati michoro yote kwenye kuta za pyramid zimaonyesha vinginevyo..., mifano ni mingi mno!

3.) Hii ya sababu ya tatu ndio inaniumiza sana, sitaki hata kuitaja.., au basi siitaji
Jisomee na fanya tafiti mwenyewe uijuwe Historia ya ukweli, usifate historia za mitaala ya shule za msingi na sekondari. Hizo zipo ku brainwash watu ambao hawatabahatika kuanza kujisomea wenyewe. Anza kwa kutafiti na kujisomea ni nini maana ya "Azania".
 
Pendekezo hilo nalitoa kwa sababu kuu tatu.

1.) Kitendo tu cha mimi kujua kwamba mzungu aliweza kuwakamata mababu zangu na kuwauza kama mbuzi kilinifanya nijione binadamu wa daraja la pili hapa duniani, inauma sana ila ukweli ndio huo; kwamba mzungu ni daraja la kwanza, ila sisi daraja la pili kama si la mwisho, naapa, kama nisingefundishwa haya, nisingeweza kupata mawazo hayo kamwe! Japo sasa nimekua na sina hata mawazo hayo, ila chini kwa chini kuna kitu nimeshaharibiwa na somo hilo.

2.) Si kila ukweli katika historia wenzetu huwafundisha watoto wao, huwa wanachagua, ikiwezekana hata kuedit historia ili kuwalinda kisaikolojia. Mfano wale Archeologists wa Kizungu walipogundua kwamba Mapharaoh wa Misri walikuwa ni watu weusi, na waliweza kuwafanya watumwa watu weupe (wayahudi) , walibadilisha na kupindisha ukweli, hata movie zao, mapharaoh wote wanaonyeshwa kwamba ni weupe, wakati michoro yote kwenye kuta za pyramid zimaonyesha vinginevyo..., mifano ni mingi mno!

3.) Hii ya sababu ya tatu ndio inaniumiza sana, sitaki hata kuitaja.., au basi siitaji
"Ni SOMO LA SLAVERY" kwa Maana ya (Slavery subject)au ni topic ya slavery yaani (MADA YA UTUMWA?)
 
Muafrika hakua na hakumtambua mungu hadi wageni walipokuja.............bulushit......historia yetu kabla ya hawa wageni kuja ni kama hakuna kitu tunachoambiwa ni kama maisha yetu yalianza walipoanza kuja hawa wageni
Tulishindwa hifadhi historia zetu
 
Jisomee na fanya tafiti mwenyewe uijuwe Historia ya ukweli, usifate historia za mitaala ya shule za msingi na sekondari. Hizo zipo ku braiwsh watu ambao hawatabahatika kuanza kujisomea wenyewe. Anza kwa kwa kutafiti na kujisomea ni nini maana ya "Azania".

H
True mengi ni uongo tuliosoma.
Mfano kitabu cha Walter rodney ni uongo mtupu na chuki tu zaidi dhidi ya race zingine Ili kuhalalisha kushindwa kwetu
 
Watu weusi tumekua tukisingizia utumwa katika failure zetu za kimaendeleo. Hopeless kabisa
 
Waafrika historia yetu tumeandikiwa na waliotutawala so imechakachuliwa sanaa..swali ni wap tutapata historia yetu waafrika og??where!
 
Waafrika historia yetu tumeandikiwa na waliotutawala so imechakachuliwa sanaa..swali ni wap tutapata historia yetu waafrika og??where!
Historia hata ya Watumwa waliouzwa marekani ilifutwa yote! Eti mtu mweusi toka Africa anaitwa Michael Jackson, hiyo Jackson imetoka wapi?! Mara Mike Tyson, hiyo ‘Tyson’ ya wapi? Mara Robert Kelly, Africa kuna ‘Kelly’?! Kunta Kinte ilikuwa kidogo tu wamuuwe kwa kutokubali jina jipya la kitumwa

 
BIASHARA YA WATUMWA
Kwa kipindi kirefu ambacho hakijulikani mwanzo wake; Waarabu waliendesha biashara hii haramu Tanganyika. Walishambulia vijiji vya Waafrika na kuteka watu na kuwafanya watumwa; ambao waliwauza Uarabuni, Zanzibar na nchi nyingine za nje. Kwa Zanzibar walitumika katika mashamba ya Karafuu na minazi. Lakini wengi walisafiriswa mbali na pwani ya Tanganyika. Walionunuliwa na Wazungu walipelekwa Amerika. Lakini Wazungu hawakununua watumwa wengi kutoka Afrika Mashariki. Wazungu walinunua watumwa wengi kutoka Afrika ya Magharibi.
Waarabu waliokuwa wanafanya biashara ya utumwa walikuwa katili kupindukia. Watumwa walipitia katika mateso yasiyo kifani. Walitendewa, ukatili wa kinyama, usio wa kiutu wala ubinadamu. Watumwa walipigwa, waliuawa. Walifungwa mikatale. Walitembea kwa miguu mwendo mrefu wakiwa wamefungwa minyororo miguuni au shingoni; huku wakibeba meno ya tembo na mizigo mingine na wakipigwa kwa kutembea polepole. Walitembea kwa miguu toka Ujiji, Kigoma mpaka Bagamoyo. Wagonjwa na dhaifu waliachwa maporini wafe peke yao au waliwe na wanyama.......

 
 
Back
Top Bottom