Napinga ACT-Wazalendo kushiriki kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) huko Zanzibar

Napinga ACT-Wazalendo kushiriki kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) huko Zanzibar

Unapinga kama nani wewe? Nyinyi ndio munatumiliwa na CCM kuleta mawazo mbadala hapa jf kuwachanganya watu ili munufaike hizo buku 7., issue ya maalim seif anasema wao wamepata ridhaa kutoka kwa wananchi wao sasa ulitaka nini tena na wananchi ndio mtaji kwa wanasiasa? Chama kinaangalia option nyengine mbadala 2025 vipi wataikabili ccm labda na wao wakiwa madarakani. mara hii ndo mushaona walifanya watakavyo hakuna kura hata moja iliyotoka kituoni matokeo yote yamepikwa.
Masahihisho : Mimi siyo ccm na sijawahi kuwa kwenye kundi la buku 7 fc
 
Unaweza kuta Zitto kazidiwa nguvu na wakina Maalim.

Amandla...
Siyo kama ''unaweza kukuta'' bali haya ni maamuzi ya Maalim Seif. Wengine wametumika kupiga rubber stamp tu. Nadhani Maalim ameona kuwa mwaka 2025 hatakuwa na nguvu za kugombea tena akaona akubali tu kuchukuwa ''pension'' yake ya kisiasa. Tatizo kubwa (kwa mpinzani yoyote Tanzania) ni kuwa wananchi hawajitokeza inapopaswa, kwa ajili ya woga. Na siku hizi kutegemea tu wahisani haisadii kwani wahisani hawawezi ku-act inavyotakiwa bila wananchi kukinukisha. Mfano ni Kenya. Kama wasingejitokeza ule uchaguzi enzi Mwai Kibaki alivyochakachua mpaka leo pengine wasingekuwa na katiba mpya. Maalim atakuwa amepiga hesabu na kuona mwaka 2015 walivyogeuza matokeo bila aibu na hakuna kilichofanyika. Akaona hata kipindi hiki kama asikubali angalau afaidi basi hakuna siku atakuja kupata tena.
 
Naomba kwanza niweke wazi kabisa kwamba mimi si mwanachama wa chama cha ACT WAZALENDO na pia si mfuasi wake na wala siingilii msimamo wa viongozi wa chama hicho kama wao wenyewe walivyoamua , bali ifahamike kwamba mimi kama Mtanzania wa kuzaliwa ninayo haki ya kujadili makandokando yoyote yanayojitokeza ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kuwekewa mipaka na yeyote kwa sababu zozote zile.

Uchaguzi wa Zanzibar kama ulivyokuwa uchaguzi wa Jamhuri ya Muungano ulighubikwa na uchafu wa kila aina , watu wamedhulumiwa ushindi , wametekwa , wameteswa na kuuawa, viongozi kadhaa wa ACT WAZALENDO akiwemo Maalim Seif, Ismail Jussa na Mazrui wamekamatwa na kuteswa vibaya sana, huku viongozi wengine kama Khamis Bakari wakifariki baada ya kujeruhiwa kwa risasi , nyumba kadhaa kisiwani Pemba zimeteketea kwa kupigwa mabomu huku vikongwe wakiumizwa bila hatia yoyote.

Walioyafanya haya wapo na wanafahamika na ndio hao hao wanaotaka ushirikiano kwenye serikali na ACT inakubali ? sababu ya kukubali ushirika huu ni zipi hasa? maana ukikubali ujinga huu ni kwamba umeyakubali mauaji ya wazanzibar na mateso yao kwamba yalikuwa halali , nani atakuamini tena?

Kwa vile mimi ni Mcha Mungu , Mpenda haki na mpinga uonevu , natangaza hadharani kupinga ACT kuingia kwenye SUK ili kujiepusha na dhambi ya kujitakia ya kushabikia mateso na mauaji ya kisiasa ya raia wasio na hatia yoyote , Nawatakia kila la heri na fanaka watakaoshiriki kwenye Uharamia huo

Mungu ibariki Zanzibar.

Nakala: Juma Duni Haji

Mkuu. Wewe Ni mrs Keyboard. Huna lolote. Hujui hata wananchi wtz wanataka nini. Unawaza zaidi uhalali wako wa kuandika hapa kuliko maisha ya mtz. Kwako hata kwetu upareni wakipata barabara huwezi sifia ila ikibomoka utaandika. Pole sana.
 
Naomba kwanza niweke wazi kabisa kwamba mimi si mwanachama wa chama cha ACT WAZALENDO na pia si mfuasi wake na wala siingilii msimamo wa viongozi wa chama hicho kama wao wenyewe walivyoamua , bali ifahamike kwamba mimi kama Mtanzania wa kuzaliwa ninayo haki ya kujadili makandokando yoyote yanayojitokeza ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kuwekewa mipaka na yeyote kwa sababu zozote zile.
Loser!
Hakuna wa kukusikiliza,hata chadema wako watawasamehe wabunge wake 19
Ninyi ni wasanii tu mnakataza watu wasuse lakini mna mbunge na madiwani waliotokana na chaguzi hizo hizo lakini mmewauhusu waape.
 
Mh Mambo ya siasa bhana.Sefu amegudua kuwa mda unampa kono sasa hakuna namna.
 
Dhambi kuu iliyotendeka ni kuwaambia Wazanzibar waingie mtaani kuandamana baada ya wizi wa kura uliokithiri. Watu wakateswa na wengine kuuawa, ushahidi upo.

Baada ya muda unakuja na kukana kuwa yaliyofanywa na dola si haramu. Hivyo, tunaingia kwenye SUK na kuanza kuiponya Zanzibar.

Huu ni uhalifu kama uhalifu mwingine. Watu walidhurumiwa hali zao za kikatiba, pia ikiwemo haki ya uhai.

Mungu ni Mkuu na mwenye maajabu sana. Hakuacha hili lipite bure. Na laana hii itapita na wengi.

Naomba wajiandae kisaikolojia kuanzia sasa.
 
Dhambi kuu iliyotendeka ni kuwaambia Wazanzibar waingie mtaani kuandamana baada ya wizi wa kura uliokithiri. Watu wakateswa na wengine kuuawa, ushahidi upo.

Baada ya muda unakuja na kukana kuwa yaliyofanywa na dola si haramu. Hivyo, tunaingia kwenye SUK na kuanza kuiponya Zanzibar.

Huu ni uhalifu kama uhalifu mwingine. Watu walidhurumiwa hali zao za kikatiba, pia ikiwemo haki ya uhai.

Mungu ni Mkuu na mwenye maajabu sana. Hakuacha hili lipite bure. Na laana hii itapita na wengi.

Naomba wajiandae kisaikolojia kuanzia sasa.
Yaliyopita yamepita. Isitoshe hata Magulifu aliwahi kumshangaa Dr Shein kwa kuendelea kugharamia matibabu ya Seif wakati Seif analeta upinzani kwenye serikali, cha ajabu mwisho wa siku wote wamekutana tena Chato.
 
Mwenyezi Mungu Mkubwa Mkuu. Huyu jamaa nilipoteza imani naye tangu alipoanza usaliti ndani ya Chadema. Pamoja na kuwa aliomba samahani hapa jamvini JF kwa kuanzisha uzi lakini baadaye akataka ufutwe na ukafutwa kwa sababu aliulizwa maswali mengi kuhusu hiyo samahani yake FEKI aliyoshindwa kuyajibu. Once A TRAITOR ALWAYS …..

Hakika Zitto kiukweli hayupo kabisa
 
Tulionya Mapema sana , lakini tulipuuzwa , Sasa leo ACT mnamlilia nani ?
 
Back
Top Bottom