Napinga Dkt. Harrison Mwakyembe kuwa Mwenyekiti wa Tume ya kuchunguza kufeli kwa wanafunzi wengi wa Law School

Napinga Dkt. Harrison Mwakyembe kuwa Mwenyekiti wa Tume ya kuchunguza kufeli kwa wanafunzi wengi wa Law School

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Mwenyekiti wa Tume ya Kuchunguza masuala ya Law school, ikiwemo wanafunzi wengi kufeli mitihani, anapaswa kuwa mtu Muungwana, Mtulivu, Msikivu na asiye na makuu, anapaswa kuwa mkweli, Mwakyembe hana sifa hizi.

Napinga uteuzi wa Harisson Mwakyembe kuwa Mwenyekiti wa Tume hii kwa vile Haaminiki, si mkweli na ni mpenda sifa.

Kwa mfano, alipokuwa Mwenyekiti wa Tume ya bunge kuchunguza Richmond, katika Taarifa yake aliyoisoma bungeni ALIFICHA BAADHI YA TAARIFA ILI KUOKOA SERIKALI, maana yake ni kwamba alificha taarifa za Mhusika Mkuu wa Jambo lile na kuangushia jumba bovu wasiohusika, leo huyu awezaje kuaminika na kukabidhiwa tume nyingine? JE, SAFARI HII HATOFICHA TAARIFA ILI KUIOKOA SERIKALI?

Mwakyembe akiwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Kyela kupitia CCM, aliwaahidi watu wa Jimbo lake kwamba AMEPATA SOKO LA UHAKIKA LA MCHELE WAO NCHINI MAREKANI (ikumbukwe kwamba mchele wa Kyela ndio unaoongoza kwa utamu duniani)

Lakini hadi anang'olewa kwenye ubunge hakuwahi kusaidia hata kilo 10 za mchele wa Kyela kuuzwa Marekani, Mtu kama huyu hastahili kuaminiwa kuongoza tume yoyote ile.

UNAPODANGANYA NYUMBANI KWENU HUWEZI KUAMINIKA UGENINI.

Harrison Mwakyembe ni mtu aliyejaa dharau kubwa sana , huyu hawezi kuwatendea haki watu wenye digrii moja wanaopigania haki yao ya matokeo.

ALIWAHI KUKATAA MASWALI KWAO KYELA kwa kisingizio kwamba wanaomhoji ni Darasa la 7, wakati yeye anamiliki digrii 4 na kwamba watu wasio na elimu wanachopaswa kumhoji ni kuhusu kama hawana hela mifukoni mwao na labda awasaidie. Huyu hafai kuongoza Tume ya kufuatilia haki popote duniani.

Tunamuomba Waziri wa Sheria ATENGUE HARAKA UTEUZI WAKE.

NITASEMA KWELI DAIMA FITNA KWANGU MWIKO.
 
Tume imejaa watumishi wa taasisi za serikali ambao wanawajibika kwa serikali ambayo inaimiliki pia taasisi ya LST chini ya Wizara ya Sheria. Kwa kweli, tunampongeza waziri Ndumbaro kwa kuchukua hatua lakini tunaomba aongeze wajumbe kwenye hiyo tume, aweke wanasheria wa kujitegemea, wajumbe wa bodi nyingine za kitaaluma, waandishi wa habari, wanafunzi waliofeli, na hata mwanafunzi aliyepo darasani sasa.
 
Matokeo ya Law School yako sawa mengine ni mihemuko tu!
Wanafunzi wengi ni weupe mno vichwani na wanakariri vitu vya kujibia mitihani tu basi!
Kwanza hata huku mitaani kuna mawakili huwezi hata amini kama wamepita Law School,ni " weupe" mno vichwani na hawasomi !
Kazi zao ni copy, paste na edit basi!
Kiingereza ndo wengi hawajui kabisa!
Msimchoshe Dr.Mwakyembe na kamati zisizo na misingi!
Chukueni Wanafunzi 30 ( randomly) then wapigwe oral interview ( Live on TV) mtaona Tanzania ilivyo na majanga mengi na sote tutaishia kuwapongeza hao Lecturers wa Law School wasiotaka ujinga ujinga katika fani ya Sheria.
 
Mwakyembe huyu huyu aliuemleta Tapeli wa Marekani Robert Shumake, aliyeahidi kuleta treni za kisasa za mjini (Metro)!! Hapana Mwakyembe hafai labda Damas Ndumbaro analipa fadhila tu kwa mwalimu wake wa zamani.
Screenshot_20221012-173031.png
 
Mwaisa hana credibility.

Hata hivyo lengo la hizi tume za uchunguzi katika mifumo ya serikali sio kupata majibu au ukweli uliojificha.....

....bali ni kuzima mjadala kwa kuonesha kuwa serikali imechukua hatua.

Mnaibiwa ndugu wadanganyika.
Kama ile tume ya mauaji ya kijana wa madini yaliyofanyika ndani ya kituo cha polisi cha Mtwara, sijui kama ilitoa ripoti mpaka leo!!
 
BAVICHA mnadandia kila kitu yaan,
Kwa akili ndogo uliyonayo ni Bavicha! Hivi Mwakyembe ndio wa kumuweka hapo. Wako wanasheria Lukuki na wenye kuwa na ukweli lakini sio Mwakyembe! Ieleweke hivo!
 
Mwenyekiti wa Tume ya Kuchunguza masuala ya Law school, ikiwemo wanafunzi wengi kufeli mitihani, anapaswa kuwa mtu Muungwana, Mtulivu, Msikivu na asiye na makuu, anapaswa kuwa mkweli, Mwakyembe hana sifa hizi.

Napinga uteuzi wa Harisson Mwakyembe kuwa Mwenyekiti wa Tume hii kwa vile Haaminiki, si mkweli na ni mpenda sifa.

Kwa mfano, alipokuwa Mwenyekiti wa Tume ya bunge kuchunguza Richmond, katika Taarifa yake aliyoisoma bungeni ALIFICHA BAADHI YA TAARIFA ILI KUOKOA SERIKALI, maana yake ni kwamba alificha taarifa za Mhusika Mkuu wa Jambo lile na kuangushia jumba bovu wasiohusika, leo huyu awezaje kuaminika na kukabidhiwa tume nyingine? JE, SAFARI HII HATOFICHA TAARIFA ILI KUIOKOA SERIKALI?

Mwakyembe akiwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Kyela kupitia CCM, aliwaahidi watu wa Jimbo lake kwamba AMEPATA SOKO LA UHAKIKA LA MCHELE WAO NCHINI MAREKANI (ikumbukwe kwamba mchele wa Kyela ndio unaoongoza kwa utamu duniani)

Lakini hadi anang'olewa kwenye ubunge hakuwahi kusaidia hata kilo 10 za mchele wa Kyela kuuzwa Marekani, Mtu kama huyu hastahili kuaminiwa kuongoza tume yoyote ile.

UNAPODANGANYA NYUMBANI KWENU HUWEZI KUAMINIKA UGENINI.

Harrison Mwakyembe ni mtu aliyejaa dharau kubwa sana , huyu hawezi kuwatendea haki watu wenye digrii moja wanaopigania haki yao ya matokeo.

ALIWAHI KUKATAA MASWALI KWAO KYELA kwa kisingizio kwamba wanaomhoji ni Darasa la 7, wakati yeye anamiliki digrii 4 na kwamba watu wasio na elimu wanachopaswa kumhoji ni kuhusu kama hawana hela mifukoni mwao na labda awasaidie. Huyu hafai kuongoza Tume ya kufuatilia haki popote duniani.

Tunamuomba Waziri wa Sheria ATENGUE HARAKA UTEUZI WAKE.

NITASEMA KWELI DAIMA FITNA KWANGU MWIKO.
Waathirik wa Law school wamkatae.
 
Back
Top Bottom