Napinga kutumbuliwa kwa Mrisho Gambo

Napinga kutumbuliwa kwa Mrisho Gambo

Gambo kama kiongozi, moja ya majukumu yake ni kutatua migogoro (conflict resolution) ikiwamo ile anayohusika yeye. Kushindwa kutatua mgogoro wake na "watumishi" wake ni moja ya kiashiria kuwa uongozi ulimshinda.

Tatizo zaidi ni kuwa mgogoro wao ulikuwa kikwazo cha maendeleo Arusha mjini. Maamuzi hayafanyiki kwa kuwa wanatunishiana misuli na wanashindwa ku-kompromaiz. Si kwamba ofisi/taasisi zote watu huelewana bali yanapokuja masuala ya kazi tofauti sharti zikae kando.

Uamuzi wa rais ni sahihi kabisa (kwa assumption kuwa sababu kubwa ni hiyo). Japo inasikitisha kuwa utenguzi umekuja wakati mbaya kwa watenguliwa hasa Gambo. Awe positive ajisahihishe, muda bado anao ikiwa ana ndoto kwenye siasa.

Hata Simbachawene, Mwigulu, Kicheere, nk walianguka kisha wakainuka.
 
Mheshiwa mkuu wa Nchi, umemtumbua Mrisho Gambo kimakosa sana.
Na hapa ninaona kama ameonewa sana.

Gambo alikuwa mkuu wa mkoa. Mkuu wa mkoa ndio top say ya mkoa wa Arusha, iweje Mkurugenzi na DC wasimheshimu?

Tofauti zao kubwa ni za kimadaraka. CED na DC ndio walistahili kumsikiliza Mkuu wao wa mkoa na kuheshimu yale wanayokubaliana.

Iweje mkuu wa Mkoa asimamie nafasi yake then hawa wa chini yake wasimheshimu?? Wamdharau??
Tunajua Mrisho ni mchapa kazi mzuri.

Haya maamuzi sio sahihi.

Gambo alikuwa anasimamia uongozi wake tu na kuheshimiwa.
Nani kakuambia kwamba kilicho mtumbulisha ni ugomvi kati yake na DC na Mkurugenzi?

Dr. Bashiru Ally Kakurwa amenukuliwa akisema Arusha kuna tatizo na tatizo ni Mkuu wa Mkoa huo. Aidha Mwenezi Ndugu Komredi huyu Polepole amenukuliwa akisema pia Arusha ipo shida na yeye alidokeza kwamba tatizo ni kutoridhika na nafasi walizonazo na kuutaka Ubunge. Hapa Komredi Polepole hakumtaja kwa cheo bali viashiria.

Mtoto huyu wa Muuza uji wa pale soko la mchikichini (Karume mliokuja hivi karibuni mjini) na yule aliyeacha shule na kutamani kuwa fundi magari kisha akaahirisha na kurudi shule ameonekana akibebwa na kugombewa na wana Arusha kuonyesha eti uongozi uliotukuka kwa mkoa (kisiasa hili Jambo huwa ni kaburi rejea ya Ndugu Waziri Mkuu Ngoyayi Lowassa 2015).

Kama kuna mtu anaweza kufanyiea hivyo kwa haki bila shaka basi ni Mkuu wa Ikulu ya CHANZIGE Pwani (Kisarawe) Bibie Jokate Mwegelo. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dr. Mghwira.
 
Nani kakuambia kwamba kilicho mtumbulisha ni ugomvi kati yake na DC na Mkurugenzi?

Dr. Bashiru Ally Kakurwa amenukuliwa akisema Arusha kuna tatizo na tatizo ni Mkuu wa Mkoa huo. Aidha Mwenezi Ndugu Komredi huyu Polepole amenukuliwa akisema pia Arusha ipo shida na yeye alidokeza kwamba tatizo ni kutoridhika na nafasi walizonazo na kuutaka Ubunge. Hapa Komredi Polepole hakumtaja kwa cheo bali viashiria.

Mtoto huyu wa Muuza uji wa pale soko la mchikichini (Karume mliokuja hivi karibuni mjini) na yule aliyeacha shule na kutamani kuwa fundi magari kisha akaahirisha na kurudi shule ameonekana akibebwa na kugombewa na wana Arusha kuonyesha eti uongozi uliotukuka kwa mkoa (kisiasa hili Jambo huwa ni kaburi rejea ya Ndugu Waziri Mkuu Ngoyayi Lowassa 2015).

Kama kuna mtu anaweza kufanyiea hivyo kwa haki bila shaka basi ni Mkuu wa Ikulu ya CHANZIGE Pwani (Kisarawe) Bibie Jokate Mwegelo. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dr. Mghwira.
Confused [emoji53]
 
Tumeshamyumbua hatubadili maamuzi
Mheshiwa mkuu wa Nchi, umemtumbua Mrisho Gambo kimakosa sana.
Na hapa ninaona kama ameonewa sana.

Gambo alikuwa mkuu wa mkoa. Mkuu wa mkoa ndio top say ya mkoa wa Arusha, iweje Mkurugenzi na DC wasimheshimu?

Tofauti zao kubwa ni za kimadaraka. CED na DC ndio walistahili kumsikiliza Mkuu wao wa mkoa na kuheshimu yale wanayokubaliana.

Iweje mkuu wa Mkoa asimamie nafasi yake then hawa wa chini yake wasimheshimu?? Wamdharau??
Tunajua Mrisho ni mchapa kazi mzuri.

Haya maamuzi sio sahihi.

Gambo alikuwa anasimamia uongozi wake tu na kuheshimiwa.
 
Week hii aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mheshimiwa Mrisho Gambo,DC Arusha Gabriel na City Director walitumbuliwa katika vyadhifa zao.Nisingependa kuwazungumzia DC na Mkurugenzi kwakuwa ni wazi watarejea katika kazi zao za mwanzo usiniulize ni kazi gani ni wajibu wako kupekenyua kama utapenda.

Mwathirika Mkuu katika kadhia hii ni Mrisho Gambo yeye itabidi arejee katika corridor za UVCCM na kujifunza upya namna ya kupiga fitna hili nafasi ikijitokezea akumbukwe tena.

Mheshimiwa Mrisho Gambo amekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa miaka 4 mfululuzo.Kazi yake kubwa ilikuwa kuvunja nguvu ya upinzani ndani ya mkoa wa Arusha.Kazi hii aliifanya kwa uadilifu mkubwa sana.Alisimamia na kuratibu manunuzi ya madiwani,viongozi wa upinzani na wabunge.Kwa hakika kazi hii ilimpatia jeuri kubwa na binafsi aliamini hakuna wa kumgusa kwasababu hakuna mkuu wa Mkoa aliyefikia viwango vyake.Jeuri na dharau aliipeleka hadi kwa viongozi wenzake ndani ya CCM na watendaji wakuu wote wa mkoa wa Arusha.

Ikiwa kazi aliyotumwa aliifanya vizuri haya mambo madogo madogo yalipaswa kufumbiwa macho.Mbona RC Makonda ni zaidi ya Gambo lakini haguswi ?.Ebu tumwache Gambo wa watu na ikiwezekana tumwachie nafasi ya kugombea ubunge Arusha kazi tuliyomtuma si ndogo turejeshe fadhila.
 
Haha,tena usikute,hata hao dc na mkurugenzi walitumwa na wabaya wake kumchokonoa makusudi ajae upepo,,
Ndo maana hakuna kitu kizuri kama self control,,usipoweza control emotion zako,unaweza kuharibu ,
Vilevile gambo mkorofi yule by nature
 
Week hii aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mheshimiwa Mrisho Gambo,DC Arusha Gabriel na City Director walitumbuliwa katika vyadhifa zao.Nisingependa kuwazungumzia DC na Mkurugenzi kwakuwa ni wazi watarejea katika kazi zao za mwanzo usiniulize ni kazi gani ni wajibu wako kupekenyua kama utapenda.

Mwathirika Mkuu katika kadhia hii ni Mrisho Gambo yeye itabidi arejee katika corridor za UVCCM na kujifunza upya namna ya kupiga fitna hili nafasi ikijitokezea akumbukwe tena.

Mheshimiwa Mrisho Gambo amekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha kwa miaka 4 mfululuzo.Kazi yake kubwa ilikuwa kuvunja nguvu ya upinzani ndani ya mkoa wa Arusha.Kazi hii aliifanya kwa uadilifu mkubwa sana.Alisimamia na kuratibu manunuzi ya madiwani,viongozi wa upinzani na wabunge.Kwa hakika kazi hii ilimpatia jeuri kubwa na binafsi aliamini hakuna wa kumgusa kwasababu hakuna mkuu wa Mkoa aliyefikia viwango vyake.Jeuri na dharau aliipeleka hadi kwa viongozi wenzake ndani ya CCM na watendaji wakuu wote wa mkoa wa Arusha.

Ikiwa kazi aliyotumwa aliifanya vizuri haya mambo madogo madogo yalipaswa kufumbiwa macho.Mbona RC Makonda ni zaidi ya Gambo lakini haguswi ?.Ebu tumwache Gambo wa watu na ikiwezekana tumwachie nafasi ya kugombea ubunge Arusha kazi tuliyomtuma si ndogo turejeshe fadhila.
Mwenye maamuzi ya kuteua na kutengua hawajibiki kutoa sababu za maamuzi yake.Ukilikumbuka hilo utakuwa na amani sana.
 
Naanza kuamini nchi hii imejaa vidikteta. Yaani kama tunadhani ni rahisi kukomesha udikteta nchi hii tunajidanganya. Kuna watu udikteta unawafaidisha hadi wako tayari kufanya lolote kuutetea. Kwa taarifa yako;

1. Kuwa mkuu wa mkoa hakumaanishi wewe ni mwamuzi wa mwisho kwa kila kitu ndani ya mkoa. Mfano, Mkuu wa mkoa hana maamuzi juu ya mgonjwa achomwe sindano au apewe vidonge. Vivyo hivyo hana maamuzi ya mwisho ya kubadilisha ramani ya jengo la serikali kwa sababu ya matakwa binafsi, hapo akijitokeza mtu akagoma kubadilisha ramani na akatoa sababu za kitaalamu mtaona anadharauliwa lakini mtaalamu atakuwa sahihi.

2. Kila mtumishi kwenye nafasi yake ana mamlaka kamili. DED ana mamlaka kamili katika nafasi yake mfano, matumizi ya fedha za Halmashauri yaliyopitishwa na Baraza la Madiwani hayawezi kutenguliwa kiboya na Mkuu wa mkoa kisa tu yeye ni msemaji wa mwisho mkoani kwake.

3. Mkuu wa mkoa ana maamuzi kamili katika nafasi yake kwa kufuata Job description ya nafasi yake lakini maamuzi yake yapaswa kufuata ushauri bora wa wataalamu alionao na siyo matakwa binafsi. Ndo maana unaona Wakuu wa mikoa wenye kujua mipaka yao huoni wakigombana na wataalamu wao. Hata wanapochukua hatua husikii mtu alisema Mkuu wa mkoa kamwonea mtu.

4. Kuna msemo siku hizi vijana wanasema "SIMAMA KWENYE JINSIA YAKO". Mkuu wa mkoa anayejitambua anatakiwa kujua mipaka ya madaraka yake. Lakini ukikuta mkuu wa mkoa anataka kukagua ghala la silaha za Polisi au kuamuru mtuhumiwa fulani aachiwe kwa vile tu yeye ni Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama (KUU) mkoa, ujue huyo ni Bomu na muda wowote atalipua mkoa.

5. Mkuu wa mkoa au mkuu yeyote wa Idara hana hiari ya kudharau wa chini yake na kuwadhalilisha hadharani kwa vile tu yeye ni Mkuu. Kuheshimu walio chini yake ni miongoni mwa masharti ya uteuzi wake. Asipofanya hivyo sheria ya Mahusiano kazini inamtaka aidha ajiondoe au aondolewe.

6. Mkuu wa mkoa hapaswi kuwa mtu wa majungu na kufanyia kazi taarifa za kuokoteza. Ukiwa mkubwa kazini fanya maamuzi ambayo kila anayeona ajue una taarifa sahihi, majungu na umbea isiwe sehemu ya maamuzi yako kama Mkuu.

Kwa hayo hapo juu, Gambo kutumbuliwa pamoja na DED na DC Arusha ni kumheshimu tu, lakini alitakiwa aondoke peke yake ili liwe fundisho kwa wakuu wa mikoa na wilaya wanaofanya kazi kinyume cha miongozo ya nafasi zao.
Kumbe wametumbuliwa 3?
Anyway, kwa gambo namshukuru tu!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
kama maneno nilio yaona sehem ni kweli Gambo sio kiongozi ila ni magumashi tu ingawa tunajua anaenda gombea ubunge kama katolewa kwa mabaya jina halitarud kamt kuu
 
Mheshiwa mkuu wa Nchi, umemtumbua Mrisho Gambo kimakosa sana.
Na hapa ninaona kama ameonewa sana.

Gambo alikuwa mkuu wa mkoa. Mkuu wa mkoa ndio top say ya mkoa wa Arusha, iweje Mkurugenzi na DC wasimheshimu?

Tofauti zao kubwa ni za kimadaraka. CED na DC ndio walistahili kumsikiliza Mkuu wao wa mkoa na kuheshimu yale wanayokubaliana.

Iweje mkuu wa Mkoa asimamie nafasi yake then hawa wa chini yake wasimheshimu?? Wamdharau??
Tunajua Mrisho ni mchapa kazi mzuri.

Haya maamuzi sio sahihi.

Gambo alikuwa anasimamia uongozi wake tu na kuheshimiwa.
Top say ndio majitu gani hayo, na wewe ndio unafaa tukutumbue humu.

Unamuabudu mtu ambaye siku zote kazi yake kubwa ilikuwa ni kunyanyasa wapinzani, nenda kwake ukamsaidie kuomboleza au mwambieni naye ajiajiri kama walivyokuwa wanawaambia wengine kuwa wajiajiri. Very hopeless.
 
Back
Top Bottom