Napinga kutumbuliwa kwa Mrisho Gambo

CCM ya sasa Mdogo akimdharau mkubwa hawaangalii chanzo cha Tatizo wao ni kufukuza wote tu, hakuna heshima kwa aliye juu tena
 
Ni hulka yetu kushangilia anapotumbuliwa mtu.
Mtu akiachishwa kazi wanaofurahia huwa wengi.
Dalili nzuri za wivu.
CCM ya sasa kutokuwa na nidhamu kwa kiongozi wako wa juu ni sifa, mfano wale wadogo wamemdharau mkubwa wao cha ajabu wametolewa wote badala ya kuwadhibu wale wadogo kwanza. Utawala bora hakuna, busara haipo tena
 
Wewe ni Gambo. Acha kujitetea. Kwani hamna kazi nyinhine nje ya u RC???

NENDA UKAJIAJIRI! SIO NDIO LUGHA MNAYOTUAMBIAGA?? NJOO MTAANI TUBEBE ZEGE!
 
DEO ni afisa elimu wilaya. DED ndio mkurugenzi kakosea tu kidogo najua ulikuwa umeelewa.

Kuna jamaa angu anaitwa DEO Ni mwalimu kumbe anacheo kikubwa hivyoo.

Hicho cheo Cha DED ata nikipewa bure sikitaki nisije kufa buree.
 
Hivi itokee mkurugenzi wa jiji la Dsm na mkuu wa wilaya ilala wamdharau Daud Bashite kuna anayeamini makonda Bashite atatumbuliwa?
 
Wewe ni Gambo. Acha kujitetea. Kwani hamna kazi nyinhine nje ya u RC???

NENDA UKAJIAJIRI! SIO NDIO LUGHA MNAYOTUAMBIAGA?? NJOO MTAANI TUBEBE ZEGE!
Kujitetea nini? Kwani kama hakuna kazi ingine zaidi ya RC ndiyo wadogo wamdharau mkubwa wao? Kubeba zege sawa lakini CCM mnawafundisha nini wadogo kwa wakubwa zao? Wewe unaafiki dharau toka kwa wakuu wa wilaya kwa RC ? Wambie wakuu wa wilaya wamdharau Naibu Rais ndugu Daud Bashite waone moto wake.
 

Sugu kwenye mijadala Star TV, agenda 2020 aliwatambua ma RC wa siku za nyuma akiwamo Marehemu Abbas Kandoro (rip) kama watu waliokuwa na wingi wa busara. Siyo hawa wa siku hizi.

Naamini Sugu alikuwa sahihi sana tu.
 
Moja ya sifa ya kiongozi mzur ni kuwa na uwezo wa kusolve disputes.. so km yy alishindwa kusolve ugomvi wake na viongozi wenzake hastahili kupewa hizo sifa unazompa/ jipa...let him go hata sisi tunataka kazi bana, acha na wengine wapate shavu!
 
Sasa ukitaka mkuu wa mkoa atolewe mpinge mdharau ukiwa huko CCM hata kama wewe ni mwenyekiti wa kijijini ili mradi wewe ni CCM lazima atatumbuliwa haraka
 
Sugu kwenye mijadala Star TV, agenda 2020 aliwatambua ma RC wa siku za nyuma akiwamo Marehemu Abbas Kandoro (rip) kama watu waliokuwa na wingi wa busara. Siyo hawa wa siku hizi.

Naamini Sugu alikuwa sahihi sana tu.
Wapo DC wenye vioja mfano DC wa Hai au DC wa jimboni kwa Nasari
 
Wakuu wengi wa mikoa wengi wanavumilia shida kwa hofu ya kutumbuliwa lakini chini chini wananyanyasika sana na wakurugenzi DC wale ndugu marafiki wa mtukufu na hasa rafiki wa Daud Bashite.
 
DC au mkurugenzi akiwa rafiki au ndugu wa mtukufu ni vigumu kupokea maagizo ya RC na hapo ndipo utawala bora umevurugwa sasa.
 
Wapo DC wenye vioja mfano DC wa Hai au DC wa jimboni kwa Nasari

Wapo wengi kwa upungufu wa hekima, kwa hakika hawakupaswa kukalia viti hivi.

Haya ni moja ya mapungufu ya awamu hii.

Badala ya teuzi labda hawa nao angalau wangekuwa wakuchaguliwa kama wabunge na madiwani.
 
Fact Fact...
 
Naona Gambo unajitetea ki aina
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…