Pre GE2025 Napinga Mchungaji Msigwa anaposema sasa atafanya kazi ya kuikashifu CHADEMA

Pre GE2025 Napinga Mchungaji Msigwa anaposema sasa atafanya kazi ya kuikashifu CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ni kweli kwamba mtu akihama Chama hawezi tena kukisifu Chama alichotoka ama sivyo ataulizwa kwanini alikihama.

Lakini haiwezekani Msigwa azunguke nchi nzima aanze kusema,"Mbowe ni mnafiki,Chadema hawafai"
Yeye amahama Chadema, mambo ya Chadema sasa hayamhusu tena.

Waachane kwa amani na Chadema kwa amani. Isiwe kwamba sharti lake la kupokelewa CCM ni kuitukana Chadema.

Hata Lowassa alihamia Chadema hatukumsikia anaikashifu CCM.

Pia soma
Huyu self taught mchungaji ni mtu wa kumuepuka. Ujio wake ccm ni kuzidi kukikoroka chama ambapo tayari kimesaliti misingi na itikadi yake. Ubinafsi ndio umetanda sasa.
 
Nimesoma pahala huko Uingereza kuna Mbunge wa Conservative amehama amehamia Labour na ameeleza sababu zote zilizomfanya kuhama na amemlaumu Waziri Mkuu Rishi Sunak na yule wa zamani Boris Johnson.

Haya ni mambo ya kawaida kwenye Siasa na ninamshauri Msigwa aongee yote lakini asiongee UONGO au PROPAGANDA.
 
Siasa ni kukosoana, alikosoa sana CCM akiwa mwana Chadema, sasa ni zamu ya yeye kueleza mapungufu ya Chadema maana ameyaona na kuyaishi.
Mapungufu ya cdm kwani ilishawahi ongoza serikali??

Kuna ujinga mwingi nchi hii
 
Siasa za Tanzania hazina mvuto tena, mi nashangaa ambavyo watu wanakomaa na huyo Msigwa.
Hata kama Msigwa asingehama, CDM ilishajifia kitambo.
Kuitoa CCM madarakani ni maamuzi ya wananchi.
Ni kweli siasa za Tanzania hazina mvuto tena kwa sasa. Na ili kuwatoa ccm madarakani ni adha kwa njia ya machafuko, ama mapinduzi ya kijeshia. Lakini kuendelea kujitokeza kwenye box la kura ni kupoteza wakati. Na watu wasiojitambua tu ndio wataendelea kushiriki hizi chaguzi za kishenzi.
 
Mimi naona umesema vzr sn statement ya kwanza. Na ndo ukweli kuwa siasa za Tanzania hazina mouton tena na watu hawana time tena nazo ni basi tu wachache wanashiriki tena kwa njaa zao.Chadema haijafa,mbona ipo inafanya mambo yake!?Jambo la kujiuliza ni kwanini siasa zife kitu ambacho ni muhimu? Inashangaza na kusikitisha jamii kubwa kujali ujinga wa mpira tena wa simba na yanga na kuipa kisogo siasa inayoamua maisha you!
Huwa nawaza ni nini hatma ya Tanzania?
Ni nani aliyeua siasa?
Magufuli ndio aliyeua siasa za ushindani hapa Tanzania kwa kushurutisha kukubalika yeye na chama chake
 
Mapungufu ya cdm kwani ilishawahi ongoza serikali??

Kuna ujinga mwingi nchi hii
Una uelewa wa kiwango chini kama mtoto wa chekechea.
Siyo lazima ujadili kila hoja, nyingine ziepuke, hilo litakufanya ulinde heshima yako.

Kuayaona mapungufu na sifa za chama cha siasa haijalishi kinaongoza serikali au chama pinzani.
Chama cha siasa ni taasisi ya uma inayosubiri ridhaa ya wapiga kura kuongoza nchi.

Katika kipindi hicho cha kusubiri maamuzi ya wapiga kura chama kinaendesha harakati mbalimbali za kijamii kuwavutia wananchi.

Harakati hizo ndizo zinazotoa mwanga kama chama hicho kiaminiwe au laa.
Harakati hizo pia ndizo zinazopelekea chama cha siasa kisifiwe au kinyume chake kishutumiwe bila kujali kipo madarakani au upinzani.

Sera, Ilani ya uchaguzi, uongozi na mipango ya chama hivi vyote ni nyenzo ambazo chama kinaweza kumwagiwa sifa au kushutumiwa na kudhalauliwa bila kujali kipo madarakani au laa.
Hivyo basi, kukosolewa na kusifiwa ndiyo maisha ya chama cha siasa.
 
Huu ni ushauri wa bure kwa Mchungaji Msigwa

Historia haiongopi. Dr Slaa alipondoka CDM alikwenda moja kwa moja Serena Hotel akiwa na CCM.
Hapa JF tulimwambia kuhama chama si tatizo, kugeuka na kula matapishi ni tatizo

Msigwa amekuwa CDM kwa muda mrefu ndani ya kamati kuu ya chama.
Bila kujali nini kimemuondoa na kwa kuzingatia haki yake ya kufanya siasa, itashangaza kama ataanza kuisema Chadema. Msigwa ni Mchungaji mtu anayebeba dhamana ya uaminifu wa kiroho na mwanasiasa.

Kauli za Msigwa akiwa CDM zilikuwa za kisiasa zikibebwa na 'uaminifu' kama Mchungaji.

Kwa miaka mingi ametunga na kusimamia sera za CDM. Matatizo ya vyama siasa hayakukosekana.
Ni Msigwa huyo wiki iliyopita alisema ' kuetetea sera za chama ni wajibu''

Msigwa aliyeandika sera na kuzisimamia tena wiki moja iliyopita akiwa mwanasiasa na Mchungaji sasa anakwenda 'kueleza uongo wa CDM'' na siyo sera alizotunga , kuzisimamia na kuzisimamia

'Kuusema 'Uongo'' wa CDM aliousimamia utaondoa sifa yake ya Uchungaji achilia mbali siasa.

Namshauri kwa dhati kabisa, Msigwa asimamie sera za CCM na kuzieleza vema! Ni haki yake

Ni haki yake pia kueleza ''uongo wa CDM na Saccos'' lakini haki hiyo itamuondolea heshima yake mbele ya jamii.
Kwamba kwa miaka mingi hakuliona hilo? Kwamba leo anakula matapishi yake, ni mzima kiroho na kiafya?

Msigwa, kuna maisha nje ya siasa, isijefika mahali jirani akatilia shaka kuomba chumvi nyumbani kwako.
Ikafika mahali watoto wako wakaacha kutumia jina la ubini kuepuka fedheha ya muda mfupi na mrefu.


JokaKuu Tindo
 
Ni kweli kwamba mtu akihama Chama hawezi tena kukisifu Chama alichotoka ama sivyo ataulizwa kwanini alikihama.

Lakini haiwezekani Msigwa azunguke nchi nzima aanze kusema,"Mbowe ni mnafiki,Chadema hawafai"
Yeye amahama Chadema, mambo ya Chadema sasa hayamhusu tena.

Waachane kwa amani na Chadema kwa amani. Isiwe kwamba sharti lake la kupokelewa CCM ni kuitukana Chadema.

Hata Lowassa alihamia Chadema hatukumsikia anaikashifu CCM.

Pia soma
Mchungaji msigwa siyo mtu wakwaza kutoka CDM na kuinanga hata Dr. Slaa alipotoka CDM aliinanga sana kwasababu yeye alikuwa anajua AtoZ ya ndani kabisa ya CDM ndiyo maana aliwahi kushangaa watu kusema Mbowe siyo Gaidi. Kwahiyo hata msigwa atabwabwaja kadiri anavyo weza ila itikadi ni Imani. Watu wenye imani na CDM hata uwaambie CDM ni mumiani hawako tayari kukihama mpaka wanyonywe Damu. Kwahiyo Msigwa aachwe asime anayo yataka kusema, na kesho na keshokutwa akitaka kurudi CDM watampokea kwani Mbowe siku zote anasema kwenye siasa hakuna Adui wakudumu. Ila adui akija kwako akikuomba urafiki nenda naye kwa tahadhari ukimkaribisha nyumba anatakiwa Aishie varandani usimwingize vyumani kwani wakati mwingine kaja kwa unafiki. Msigwa ajaenda CCM kwa kupenda ala kufuata Maslai. Kaamua kuuza utu wake na sasa anasaliti Chama chake kwa vipande vya mkate. Anajua kabisa CCM hawamuitaji kwa lolote zaidi ya umaarufu wake kwa sasa na mda wowote ukiisha watamtupa kama takataka nyingine.
 
Watu hawapendi kujifunza, Hayati ENL alihama CCM ila hakusema ataanza kuinanga CCM alifanya siasa za kistaarabu, tujaribu kujifunza kwake.
 
Una uelewa wa kiwango chini kama mtoto wa chekechea.
Siyo lazima ujadili kila hoja, nyingine ziepuke, hilo litakufanya ulinde heshima yako.

Kuayaona mapungufu na sifa za chama cha siasa haijalishi kinaongoza serikali au chama pinzani.
Chama cha siasa ni taasisi ya uma inayosubiri ridhaa ya wapiga kura kuongoza nchi.

Katika kipindi hicho cha kusubiri maamuzi ya wapiga kura chama kinaendesha harakati mbalimbali za kijamii kuwavutia wananchi.

Harakati hizo ndizo zinazotoa mwanga kama chama hicho kiaminiwe au laa.
Harakati hizo pia ndizo zinazopelekea chama cha siasa kisifiwe au kinyume chake kishutumiwe bila kujali kipo madarakani au upinzani.

Sera, Ilani ya uchaguzi, uongozi na mipango ya chama hivi vyote ni nyenzo ambazo chama kinaweza kumwagiwa sifa au kushutumiwa na kudhalauliwa bila kujali kipo madarakani au laa.
Hivyo basi, kukosolewa na kusifiwa ndiyo maisha ya chama cha siasa.
Kwenda we bumunda tu

Mlaumu yule anayeharibu mifumo ili atawale milele
 
msigwa anazunguka kwenye mikutanobya ccm kama nani? anakaa nukwaa kuu kufanyann? hiyu ni mwanachama wa kawaida hiyo water mouth reception anapewa kwa kazi gani?

kutuambia chadema kuna uozo 123 ni upuuzi tu, angepambana nao kwanza ndani ya chadema wakamtimua kama kafulila zitto kitila tungeleewa otherwise ni utopian tu.

msigwa amekaa cxm miaka saba na hayo madudu uzunguni kwake alikuwa wapi kuyafurusha. kama hakuyafurusha ya cdm ya ccm atayaweza? ana uhakika gani madudu hayohayo ccm hayapo?

msigwa na mwenzie peneza wanaccm wanataka kujua ni vipi atawanufaisha wanaccm, ni namna gani ccm imepata mawazo chanya mapya,

ooh cdm kuna ma pakashume its non of our business
 
Back
Top Bottom