Narudi bongo, msaada wakuu!

Chrispin mi ni HE. Na ushauri wa wengi nitumie Tigo. Nimeonelea nikija ntakucheki unipe hiyo Tigo. Hapa nafuata ushaur wa FirstL na wengine wengi. Thanx in advance

Mimi ni liHE. Karibu sana kama utaweza kuvumilia matumizi yake. Ni very complicated.
 
ah yoyo, umefufuka? ulipotea wapi lakini bwana, chriss, geof, nguli, fidel na masanilo wanasumbua sana hapa, i hope hutakuwa upande wao, au ndo chama kubwa lenyewe na wewe?
Nipo hasa vijijini mkuu 2010 imekaribia......
 
Mtandao tumia tigo,kuhusu vyumba karibu na airport mi sikushauri,coz kunamisukosuko ya bomoa bomoa usije liwa fedha zako bure!!
 
anatuzingua tuu hamna mtu TZ ambae hana ndugu anaeisi Dar es salaa, hata wa kufosi?miaka 2 nyuma alikua anakaa wapi? awaambie ndugu zake waje kumpokea?kwani maswali haya hawezi kuuliza ndugu zake, na je eti anataka kujua aina ya sim mwanzo je alitumia sim gani?atasema nataka umaaruf JF! Kaazi kweli kweli
usituzingue bwana toa ushamba wako huko
 
Wabongo kwa kujibu maswali daaaah
 
Mazee yaelekea una kichwa kigumu sana..jifunze kuelewa wengine wanachoandika..lol.

Sizungumzii rangi wala 'uswahili ' ule unaouelewa wewe, nazungumzia ukosefu wa ustaarabu, hisani na kushindwa kuheshimu thread za wengine.

Mbado?

Achana na Crispin ... jamaa ni sexually frustrated in real life. Mwache ajitutumue humu apate moyo kwamba na yeye ni mwanamme rijali.
 
Mi nimemshangaa Tripo9 kwa thread yake isiyokuwa ma kichwa wala miguu. Ina maana hana ndugu aliowaacha, jamani mbona wa-Afrika hata yule ndugu wa mbaliiii anaitwa dada au kaka e.t.c. Eti miaka miwili tu mtu amesahau wapi pa kulala???Bwana eeh tuondolee ulimbukeni wako! huo ni upoli poli u know!
 
Karibu Bongo, Mtandao rahisi ni Tigo kwa simu, mtandao wa internet ambao kidogo uko faster na haukatikati ni Sasatel ni wazuri hawa .
Kuhusu Nyumba au chumba hilo sina uhakika nalo , kwanini kwanza ukae huko Airport ni una ndugu wako maeneo hayo? , navyojua huko kuna foleni mbaya kwenda na kurudi na nadhani ungetafuta sehemu za Mikocheni B ni nzuri , vibaka hakuna na bei una weza pata sio mbaya sana inategemea umejipangaje ,Ongea na madalali wa Mikocheni B labda wanaweza kukusaidia.


To Wabongo
Lakini wabongo kwanini mna mawazo ya kimasikini namna hiyo ?, mwenzenu kosa kukaa nje ya TZ nyie bado mnaona eti anawaringishia, tatizo ni umasikini wa wa tanzania , mtu huwezi sema jana nime rudi toka New York bila kurogwa , acheni fikra za karne ya zilizo pita ,Siku hizi kusafiri na kuka nje ni jambo la kawaida sana ,so msione ni ajabu mtu kusema na rudi Bongo , kwani kuna ubaya gani akiuliza ?, huwezi jua mambo mengi yamebadilika kwa mwaka mmoja tuu sembuse miala miwili.
 

Acha uzushi miaka miwili hakuna mabadiliko yoyote bana...mie nimekaa ughaibuni miaka 15 nimerudi naona hakuna mabadiliko yoyote
- maji bado ni ya ndoo
- umeme wa mgawo
- barabara mbovumbovu, kidogo za mjini wametia vijilami vya mchina.
- uchafu kama kawa
- UFISADI kwa kwenda mbele
- magomeni kota,ilala kota,kinondoni kota bado zipo
-viongozi wale wale i.e KINGUNGE NGOMBALE MWIRU et al.
- Ajali,vibaka,rushwa,uzembe kila eneo kama kawa.
- Hayo sijui matigo,mazain,maceltel yale yale, sema ni majina tu yamebadilika.
habari ndo hio............
 
Poa man 'mtoto wa kishua' hawa sasatel wana kua wanachaji kivipi yaan. Labda kwa mwez au kwa bytes unazo2mia.
Na kwa wale wanaosema nkae kwa ndugu mie simaindishi mambo hayo. Wapo ndugu wakuvuta na kamba dar ndio but km naweza kujilipia haina haja. Ndugu wako mkoani nsingependa nibebe mamzigo yote mpaka huko. Argh! Great thinkerz wengine bwana!
 

Ni mtazamo tu. Usilazimishe wengine mtazamo wako.

Kama miaka 15 iliyopita ulikuwa na uwezo wa kuwa na simu, basi at least utagundua sasa hivi unazungukwa na watu wengi zaidi wenye simu kama wewe. Hilo ni badiliko. Kama miaka 15 iliyopita ulikuwa huna uwezo wa kununua simu, utagundua sasa hivi unao uwezo wa kufanya hivyo. Hilo ni badiliko pia. Kwani miaka 15 iliyopita ulipokuwa hapa mtandao gani wewe ulikuwa unaongea kwa sh. 1 kwa sekunde? Utagundua mambo yamebadilika sana tu.

Mimi niko hapa hapa bongo miaka yote, na ninaona mabadiliko.
 
UNATUZINGUA
kama unandugu mikoani na hapo dar wa manati si uwaulize hayo mambo ya sim? inamaana hata ndugu zako hauwasiliani nao ulipo...afu mara unakaa wiki mara wiki mbili acha kutuzingua
hauko pekeyako wanaokaa nje, wapo kibao na wanarudi baada ya miaka 5 na wanawasiliana na ndugu zao
ACHA UKUDA NA USHAMBA/ULIMBUKENI et all
 

Ukiondoka majuu kwa miaka miwili ukaja Bongo, utakaropudi utakuta leaps of changes. Kama ukiondoka Tanzania akishi majuu kwa miaka 20 hata ukirudi utakuta kila kitu ni vilievile, mabadiliko yanayotokea mengi ni negative, ingawa kuna mawili matatu positive. Sasa mabadiliko 20 negative vs mawili positive, ndio hayo jamaa anayesema miaka 15 hajaona lolote la maana, which is true.
 







[ame="http://www.youtube.com/watch?v=ce9D8ULCGaI&feature=related"]
[/ame]









Mimi nina kubaliana na Ndugu Tripo9 ana haki ya yote aliyo yauliza je mtakubaliana na mimi pia ninauliza je nikija huko Bongo toka majuu niulize kama ndugu Tripo9? Kwa sababu Tangu nilipoondoka hapo Bongo sasa ni miaka 17 niambieni Uwanja wa ndege upo wapi? na hali ya Mji ikoje?barabar za miji ipoje? je sokoni kariakoo kusafi? hali ya umeme na Maji safi yatokayo katika Bomba yapo? au bado mnatumia maji ya Visima? Mie hata huo mji nimeusahau nilikuwa nakaa Magomeni Kagera sasa niambieni huo mji ukoje? kwa mfano Manzese nasikia lipo Daraja la kuvuka watu kwa juu niliwauliza baadhi ya wabongo waliotoka huko hivi karibuni wakaniambia Manzese kwenye hilo Daraja watu ikifika usiku wanakabwa je ni kweli? haya Tandale vipi sokoni kukoje?Mburahati kukoje?Makurumla bado ipo shule ya msingi?jaribu kunielewesha maana nikija nisipate kupotea kwa huo mji nikakutanana Matapeli maana kukaa miaka 17 majuu si mchezo bwana huku majuu tumezoea kuona majumba ya Magorofa makubwa barabara nzuri hali ya hewa baridi,unakuwa mtu mwenye furaha hakuna mambo ya kukatika Umeme Au maji hakuanamambo ya Foleni eti foleni ya sukari au mchele au sabuni yaani kwa wastani maisha ni mazuri masikini anaishi kwenye nyumba nzuri na anakula chakula kizuri na anavaa vizuri lakini si unajuwa waswahili wanasema nyumbani ni nyumbani hata kukiwa kubaya lakini ni nyumbani tu. au kuna msemo mmoja wa waarabu wanasema nyumbani ni nyumbani hata kukiwa juu ya mlima lakini ni nyumbani kwako
na azarau kwao ni mtumwa huyo asanteni sana Ndugu zangu Wana JF Msimlaumu ndugu Tripo9 kwa kuuliza Swali lake hilo hata akina sisi wengine tumesha sahau bongo
 
karibu sana, ila kuwa makini, tigo ni bomba
 


lol!
mimi nilijua mishebeduo ya hivo ilikwisha zamani. mbona watu kibao tu hm JF wanashuka bongo bila MATANGAZO? mtu ana miaka mitano tu nje anajifanya mwenyeji wa Ughaibuni mgeni wa BONGO! teh teh! kaaaz kweli kweli! hapo tu anajifanya ana ndugu wengi mtoni kuliko Tabora! mweh1...mijitu mingine sijui NGUMBARU!
kARAGHAbaho.
Naizimia Bongo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…