NASA yaingia kwenye anga hewa la jua

CCM ikifafanua kwa wananchi jinsi ambavyo imeipaisha Tanzania ndani ya miaka 60 ya uhuru hadi kukaribia mafanikio ya NASAπŸ‘‡πŸ˜πŸ˜πŸ˜
Your browser is not able to display this video.
 
Akili yangu bado ina wenge.....

"[emoji3578]Hivyo chombo cha parker solar probe kimeendelea kuweka record za kibabe ya kuwa chombo chenye kasi kubwa zaidi kuwahi kutengenezwa na mwanadamu ambapo huweza kwenda kasi ya Kilometer 194 kwa sekunde (194 Km/s) ama Kilometer 700,000 kwa saa ( 700,000 Km/h) [emoji2930][emoji100][emoji91]"

Mfano:
Safari ya Dar mpaka Moro, just for one second...?

Hicho chombo kikiwa kwenye maximum speed, sidhani kama kitaonekana kwa macho au hata camera.

Ufafanuzi please...
 
Inanishangaza San mm hiki kitu wanachofanya Hawa wazungu Ni sawa na kwenda kumchokoza muumba wa vitu hvyo

Alfu unasema. Speed ya chombo Ni km/h 194 kwa second hiyo kitu HAKIWEZEKANI YAANI HATA KWA MACHO AKIONEKANI hpn kwa kweli duh kufumba na kufumbua km 194. Hap na Moro kwa sec
 
Sidhani kama hicho chombo sio tu kutua Bali hata kulisogelea jua kwa ukaribu kimeweza. Usifanye mchezo na joto la jua! Jua halisogeleki kabisa wala kugusika!
 
Good!
 
CHOMBO CHA PARKER SOLAR PROBE CHAFIKA KATIKA ANGA HEWA YA JUA 🌞🌞

Soma Hapa Uelewe kwa Undani

Ndio chombo cha kwanza kilichotengenezwa na mwanadamu kuweza kufika katika maeneo ya anga hewa za Jua kwanza kabla ya kuendelea hivi hunafahamu hata kwenye sayaru yetu ya dunia bado tupo katika anga hewa ya Jua inayoitwa Corona yaani hili Joto lote tunalolipata mpaka kwendelea huko pluto ni kutokea kwenye ule mlipuko wa anga hewa ya corona anga hewa ya Jua huisha tu mpaka pale utakapofikia interstellar space

Chombo hichi kilirushwa 2018 na Nasa ila kilitengenezwa nchini canada siunajua Nasa wanamatawi mengi lengo la chombo hichi ni kwenda kulisoma Jua kiundani zaidi yaani tangu hapo mwanzo tumekuwa tukilisoma Jua kwa umbali fulani kwasasa tumeamua kwenda indeeep zaidi ila hatutazidi umbali wa 8-5 million kilomita kwasababu hatutakuwa na chombo kitakachoweza kuhimili Joto kali sana

Kwasasa chombo kimefika katika Anga hewa ya Jua ambayo inafahamika kama Corona umbali wa Takribani 8 million km kutokea kwenye surface ya Jua kimevunja rekodi kufika katika eneo hilo ambalo ndio eneo lenye Joto sana au tuseme Joto linalotawanywa kwenye maeneo mbalimbali ya solar syetem baada ya kutoka kwenye kiini kuja kwenye surface na kuanza kusafiri hapa Joto huweza kufikia mpaka 1 million centigred

Ndio katika anga hewa la corona hufikia hadi 1 million centigred kutokana na " baada ya joto kuzalishwa Jingi huko ndani kwenye ule mchakato wa Nuclear fission Joto huzidi sana na huwa linatafuta sehemu ya kutokea ambapo kutokana na solar magnetic zinazoizunguka Jua huchana baazi ya maeneo ya Jua na lile joto lililokuwa na uji uji wa moto huruka juu kama fataki wakati wa kutoka hukutana na solar winds ambapo hizi winds hubeba punje punje za ule moto anga hewa corona na hutawanja maeneo mbalimbali ya ulimwengu

Je Kwanini chombo hicho hakiwezi kupata madhara ?

Chombo hakiwezi kupata madhara kama kitazunguka katika umbali uliopangwa kumbuka ni 8-5 million km tu kikizidi hapo bye bye

Chombo kimewekewa ngao yenye kuhakisi mwanga kumbuka kitu chochote chenye kuhakisi mwanga hupunguza ukali na Joto la Jua tofautisha na vile vinavyosharabu kwahiyo baada ya ile ngao nyuma yake kuna madini ya carbon ambayo wengi wetu tunayajua fuatilia kwenye rocket ya starship utaona kuna kama madude meusi huku chini

Kwahiyo kwa uwepo wa ngao inayoakisi mwanga na madini ya carbon pia hiyo haitoshi kuna mfumo wa kupoza kumputers umewekwa baada ya madini ya carbon hivyo kufanya computer na camera zote na mifumo mengine yote kuwa salama bila ya kuathiriwa na Jua yaani hapa tuseme ni kama kwenye dunia yetu tuna ngao ya asili earth magnetic field ambayo hupambana na hizi solar winds ambazo zina miale mikubwa sana ya moto kutokea kwenye Jua

Chombo hichi kimeweza pia kufikia spidi ya 194 km/s ambayo ni sawa na 700,000 km/h kumbuka chombo kiliweza kukusanya nguvu kupitia maeneo mbalimbali ili kuweza kupenetrate katika eneo hili

πŸ€” Kwa wale wanaouliza maswali haya kuhusu picha nani aliyepiga picha napenda kuwajibu kwamba hizo picha ni za computer generated kwasababu chombo kipo pekee yake huko na kumbuka kinapiga picha jua hakiwezi kujipiga picha chenyewe hivyo wanasayansi wanatoa picha hizi kwa sababu tupate kujifunza na kitambua kumbe chombo hukaa kwa mkao huu huko kwenye Jua

πŸ€” NB: NITAANDAA UZI MAALUM KWA MASWALA YA ELIMU YA ANGA , SAYANSI NA TEKNOLOJIA ZAKE. MNAKARIBISHWA KUULIZA NA KUTOA MAJIBU NA UFAFANUZI UKIWA NA UELEWA WA MASWALA YA SAYANSI YA ANGA PAMOJA NA MAMBO YA TEKNOLOJIA
 
Ni nini kimetumika kuipiga picha hiyo solar probe?
Kwa wale wanaouliza maswali haya kuhusu picha nani aliyepiga picha napenda kuwajibu kwamba hizo picha ni za computer generated kwasababu chombo kipo pekee yake huko na kumbuka kinapiga picha jua hakiwezi kujipiga picha chenyewe hivyo wanasayansi wanatoa picha hizi kwa sababu tupate kujifunza na kitambua kumbe chombo hukaa kwa mkao huu huko kwenye Jua
 
Wao walionaje kama kinakaa kwa mkao huo?

Na kama wameweza kutengeneza picha isiyo halisi kwenye computer tunawezaje kuwa na hakika kama wamefikisha hiko chombo?

Eti mkuu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…