NASA yaingia kwenye anga hewa la jua

NASA yaingia kwenye anga hewa la jua

Poa mkuu najitahidi kukuelezea ila usikaze ubongo,ipo hivi
Spacecraft zote huwa zinafungwa kamera ili kupiga picha mahali ambapo imetumwa,mfano kama imetumwa iende sayari ya mars basi itafungwa kamera ikapige picha hiyo sayari ya mars kama vile ilivyofanya curiosity rover,kama imetumwa iende saturn basi itawekewa camera ikapige picha sayari ya saturn. Lakini hamna spacecraft inayofungwa kamera ili ijipige yenyewe wakati ipo safarini .Hizo picha za spacecraft unazoziona kama hiyo parker solar probe ni picha zilizotengenezwa tu na computer kwa ajili ya simulation ya mission na pia kurahisisha watu waweze kuelewa kinachoendelea kiurahisi, just imagime NASA au ROSCOSMOS ya urusi wangekuwa hawatoi picha yani watupe tu data ya vyombo vyao wanavyotuma huko si tungekuwa tunatafutana sahivi, kwa hiyo ili kurahisha mambo wakaona sehemu ambazo huwa haziwezi kupigwa picha huwa wanatengenezea wenyewe kwenye computer. Kwahiyo kiufupi kuna picha ambazo ni halisi na nyengine sio halisi ,picha halisi ni zile zinazopigwa na spacecraft zikiwa huko zilipotumwa kisha zinatumwa duniani mfano picha za dunia kutoka kwenye ISS,picha ya sayari ya mars,picha za saturn,picha kutoka kwenye satellites etc. Na picha ambazo si halisi ni zile ambazo kuna sehemu hamna namna ambayo utaweza kupiga picha kwa hiyo huwa wanazitengeneza tu kwa computer mfano ndio kma hicho chombo kikiwa safarini kuelekea kwenye jua huwezi kukipiga picha kwakua kinasafiri spidi kali mno na pia hamna kitu kilichopo huko kwenye jua ambacho kitaweza kukipiga picha
Asante sana nimekuelewa vizuri, sasa kama hizo picha si halisi yani watu wamecheza na adobe je, kutakuwa na uhakika gani kama hata hiko kifaa kimefika wakati hamna picha halisi zote ,zimetengenezwa?

Mfano mimi nikianzisha taasisi inayo husiana na sayansi ya mambo ya anga then nika utangazia umma kuwa nimepeleka chombo hilo eneo halafu nikatengeza picha za namna hiyo, lakini niwe sijapeleka chombo wala nini. Nasa watakuwa wamenizidi kitu gani hasa katika fact?
 
Asante sana nimekuelewa vizuri, sasa kama hizo picha si halisi yani watu wamecheza na adobe je, kutakuwa na uhakika gani kama hata hiko kifaa kimefika wakati hamna picha halisi zote ,zimetengenezwa?

Mfano mimi nikianzisha taasisi inayo husiana na sayansi ya mambo ya anga then nika utangazia umma kuwa nimepeleka chombo hilo eneo halafu nikatengeza picha za namna hiyo, lakini niwe sijapeleka chombo wala nini. Nasa watakuwa wamenizidi kitu gani hasa katika fact?
Uhakika upo mana nishakwambia kwamba chombo kikfika huko pia kinapiga picha na kuzituma duniani,wewe umetuma chombo Mars kimefika na kikapiga picha huko Mars halafu kikakutumia utakua bado hujaamini tu?
Pia chombo kikisharushwa huko kwenye space tunaweza kuwasiliana nacho huku duniani na tukajua kipo wapi kinatembea spidi gani kina temperature kiasi gani na tukiomba picha za huko kinatutumia na mambo mengine mengi tu.Hata wewe sahvi unaweza ukadownload apps kwenye simu yako ambazo zinakupa mawasiliano na baadhi ya satellites ambazo zipo kwenye space mfano ISS pia kama una telescope unaweza ukaviangalia mwenyewe kupitia telescope yani kuna njia nyingi sana za kujua, sio wewe ukae tu useme umerusha chombo angani haya tukikwambia tunataka kukiona hicho chombo kwa telescope au tuwasiliane nacho kwa computer au tukiombe hicho chombo kiturushie picha za huko kilipo utafanayaje?
Nikutolee mfano satellite ya kwanza ilirushwa na warusi kipindi hicho ilikiwa ni soviet union, walivyoirusha walijua kabisa wapo watu watabisha kama hawajarusha sattelite kwa hiyo walichokifanya wakafunga radio transmitter kwenye hiyo sattellite ili ikishafika huko nje ya dunia iweze kutuma radio signals duniani, so wewe kama ulikuwa unataka ujue kama warusi kweli wamerusha satellite ulikuwa unachukua kifaa maalum kinachopokea mawimbi ya radio halafu kikishapokea hayo mawimbi kinaanza kutoa sauti,uwe marekani uwe Canada uwe ulaya uwe China hayo mawimbi ya radio yatakufikia tu ukitumia kifaa maalum cha kuyapokea. kwahiyo dunia nzima waliiamini satellite ya urusi mana hakukuwa na namna unaweza kubisha wakati satellite ipo na inasikika.
Na pia hao NASA wana washindani wao wakarne na karne ambao ni ROSCOSMOS ya urusi na space agency ya China,yani hata wakidanganya hao washindani wao hawawezi kukaa kimya hata siku moja mana wanashindana kwelikweli kila mmoja anatak aonekane yeye ndio yupo juu kwenye tafiti za anga kuliko mwenzake so sio rahisi kudanganya hata kidogo lazima uumbuliwe na hii tafiti ya kwenda kwenye jua Marekani amewapiga gepu kubwa sana warusi na wachina kwahiyo isingekuwa ya kweli wachina na warusi wasingenyamaza.
 
AS
Poa mkuu najitahidi kukuelezea ila usikaze ubongo,ipo hivi
Spacecraft zote huwa zinafungwa kamera ili kupiga picha mahali ambapo imetumwa,mfano kama imetumwa iende sayari ya mars basi itafungwa kamera ikapige picha hiyo sayari ya mars kama vile ilivyofanya curiosity rover,kama imetumwa iende saturn basi itawekewa camera ikapige picha sayari ya saturn. Lakini hamna spacecraft inayofungwa kamera ili ijipige yenyewe wakati ipo safarini .Hizo picha za spacecraft unazoziona kama hiyo parker solar probe ni picha zilizotengenezwa tu na computer kwa ajili ya simulation ya mission na pia kurahisisha watu waweze kuelewa kinachoendelea kiurahisi, just imagime NASA au ROSCOSMOS ya urusi wangekuwa hawatoi picha yani watupe tu data ya vyombo vyao wanavyotuma huko si tungekuwa tunatafutana sahivi, kwa hiyo ili kurahisha mambo wakaona sehemu ambazo huwa haziwezi kupigwa picha huwa wanatengenezea wenyewe kwenye computer. Kwahiyo kiufupi kuna picha ambazo ni halisi na nyengine sio halisi ,picha halisi ni zile zinazopigwa na spacecraft zikiwa huko zilipotumwa kisha zinatumwa duniani mfano picha za dunia kutoka kwenye ISS,picha ya sayari ya mars,picha za saturn,picha kutoka kwenye satellites etc. Na picha ambazo si halisi ni zile ambazo kuna sehemu hamna namna ambayo utaweza kupiga picha kwa hiyo huwa wanazitengeneza tu kwa computer mfano ndio kma hicho chombo kikiwa safarini kuelekea kwenye jua huwezi kukipiga picha kwakua kinasafiri spidi kali mno na pia hamna kitu kilichopo huko kwenye jua ambacho kitaweza kukipiga picha
asante kwa kunisaidia kujibu
 
Mkuu hiko kifaa.
1.kimetengenezwa na materials gani? na
2.kinatumia mafuta,gesi au nini muda wote huo kutembea?
3.kinatuma taarifa kutoka huko hadi duniani kwa kutumia mfumo gani?
4.Huko anga za mbali,hakuna hewa wala gesi,wala chochote,je hiko kifaa kinawezaje kutuma data zake?
1.Chombo kimetengenezwa kwa materials mengi mno yani kila sehemu na kila component ina materials yake,ila nahisi utakua umemaanisha materials ambyo yanayokifanya chombo kisiathiriwe na joto kali la jua,
Chombo hakiathiriwi na joto la jua kwa sababu kina heat shield ambayo imeundwa kwa carbon composite materials.Heat shield inalikata na kureflect joto la jua yani inafanya kama kulikwepa ndio mana haiathiriwi japo kuwa joto la jua ni kali mno.Kwa lugha nyepesi heat shield haijaundwa ili kupambana na joto la jua bali imeundwa ili iweze kulikimbia joto la jua. Heat shield ya chombo ingeundwa ili ikapambane na joto la jua basi chombo kingekuwa kishayayuka zamani tu.

2.Kwanza inabidi ujue speed ya hicho chombo imepatikana kutoka kwa rocket iliyotumika kupeleka chombo huko kwenye space inaitwa DELTA 4 heavy, na kitu kikishafika huko kwenye space kama tayari kina spidi ya kutosha hakiwezi tena kusimama kwa sababu huko hamna external force kama vile air friction itayoifanya hicho chombo kisimame , kinachotumika kama mafuta ni nishati inaitwa hydrazine monopropellant ambayo inatumika tu kusahihisha njia ya chombo wakati inapokosea,na hiyo nishati haiishi leo wala kesho kwa sabbu inatumika kwa uchache mno.
Pia chombo kina solar panels ambazo zinazalisha umeme ili kuviwezesha vifaa mbalimbali ndani ya chombo viweze kufanya kazi kama vile kamera,sensors na antenna

3. Kinatuma taarifa kupitia antenna, antenna zinatumia Radio waves ambazo zinasafiri kwa spidi ya mwanga na ndizo zinazobeba data zinazokusanywa na parker solar probe na kuzituma duniani.

4. Data zinatumwa kupitia radio waves ambazo zinafanya kazi mahala popote hata kama hamna gesi wala upepo
 
Broaden your knowledge by passing through here. Do not just sit and argue foolishly (sijakutusi lakini)
Screenshot_20211222-152403.jpg
 
SPACE X WAFANIKISHA KUPOKEA BOOSTER KWA MARA YA 100 👏👏👏

Hapo jana kampuni ya space x imeweka rekodi ya kupokea kwa ukamilifu booster ya 100 katika kipindi cha miaka 6 tangu wafanikiwe kupokea booster yao ya kwanza miaka 6 iliyopita

Kumbuka awali ya yote ilikuwa ni kitu kigumu sana kwa shirika lolote lile kuweza kupokea booster zilizokwisha kutumika baada ya kupeleka mzigo kwenye orbit ndogo ya dunia mashika mengi huziachilia booster zote baharini na kuja kuzichukua baadae ila huwa ni risk sana kwakuwa zengine huwa zimesharibika baada ya kujipigiza vibaya kwenye bahari

Kampuni ya space x ilikuja na wazo la kuzipokea hizi booster kwa mfumo maalum ambapo ilikuwa ni ngumu sana na kujikuta wakipata tabu sana kufanikiwa kwakuwa booster zote zilikuwa zinalipuka mara baada zikikaribia tu kufika chini au mara baada ya kufika chini lakini umahiri wa wanasayansi wa kampuni hii hatimaye waliweza kufanikiwa mnamo mwaka wa 2016 hivyo ndio ukawa mwanzo mzuri sana wa matumizi ya rocket bora ambazo zipo chini ya tajiri elon musk

Siri kubwa ya mafanikio usikate tamaa kuwa na imani weka nia wekeza usiogope wekeza katika kile unachokiamini hasara ni moja ya changamoto katika kuelekea kwenye mafanikio bora

Kupanga Ni kichagua


Ameandika:Moudy Swema

FB_IMG_1640187785206.jpg


FB_IMG_1640187792202.jpg


FB_IMG_1640187797749.jpg


FB_IMG_1640187803099.jpg
 
Ni upuuzi uliopiliza kuamini uongo huu . Hakuna chombo chochote kilichowahi fika kwenye jua halafu unatutajia nyuzi joto zake ulipima kwa kutumia nini? Km 7Mln umezipimaje wakati hakuna chombo kilichowahi kufika kwenye jua?, Ni chuma au Madini gani hayo yatayoweza kuhimili Moto Mkali namna ile kutoka kwenye jua na yanapatikana sehemu gani Duniani? . Uletewa picha za kutengeneza kwenye computer nawe unafumvazwa akili unaamini. Amka Mwana fikra pevu waza bila box usiwaze nje ya box.
Kujifunza si ujinga... Toka huko gizani[emoji23]

 
Kujifunza si ujinga... Toka huko gizani[emoji23]

Watu wa dizaini hiyo huwaelezi kitu mkuu, yani wana maswali halafu wanajijibu wenyewao majibu wanayotak wao.Mtu hajui kitu kinasurvive vipi kwenye jua so hapo inabidi aulize ili ajifunze watu wametumia teknolojia gani kukilinda chombo kisiathiriwe na jua ila yeye unakuta anajijibu mwenyewe tu kwamba haiwezekani na hao NASA watakua waongo. Watanzania wenzangu tusiwe na akili closed namna hii kitu kama hujui uliza utajibiwa mana wewe unachoona hakiwezekani ujue wenzako huko duniani wanakifanya tena bila ya shida yoyote.
 
Watu wa dizaini hiyo huwaelezi kitu mkuu, yani wana maswali halafu wanajijibu wenyewao majibu wanayotak wao.Mtu hajui kitu kinasurvive vipi kwenye jua so hapo inabidi aulize ili ajifunze watu wametumia teknolojia gani kukilinda chombo kisiathiriwe na jua ila yeye unakuta anajijibu mwenyewe tu kwamba haiwezekani na hao NASA watakua waongo. Watanzania wenzangu tusiwe na akili closed namna hii kitu kama hujui uliza utajibiwa mana wewe unachoona hakiwezekani ujue wenzako huko duniani wanakifanya tena bila ya shida yoyote.
Nailed it mkuu... Watu wapo gizani sana
 
Asante sana nimekuelewa vizuri, sasa kama hizo picha si halisi yani watu wamecheza na adobe je, kutakuwa na uhakika gani kama hata hiko kifaa kimefika wakati hamna picha halisi zote ,zimetengenezwa?

Mfano mimi nikianzisha taasisi inayo husiana na sayansi ya mambo ya anga then nika utangazia umma kuwa nimepeleka chombo hilo eneo halafu nikatengeza picha za namna hiyo, lakini niwe sijapeleka chombo wala nini. Nasa watakuwa wamenizidi kitu gani hasa katika fact?
We jamaa umenichekesha sana unachoshindwa kujua ni kwamba hao jamaa hawapo kwaajili ya kukupa uhakika wewe bali wapo kwenye mambo yao
 
Uhakika upo mana nishakwambia kwamba chombo kikfika huko pia kinapiga picha na kuzituma duniani,wewe umetuma chombo Mars kimefika na kikapiga picha huko Mars halafu kikakutumia utakua bado hujaamini tu?
Pia chombo kikisharushwa huko kwenye space tunaweza kuwasiliana nacho huku duniani na tukajua kipo wapi kinatembea spidi gani kina temperature kiasi gani na tukiomba picha za huko kinatutumia na mambo mengine mengi tu.Hata wewe sahvi unaweza ukadownload apps kwenye simu yako ambazo zinakupa mawasiliano na baadhi ya satellites ambazo zipo kwenye space mfano ISS pia kama una telescope unaweza ukaviangalia mwenyewe kupitia telescope yani kuna njia nyingi sana za kujua, sio wewe ukae tu useme umerusha chombo angani haya tukikwambia tunataka kukiona hicho chombo kwa telescope au tuwasiliane nacho kwa computer au tukiombe hicho chombo kiturushie picha za huko kilipo utafanayaje?
Nikutolee mfano satellite ya kwanza ilirushwa na warusi kipindi hicho ilikiwa ni soviet union, walivyoirusha walijua kabisa wapo watu watabisha kama hawajarusha sattelite kwa hiyo walichokifanya wakafunga radio transmitter kwenye hiyo sattellite ili ikishafika huko nje ya dunia iweze kutuma radio signals duniani, so wewe kama ulikuwa unataka ujue kama warusi kweli wamerusha satellite ulikuwa unachukua kifaa maalum kinachopokea mawimbi ya radio halafu kikishapokea hayo mawimbi kinaanza kutoa sauti,uwe marekani uwe Canada uwe ulaya uwe China hayo mawimbi ya radio yatakufikia tu ukitumia kifaa maalum cha kuyapokea. kwahiyo dunia nzima waliiamini satellite ya urusi mana hakukuwa na namna unaweza kubisha wakati satellite ipo na inasikika.
Na pia hao NASA wana washindani wao wakarne na karne ambao ni ROSCOSMOS ya urusi na space agency ya China,yani hata wakidanganya hao washindani wao hawawezi kukaa kimya hata siku moja mana wanashindana kwelikweli kila mmoja anatak aonekane yeye ndio yupo juu kwenye tafiti za anga kuliko mwenzake so sio rahisi kudanganya hata kidogo lazima uumbuliwe na hii tafiti ya kwenda kwenye jua Marekani amewapiga gepu kubwa sana warusi na wachina kwahiyo isingekuwa ya kweli wachina na warusi wasingenyamaza.
1. Kuna uhakika gani kama picha zinazo tumwa ni kweli zimepigwa eneo la tukio na sio za kutengeneza?

2. Hizo telescope zinauwezo wa kuview distance gani na zinapatikana wapi?

Hapo mwishoni hujaniwekea facts ila umetaka niamini kwa sababu fulani hajabisha au niamini kitu kwa sababu serikali imesema.

By the way nipo kujifunza naomba msaada mkuu
 
We jamaa umenichekesha sana unachoshindwa kujua ni kwamba hao jamaa hawapo kwaajili ya kukupa uhakika wewe bali wapo kwenye mambo yao
Pengine una tabia ya kucheka tu, hapa tunaelewashana na ndio maana watu wanao elewa umuhimu wa mijadala kama hii wapo wanaendelea kutuelimisha sisi tusio jua.

Hapo kinakuchekesha nini haswa?
 
Akili yangu bado ina wenge.....

"[emoji3578]Hivyo chombo cha parker solar probe kimeendelea kuweka record za kibabe ya kuwa chombo chenye kasi kubwa zaidi kuwahi kutengenezwa na mwanadamu ambapo huweza kwenda kasi ya Kilometer 194 kwa sekunde (194 Km/s) ama Kilometer 700,000 kwa saa ( 700,000 Km/h) [emoji2930][emoji100][emoji91]"

Mfano:
Safari ya Dar mpaka Moro, just for one second...?

Hicho chombo kikiwa kwenye maximum speed, sidhani kama kitaonekana kwa macho au hata camera.

Ufafanuzi please...
Una haki ya kutowaamini hawa viumbe..haswa wamarekani.
Miaka ya 60s walituambia walitua mwezini, wakaja na picha kibao zenye utata.

Ajabu mpaka sasa tuko 2021, pamoja na mabadiliko makubwa ya utaalam wa anga za juu, hawajawahi kurudi tena huko.
Hii inatia mashaka makubwa kama kweli walitua mwezini.
 
Back
Top Bottom