Nasema tusiwapishe viti wazee kwenye daladala, walichezea ujana

Nasema tusiwapishe viti wazee kwenye daladala, walichezea ujana

Mzazi mwema huacha urithi hadi kwa wana wa wa wanawe yaani wajukuu.

Hivi kama una mali za hadi kutumiwa na wajukuu utagombana na wanao kuwa hawakutunzi?!

Mali zako zitakutunza
Hadi Yesu arudi bila kuhusudu msaada wa watoto wako wala wajukuu.

Utaendelea kuwa mshauri tu wa nyendo zao ili kuepuka mabaya na familia zao.
Kuna watu huwa nawashangaa wanamponda MO eti hela za urithi,urithi kwa kizazi chako ni kitu chema,unakata mnyororo wa umasikini
 
Ni masikini tu yule wa kuigiza maisha na asiye na akili ya kitajiri ndo anafikiri kila anayepanda daladala hana gari kama yeye. Lolote linaweza kutokea ukapanda daladala bila kujali una magari au la.
 
Ukiwa mzee halafu huna hela unadharaulika sana. Kama mimi hapa hata siitwagi kwenye vikao vya familia.
Utasikia huyu sijui atakuja kuongea nini si aendelee na vibarua vyake taarifa yakikao atapata tu hata asipohudhuria
 
Walemavu tuwapishe hawakuomba kuwa walemavu. Wajawazito na wenye watoto inahitaji mjadala Ila wazee hapana.

Mitaani kuna magari hadi milioni tatu, bodaboda used mpaka laki sita, hivi kweli mpaka unafika miaka sitini na zaidi hata pikipiki imekushinda.

Tukiacha kuwapisha tutawapa uchungu wa kupambana na maisha hata katika uzee wao.

Kuwapisha siti ni kuwadekeza na kuwafanya wabweteke. Vijana pambaneni msitegemee hisani ya kupishwa siti uzeeni

Mimi hata ukija na miaka 89 sikupishi nakuangalia macho makavu sikupishi. We kula bata ujanani ila jua uzeeni tutakutana kwenye daladala.

Uzee si ugonjwa ni baraka tusiogope uzee, nimejisikia kuwatania babu na bibi zetu.
Deep down wazee wengi walikua wajinga wakawa wapumbavu inasikitisha Sana hii ila ni ukweli mchungu
 
Kuna mmoja alikataa kumpisha mzee kwenye daladala akiwa anaenda interview wakashuka wote kwenye basi

Kuingia ofisi ya interview akakuta yule mzee ndie wa kumhoji oral interview

Kilichofuata alimwamkia tu mzee akamwambia nenda.Alitoka analia akajua kitakachofuata.Hakupata kazi
Chai ya kijiwe hii
 
Nadhani vijana wengi humu wanaongelea nadharia kuna kundi kubwa sana la vijana ambao sasa hivi wana Miaka kibao ajira hamna wengine wana Miaka 40 sasa hivi hawajapata kazi na wamesoma muda sio mrefu wataingia kundi la wazee Kusema walichezea maisha ni kukufuru na kutowapisha viti ni kuwaadhibu Mara mbili

Anyway kifupi mleta mada ana roho ya kishetani na wote wanaom mu support wana roho za kishetani mtakwama mbeleni kimaisha kwa sasa mwajiona salama kwa visenti vichache na vigari mitumba vilivyookotwa majalalani Japan mnavyotembelea .Lakini safari bado ndefu. MUNGU AWALAANI KWA KUTOHESHIMU WAZEE

Amri ya Mungu inasema waheshimu Baba yako na mamako update kuwa na siku nyingi zenye heri duniani .Kutoheshimu wazee kunafupisha maisha au siku zenye heri ndio maana vijana wengi sana sasa hivi wanakufa kuliko wazee na wanaharibikiwa sana vitu vingi kama ukosefu wa kazi,maisha magumu maofisini na majumbani kwenye familia zao,nk lakini sababu kuu ni kuwa heshima kwa wazee hamna .
Na mlaaniwe na Mungu wote mlioonyesha kutokuwa adabu kwa wazee humu riziki zenu zipotee na muwe na maisha magumu ambayo hakuna atayeweza kuyabadilisha hadi mfe
 
Kuna mzee mmoja huwa ananiomba nimsaidie kutoa hell zake huwa aninipa password yake kbsa pia Ana watot 3 ila hawaamini Yuko radhi anisubiri mpk nije ndio nikamletee hella nmb au mpesa anazotumiwa za mazao shambn kwake ..


Watot wake wa kike alinifata nimpe namb za Siri za Bab ake ila nimegoma siku hz wananichukia San yey na mam yake mzeee ananimbia nikijaribu kutoa password nitakufa namm nimeingia ofu mbaya Ana account mbili za nmb na crdb hyo ya nmb ndio zilizoingiza hzo pesion
Mzee yule alishakuwa mpk mkurugenzi wa halmashuri kadha hapa nchin

Kwa kweli kila nilifanya muahama wowote napata 20000 jus Kati ndio akanikunjia Mia mbili baada ya kumuelezea tatizo Langu
Endelea kuwa na Imani hiyo, endelea kuwa mwema na wala usije kutoa Siri zake wala usimuibie. Hizi familia zetu hasa mke anapokuwa mbabe maelewano Huwa yanakuwa hafifu. Watoto wa kike mara nyingi wakiingiziwa ujinga wa mama Yao mbabe Huwa ni changamoto sana sana.

Endelea kuwa mwaminifu kwake
 
Mi wazee nawaheshimu sana.
Kuna Bar Moja nilienda hapo tabata Aroma, kuangalia mishe ya umeneja wa Bar.

nikamkuta mzee mmoja anagonga konyagi yani yuko tungi aisee mida ya saa nne asubuhi..

Mzee yule nimemkuta meza za mwanzo kabisa nikamsalimia vizuri akaitika. Nikaenda counter nikawaambia nimeleta CV zangu kwa kazi flani.

Wakanipokea, nikakaa pale kama nusu saa nasubiri INTERVIEW.

Baada ya muda yule dada wa counter akaniita ananiambia mzee anakuita (yule niliemsalimia mwanzoni) kwa ajili ya interview.

Dah nilijiuliza maswali mengi sana endapo ningempita bila salam ingekuwaje.

mzee tukasalimiana tena akaniomba vyeti na barua, akatazama pale huku anasifia.

Hapo hapo akaniambia You are my new Bar manager[emoji3062][emoji3062][emoji28][emoji28][emoji28]

Jamani nilifurahi sana! nimekula laki 3 tatu hapo na posho miezi mitano nashukuru mpaka sasa nina mtaji wa Biashara
Weka picha au ni chai???
 
Kuna watu huwa nawashangaa wanamponda MO eti hela za urithi,urithi kwa kizazi chako ni kitu chema,unakata mnyororo wa umasikini
Sifa kuu ya koo au familia maskini kila mtu huanza sifuri kujenga maisha yake ndio maana umaskini ni endelevu kwenye hizo koo au familia.Za matajiri wanaojielewa hawaanzii zero wanarithi
 
Si wanasemaga malaika anaweza kuja kwa dizain nyingi kukupima .....shauri yako
 
Kuna roli nilisoma nyuma,eti "Ukiwa kijana mvivu,itakuja kuwa mzee msumbufu"Sasa naona Kama inataka kufanana na huu Uzi......Mimi sipishi mwanamke mwenye mtoto Wala mimba...mzee inategemea na uchovu wa mwili wangu na urefu wa safari
 
Back
Top Bottom